Pascal Mayalla
Platinum Member
- Sep 22, 2008
- 57,135
- 128,774
Mkuu JME, nimekusaidia kidogo kwenye maeneo niliko weka red!, jina rasmi la Pengo ni Muadhama Policarp, Kardinali Pengo.Kunapofanyika makosa, tunatumia sheria mbili, jinai, na madai (criminal na civil), criminal mshitaki ni jamhuri, na kwenye civil mshitaki ni aliyeadhirika!. Kwenye hili Pengo hajashitaki popote hivyo hata akisamehe, msamaha wake haizuii jamhuri kuendelea na uchunguzi wake wa kijinai!.Kanisa Katoliki ni moja ya madhehebu ambayo yako very strict kwenye kufuata sheria, taratibu na kanuni, na linapokosema na mtu ambaye sii muumini, huweza kutoa msamaha kama huu kirahisi rahisi tuu kwa maana kwa mujibu wa kanisa, huyo Gwajima ni kama mtu tuu wa mataifa hajui atendalo!. Angekuwa ni Mkatoliki ingempasa kuungama, na kupewa adhabu ya kutimiza malipizi!.PascoAskofu Mkuu wa Jimbo Kuu la Dar es Salaam Mwadhama Polycarp, Kardinali Pengo amesema amemsamehe Mchungaji Gwajima na wote walioguswa .ameyesema hayo wakati wa ibada ya leo Jumapili katika kanisa la St. Joseph amesema "naomba niseme kutokana na hali iliyopo kuwa kutoka moyoni kabisa nimesamehe yote yaliyosemwa na naomba tumuombee na kuwaombea wote walioguswa sina kinyongo chochote"waumini walilipuka kwa makofi baada ya kusikia kauli ya Mwadhama.My take:Niishauri serikali kuachana na Gwajima madam Mwadhama ametamka tena huku akiwa amekalia kiti cha kiaskofu kwa sisi Wakatoliki nadhani tunajua maana ya tamko linapotolewa huku askofu akiwa amekalia kiti chake maana yake Mungu ameupokea msamahasource Mimi mwenyewe nilikuwepo kwenye misa