Pengo: Nchi imeoza!

Pengo: Nchi imeoza!

Nyaraka kaama hizo si ngeni kutoka toka kuanza chaguzi za vyama vingi. Lakini hii yaonekana yaonekana kukilenga chama tawala kwa muono wa Serikali ambayo i sawa na kusema CCM kwa sasa hivi. Kwa baadhi wameenda mbali zaidi na kuona kuwa, waraka huo si tu unailenga CCM, bali ni Rais Kikwete na washabiki wake serikalini kwa kuonekana kutolisikiliza kanisa katoliki kama ilivyokuwepo kwa akina Nyerere na Mkapa.

Wataalamu wa mambo ya siasa, wameeleza kuwa nguvu au ushawishi wa kanisa katoliki ndani ya serikali umepungua sana. Na hii imetokana na Kikwete kutaka kutenganisha kabisa dini na serikali kwa vitendo kitu ambacho kitakuwa kipya kabisa toka tukiwa Tanganyika na hatimaye Tanzania. Kwa maana hali hiyo ilirithiwa toka kwa wakoloni na kupewa baraka zote na mataifa ya magharibi.

Kikwete aliweza kuwashinda kidiplomasia akina Pengo na wafuasi wake, na ndio maana wakathubutu kutamka kuwa Kikwete ni chaguo la Mungu. Rais Kikwete alijua wazi kuwa kuna gharama kubwa ya kulipa kwa kuungwa mkono na makanisa yote. Ni vipi alijiandaa na hilo, hakuna ajuaye isipokuwa waliyekaribu naye tu. Kwa vile yeye ni mkongwe wa siasa wa muda mrefu, ninahakika kabisa anaelewa Nguvu na ushawishi wa kanisa Katoliki duniani. Tena liko tayari hata kuleta vita pale ambapo linaona kuwa linapoteza umaarufu, kwa nia ya kujipanga upya.

Waraka wa Katoliki ni mzuri, lakini inaonekana tunadandia dandia bila kujua undani wake. Inaonekana hata Waislam wamedandia dandia kwa kufuata mkumbo tu bila kujua undani. Angalieni ya Uganda! Mbuyu ulianza kama mchicha jamani.
 
Haya mambo yanahitaji tafakuri ya hali ya juu sana ili kuyaelewa.Yawezekana wengi hatujausoma huo waraka na tunajibizana kutokana na jinsi vyombo vya habari vinavyoandika au wanasiasa wanasemaje na mbaya zaidi kila mtu anatoa hoja akitokea upande anaodhani yeye uko sahihi. Kwa kuusoma na kuujadili waraka huo kwa pamoja tunaweza kujibu Maswali mengi bila hata kuhitaji msaada wa mtu mwingine.Ninasisitiza ili tuwe analytical tuusome waraka huo kwa makini tujue Wakatoliki (AU WAKRISTO in general kama wengine wanavyosema) wana hoja gani ndani yake.

Hebu fikiria sisi tuliosogeza madarasa mbele kidogo tunashindwa kuutafsiri je wale ndugu zetu wengine tuliwaacha madarasa ya nyuma kidogo itakuwaje?Tuusome na tuwasaidie wengine kuujua vizuri kama utatusaidia tuudumishe na kama utatutgawa basi wakatoliki/Wakristo tutawauliza kwa nini wanataka kutugawa.

Mungu awe nanyi Daima

Anayetaka kuusoma tena na tena huu hapa:








BARAZA LA MAASKOFU KATOLIKI TANZANIA


(TEC)













MPANGO WA KUHAMASISHA


HUDUMA YA KICHUNGAJI KATIKA JAMII


KUELEKEA UCHAGUZI MKUU 2010















Idara ya Kichungaji


TUME YA HAKI NA AMANI - TEC



MPANGO WA KUHAMASISHA HUDUMA YA KICHUNGAJI


KATIKA JAMII KUELEKEA UCHAGUZI MKUU 2010



DIRA

Mungu anakuita, anakuhitaji.
Dunia imeumbwa na Mungu ili iendelee kuwa mahala panapodhihirisha Ufalme wa wake. Ukuu wa uumbaji huu ni mwanadamu ambaye ndiye kiumbe aliyekirimiwa utashi na uelewa ili awe mshiriki na mdhamini wa kazi ya Mungu. Mungu ametuchagua tuchukue wajibu huu, na pamoja naye tupunguze uovu na taabu, na kujenga dunia ambamo upendo na maelewano vinamhakikishia kila mmoja kufurahia utu wake.

Kama wakristo, tunapokea mwaliko wa Kristu uwe mwaliko wetu. "Roho wa Bwana yu juu yangu, kwa maana amenitia mafuta kuwahubiri maskini habari njema. Amenituma kuwatangazia wafungwa kufunguliwa kwao, na vipofu kupata kuona tena kuwaacha huru waliosetwa, na kutangaza mwaka wa Bwana uliokubaliwa" (Lk 4: 18 – 19).
Kwa kutilia mkazo mwaliko huu, tunaelezwa kuwa Mwana wa Mtu atakaporudi atayahukumu mataifa kwa kigezo cha huduma tuliyotoa kwa wenye njaa, kiu; walio wageni, uchi, wagonjwa na wale walio kifungoni (rej. Mt. 25: 31 – 46).

Mungu alipomuumba Mwanadamu alimpa wajibu wa pekee, sio tu kuwa mlinzi na mdhamini wa dunia/uumbaji, bali pia kuwa mshiriki katika kuumba, na kutunza. Ni wito wa kushirikiana na Mungu katika kupambana ili kuuondoa uovu katika jamii yetu na kujenga ulimwengu ambamo kila mmoja ana wajibu wa kutekeleza na wakati huo huo ana haki ya kufurahia matunda ya dunia yetu.

Programu yetu ya kulihamasisha Kanisa kutekeleza wito wa kichungaji katika mambo ya kijamii ni kuwatia moyo waamini wote kutambua na kukubali wito wao wa Kikristo, wito wa kuwapelekea watu habari njema ya Yesu katika mambo ya kijamii na ya kitaifa. Kutakatifuza malimwengu, kuifanya nchi yetu na watu wetu kuishi pamoja huku manufaa ya kila mmoja yakiwa yanatimizwa: kupata huduma msingi za maisha na kuheshimiwa utu wa kila mmoja. Hapa maslahi na manufaa ya wote na ya kila mmoja katika jamii yanapaswa kuzingatiwa. Huu ni wajibu wa kila mmoja.

Mungu anakuhitaji, haya si maneno tu, bali ni uamuzi wa makusudi wa Mungu anayetukabidhi wajibu huu. Kutopokea mwaliko huu unaotoka kwa Mungu ni kushindwa kutimiza wajibu wetu, ni dhambi ya kutotimiza wajibu wa wito wetu wa Kikristo. Wito wa kutimiza wajibu wa kijamii, ambao ni kutia chachu ya tunu za injili na Mafundisho ya Kristo katika masuala na shughuli za kijamii, kiuchumi na kisiasa ya taifa letu.
Wito huu haujaeleweka vema na jumuiya zetu. Watu wengi wanadhani kwamba mambo ya umma sio sehemu ya majukumu yetu ya kidini na kiimani, na hivyo Kanisa halipaswi kujishughulisha na mambo hayo. Kinyume chake Kristo anatualika kuleta mafundisho ya Mungu, maadili ya asili yetu ya kibinadamu kama tulivyoumbwa na Mungu. Tunaalikwa kuyafanya hayo yawe ndio msingi na mwanga unaoongoza maamuzi na sera zetu.

Tunaona kwamba ikiwa maadili hayo yatakuwa sio msingi wa maisha yetu ya pamoja na kuyashuhudia katika utendaji wetu na mienendo yetu, hapo tutaingia haraka katika uovu na ubinafsi na uchoyo, mambo ambayo yanaangamiza jamii yetu.

Katika miaka ya hivi karibuni sote tumeshuhudia haya yakitokea na tumepata madhara yake katika amani na utulivu katika taifa letu. Kumekuwa na mgawanyiko miongoni mwetu, kumejengeka matabaka ya wenye mali nyingi na watu wengi ambao wana mali kidogo sana, maskini na fukara hasa . Mwelekeo huu unatishia na kuhatarisha amani na moyo wa ujamaa tuliokuwa nao na kushamiri kwa utengano na chuki kati yetu.

Sote tunawajibika kwa nchi yetu na taifa letu. Ndio maana Mungu ametujalia sote kuenzi hadhi ya utu wetu sawa. Kwa hiyo tusiruhusu nchi yetu Tanzania ikawa na watu ambao thamani ya utu wao ni zaidi ya wengine. Tusisahau kila mmoja wetu ameumbwa katika sura na mfano wa Mungu (Taz. Mwa 1: 2.

Ni kwa sababu hiyo tunazindua programu hii ya kuhamasisha jumuiya zetu kuelewa wito wao wa kijamii, kuinjilisha na kuifanya jamii yetu iwe ya kiutu kulingana na mpango wa Mungu wa uumbaji na haswa kwa jamii ya wanadamu. Msingi wa utu wa mwanadamu ni asili yetu ya kwamba tumeumbwa na Mungu. Huu ndio msingi ambao dini zote zinausadiki na kuuheshimu. Kwa hiyo tunaweza kushirikiana na waislamu, wahindu, na watu wenye kufuata dini za jadi. Sote kwa pamoja tujenge dunia yetu kulingana na mpango wa Mungu.


WITO

Tumetumwa katika jumuiya zetu, Parokia na jumuiya ndogo ndogo, kuwahamasisha watu wafanye tafakari juu ya hali halisi ya maisha na kujua ni kwa namna gani mafundisho ya Kanisa na Injili yanatupatia mwanga wa namna ya kuboresha maisha yetu na katika Taasisi za jamii yetu. Tunachukua hatua katika kurekebisha mambo yanayokwenda vibaya na kuimarisha mambo mazuri. Ni mwaliko wa kuwasaidia watu katika kutekeleza maamuzi yaliyothibitishwa katika ahadi yao waliyoweka wakati wa ubatizo.

Hatua zifuatazo zinapendekezwa kutumika katika utekelezaji:
- Kuchunguza hali, kutambua na kubaini tatizo.
- Kutumia Mwanga wa mafundisho ya Kristo na kutoka katika Mafundisho ya Kanisa kuhusu Jamii.
- Kuamua hatua ya kuchukua na namna ya kufuatilia utekelezaji.


UTARATIBU WA KUZINGATIA (METHODOLOJIA)

Programu hii ya kichungaji inahitaji uongozi mzuri na hatua madhubuti za ufuatiliaji. Hapo tutaweza kufanikiwa na kuleta matokeo katika maisha ya Jumuiya ya Kanisa na ya taifa letu.

Katika hatua ya utekelezaji wa programu hii tunapendekeza:

1) Kufanyika mikutano ya makleri na viongozi wa halmashuri walei. Ni lazima katika mkutano huu ijadiliwe programu hii katika ngazi ya Jimbo na kupewa umuhimu unaostahili.
2) Wajumbe wa Mkutano huu: Wakurugenzi wa Kichungaji na Wajumbe wa Tume ya Haki na Amani watakuwa wakufunzi – kueleza na kufafanua mada za programu yetu.
3) Katika kazi ya kuongoza mkutano (no. 1), wajumbe wa CPT na wawakilishi wa Serikali waalikwe kutoa maelezo juu ya hali halisi pale watu wanamoishi.
4) Inapendekezwa paundwe timu ya Jimbo kwa ajili ya ufuatiliaji wa programu hii.
5) Katika ngazi ya Parokia programu ilenge kufundisha wanavijiji/watu mitaani na katika Jumuiya Ndogo Ndogo ili waweze kujadili masuala yaliyomo katika programu.
6) Ripoti za majadiliano hayo zitumwe Parokiani (Paroko na Halmashauri) kila baada ya miezi mitatu. Ripoti hizo zionyeshe mambo yaliyojadiliwa na maamuzi yaliyofikiwa.

Kwa kupata uelewa zaidi mada zilizojadiliwa katika mkutano wa Wakurugenzi wa Kichungaji na Wajumbe wa Tume ya Haki na Amani (TEC) ni:
1) Vipaumbele kwa mujibu wa Mafundisho ya Kanisa kuhusu Jamii.
2) Umuhimu wa uongozi wenye maadili katika kuleta mabadiliko ya kijamii, kiuchumi, kisiasa na kidini katika Tanzania.
3) Mfumo wa Sheria Tanzania: Nguvu na Changamoto.
4) Haki za Binadamu katika sera za biashara na fedha.
5) Mtazamo wa kimaadili katika mfumo wa kisiasa na kiuchumi.
6) Hifadhi ya jamii.

Mada hizi zinapatikana kwa kiswahili na kiingereza, kama unazihitaji wasiliana na:
- Ofisi ya CPT - St. Josephs Cathedral Dar es Salaam
Tel: 022-2127675/0713-329984
E.mail: cptprofessionals@yahoo.co.uk

Tunaweza pia kukusaidia kupata Katiba ya Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania ikiwa utatujulisha mahitaji yako.

MADA KUU ZA TAFAKARI



Agenda hizi ndizo zilizoazimiwa katika Mkutano wa Wakurugenzi wa Kichungaji na Wajumbe wa Tume ya Haki na Amani TEC uliofanyika tarehe 20 – 22 Januari, 2009.

1. UTU
Utu aliokirimiwa kila mwanadamu bado haujawa ndio kiini na msingi wa mienendo yetu kama watu binafsi, katika vikundi na kama jamii. Kasoro hii tunaiona katika jumuiya za kidini, katika mila, desturi na tamaduni zetu, katika shughuli zetu za kiuchumi na katika uwanja wa kisiasa.

Kila mwanadamu ana utu sawa na utu wa mwingine na kwa hiyo lazima utu wa kila mmoja uheshimiwe na wengine: watu binafsi, taasisi na utawala. Ikiwa mwanadamu anapewa hadhi kutokana na utu wake, na haki zake atajengeka na kuwa na utu kamili, na yeye mwenyewe atajenga uwezo wake kikamilifu.

Vile vile bila kufanya hivyo jamii yetu haiwezi kamwe kukua na kuwa jamii yenye watu wenye kuenzi ukweli, utu na usawa. Kuigawa jamii katika matabaka ni kosa na ni dhambi, licha ya kuwa huko ni kuzuia jamii kufikia uwezo wake kamili na kuwa jamii yenye furaha. Katiba ya Jamuhuri imeweka bayana kwamba haki, wajibu na uhuru wa binadamu lazima vilindwe, viheshimiwe na kutolewa sawa kwa wote.

Kwa hiyo tunapaswa kufundisha watu dira hii katika:

- Ngazi ya familia, katika ujirani na Jumuiya ndogo ndogo. Ni hapa ndipo msingi wa jamii na kanisa unapojengwa.
- Katika mashule, tuangalie upya sera zetu za elimu na malezi na upande wa kimaadili tuchunguze yaliyo katika mitaala na ratiba katika mashule. Kwa sasa hakuna msisitizo wa kutosha katika malezi ya ubora/sifa za kiutu.
- Katika mambo ya kisiasa na kiuchumi: heshima na utu wa mtu sio suala la kubaki katika maneno na hotuba nzuri na matamko. Taasisi na sheria zetu lazima zikumbuke kuwa kanuni za kimaadili yapasa ziongoze kazi yao.
- Katika ngazi za Kanisa: mkazo zaidi uwekwe katika kuwajenga watu katika mambo ya kiroho ambayo ni ya lazima katika kuongoza tabia ya kijamii. Hapa ni zaidi ya kuweka kanuni na taratibu. Kinachohitajika hasa ni roho ya kiinjili na wito wa kinabii.

Mambo yanayopendekezwa kufanywa katika kufundisha na kuhamasisha utu ni:
- Mafungo katika ngazi ya Parokia na taasisi za Kanisa.
- Mikutano na wazazi ili kuwahamasisha na kutafakari namna ya kufundisha maadili katika ngazi ya familia.
- Semina na Waalimu.
- Kujadili na mamlaka ya elimu ngazi ya wilaya na mkoa.
- Tathmini ya kiroho ili kupima mambo ya kiroho na kupendekeza dhamira za kichungaji ambazo zinaweza kutumika katika mahubiri na miongozo ya katekesi.
- Kufanya utafiti katika ngazi ya Parokia ili kujua nini vijana wanapendelea na kutafuta njia ya kuwajengea hadhi ya utu wao kwa kutumia mambo yanayowavutia vijana.
- Kuchunguza vitabu vinavyotumika mashuleni kama vinahimiza au vinachochea maadili mema.


2. UONGOZI
Dira
Suala la uongozi ni pana. Kuna aina nyingi za uongozi (kiroho, kiutamaduni, kielimu, kiutawala, kisiasa, kiuchumi). Vile vile zipo ngazi mbalimbali za uongozi (familia, ujirani, vijiji, taasisi, kidini, kitaifa). Uongozi unahitaji watu wenye sifa ya huduma, wanaojali, walio wazi, wanaowajibika, wanyenyekevu, wenye hekima na upendo. Uongozi kila mara unashawishika kutenda kinyume na hayo na kuwa na uchoyo na kutumia madaraka vibaya. Kwa hiyo ni muhimu kuandaa viongozi, kushirikiana nao na kushikamana nao na kuwadhibiti kwa lengo la kuwasaidia kuwa jasiri walio waaminifu katika kazi zao.

Hali yetu inadhihirisha kuwa:
- Katika miaka ya hivi karibuni tumeona matatizo mengi ya uongozi. Kwanza kabisa yapasa tujadili kiini chake na kisha tutafute tiba yake.
- Katika uwanja wa kisiasa tunapaswa kuangalia namna wagombea wa na vyoteuliwa na vyama vyao. Tunahitaji kutafuta taarifa ya njia na vyanzo vya upatikanaji wa fedha za vyama vya siasa na namna wanavyozitumia. Watu wajadili kama mfumo wa uwakilishi kiuwiano (proportional representation system) haungeweza kuwa bora kuliko ule wa sasa. Kuna haja kubwa pia ya kusaidia watu kuijua Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
- Ni lazima katika mambo ya kijamii tuwahimize watu kueleza matatizo wanayokumbana nayo katika maisha yao na kuyatolea taarifa katika ngazi ya Parokia hadi Jimbo/Wilaya. Tuwasaidie kushiriki katika utawala tangu ngazi ya Serikali za kijiji/mitaa hadi ngazi ya halmashauri ya wilaya na kutafuta taarifa kisha kufuatilia nini watumishi wa umma wanafanya katika kuhudumia watu. Njia nzuri ni kuanza na kundi mahalia kushughulikia matatizo ya hapo walipo.
- Katika Kanisa tuhimize watu kutoa maoni yao katika Jumuiya ndogo ndogo na kusaidiana kuwa waaminifu katika wito wa Kikristo. Jumuiya ya Kanisa ni mahala ambapo mtu anakuwa na nafasi ya kutimiza wajibu wake wa kushiriki vilivyo katika shughuli za jumuiya. Hiarakia ya Kanisa haimaanishi kuwa ni kutoa amri tu kwa watu wa ngazi ya chini, bali kazi ya Hiarakia ni kuongoza namna ya kutimiza ahadi tuliyoweka wakati wa ubatizo.

Kwa agenda hii tunapendekeza:

Katika ngazi ya kisiasa: kuunda timu ya CPT na wajumbe wa halmashauri kutengeneza maswali maalum, kuendana na hali mahalia, watu wajadili na ili kutoa mawazo na maoni mazuri, wapatiwe habari zinazohitajika kwa ajili ya tafakari. Hapa tusiwape nafasi wale ambao ni wagombea wa kisiasa kutawala mjadala.

Kijamii: Watu watafute ni mashirika gani yapo hapo na huduma zipi hutolewa, na wangeweza kupata msaada gani katika kutatua matatizo yao. Ni taarifa gani tunapaswa kuwapatia watu ili waweze kufanya tafakari katika Jumuiya ndogo ndogo.

Kanisa: Tunawezaje kuimarisha tafakari katika jumuiya juu ya namna Parokia inavyoendeshwa. Halmashauri inafaa iwe chombo ambamo tathmini hiyo inaweza kufanyika. Ikumbukwe Parokia sio chombo cha utawala, bali lazima iwe ni jumuiya hai ya kusaidiana katika kuleta ubora wa maisha ya kiimani, matumaini na mapendo. Kwa pendekezo hili tufanye tathmini ya kiroho katika dhamiri na kuweka ahadi ya uwajibikaji katika kuwa zaidi mashahidi wa ujumbe wa Kristo katika hali halisi ya Tanzania leo.

3. HAKI

Dira
Lazima mfumo wa sheria uwe ni kwa ajili ya jumuiya ya watu katika kulinda na kudumisha amani, ukweli, haki, uhuru, mshikamano na usalama. Mfumo huu unapoleta ukosefu wa haki, watu wanapoteza imani nao.

Tutafute:
- Kwa njia gani tutawasaidia watu kujua haki zao na kuelewa sheria zinazoathiri maisha yao.
- Kuona kama shule zetu zinafundisha Katiba ya nchi na umuhimu wake.
- Tuone kama Wabunge wanawasiliana na majimbo yao na kuwa kweli wawakilishi wao. Kujadili kama wanadhibiti ya kutosha utendaji wa serikali. Ni kwa vipi watu wanapeleka masuala yao katika vyombo vya serikali na kusikilizwa?
- Mahakama za mwanzo zinahudumia watu wengi lakini ziko katika hali mbaya. Je, tunaweza kuziboresha vipi?
- Watu wanaona adhabu zinatolewa kwa makosa madogo, lakini wenye makosa makubwa, wanaachwa tu. Kwa nini watu wanafikiri hivi?
- Lazima tufikiri njia mbadala ya kutoa adhabu na kuona wafungwa kama watu wenye haki pia. Vile vile kutambua kuwa lengo la magereza ni kujenga amani na kurekebisha watu waliofanya makosa.
- Kila mara mfumo wa sheria unafanya kazi taratibu na hivyo watu husubiri mno haki kutendeka. Kukosa ufanisi na utaratibu wa utekelezaji vinasababisha ukosefu mwingi wa haki. Tunawezaje kuboresha hali hii?
Katika mjadala tulenge kuona kwamba "Mamlaka za siasa zichaguliwe na uamuzi wa hiari wa raia, nazo lazima zijali kanuni ya "utawala wa sheria," ambamo ukuu ni wa sheria na si wa matashi ya watu wasio na sheria."1

4. BIASHARA NA FEDHA

Dira
Hizi ni taasisi za biashara na fedha na shughuli nyingine zinazotoa huduma katika jumuiya. Biashara zinazotoa mahitaji ya vitu/bidhaa na kubadilishana na bidhaa hizi. Taasisi za fedha zinatunza thamani ya fedha, kwa kuweka kiwango cha kubadilisha fedha.

- Katika biashara, motisha haipaswi kuwa katika faida tu. Biashara inawafikishia watu bidhaa, hivyo isiendeshwe kiunyonyaji.
- Ni vipi tunaweza kuwasaidia watu kutetea maslahi yao na kuzuia wasinyonywe.
- Moyo wa ushirika umepungua mno na matokeo yake watu wameathiriwa na biashara zilizokosa uwaminifu. Tunawezaje kusaidiana.
- Mfumo wetu wa benki unafikisha huduma kwa watu wachache tu, na hasa kwa watu wa mijini na kwa wale wenye kiwango kizuri cha kipato. Lazima tusaidiane, hasa wale ambao hawana kipato cha kutosha, kuunda SACCOS na vikundi vya kusaidiana. Kanisa lazima lifanye bidii kuhamasisha hayo.
- Wachache walio katika mamlaka au katika nafasi za juu za utawala wana marupurupu mengi mno. Tusukume kupunguziwa hayo ili wawe na maisha ya kawaida.
- Tuwe makini na uporaji wa ardhi unaofanywa na makapuni makubwa na watu binafsi, matajiri. Tukumbuke ardhi ni ya thamani na ni hitaji la lazima kwa kila mmoja.
- Rushwa katika biashara, huduma duni, bidhaa duni vinaleta sifa mbaya, na hii ni tabia iliyo dhambi. Miongoni mwa watu hali hii inawajengea hasira na kukosa uaminifu na vile vile watu hujitetea kwa nguvu na kujengea watu fikra ya kulipiza kisasi.
- Udanganyifu katika biashara ni kushusha sifa mmiliki kwa wateja.
- Serikali iwe makini katika kuweka mikataba na wawekezaji wa umma na watu binafsi. Imekwishabainika kuwa katika mikataba hiyo maslahi ya wananchi hayalindwi kikamilifu badala yake wawekezaji hupewa unafuu mkubwa kwa kisingizio kuwa ni kivutio kwao.
- Makapuni ya ndani ni lazima yatiwe moyo na kuungwa mkono ili yaweze kuboresha utendaji wao uwe wenye tija.


5. UCHUMI.

Dira
Uchumi ni kwa ajili ya kuhudumia watu ili wawe na maisha mazuri: wapate mahitaji msingi na walindwe dhidi ya hali zinazowakuta na kutishia usalama wao na majanga mengine yanayoadhiri ubora wa maisha. Maadili katika shughuli ya kiuchumi na kuhakikisha mahitaji haya muhimu katika kumpatia mtu maisha mazuri yanapatikana. Sera za kiuchumi ni lazima ziweke kipaumbele kwa kuzingatia maadili na hivyo kufikia manufaa kwa wote na kulinda utu wa kila mmoja. Kwa hiyo tujadili pamoja na kama jumuiya za kanisa ni lazima tujifunze kuhimiza mahitaji yetu yazingatiwe na wenye maamuzi. Maoni yetu yasikilizwe na kufanyiwa kazi, tunu za kikristo tunazosimamia zionekane katika sera na katika mgawanyo wa bajeti ya serikali.

- Tunaweza kupunguza umasikini kwa kiasi kikubwa katika nchi yetu ikiwa watu wataelewa wajibu wao na kushiriki katika kutatua matatizo yetu: kwa mfano: kushiriki katika namna ya kupata huduma ya maji vijijini, namna ya kudhibiti matumizi ya fedha zinazotumwa katika serikali za mitaa.
- Ni kwa njia gani madiwani watafikisha maombi ya watu wao katika mgawanyo wa bajeti ngazi ya wilaya.
- Je, matumizi katika serikali ngazi ya chini yanawekwa wazi kwa wananchi kujua?
- Wabunge na viongozi katika ngazi ya Mkoa wanatoa fursa ya watu kuwauliza na kuwaeleza mahitaji yao? Tunawezaje kuboresha hali hiyo?
- Je, wakristo wetu wanazielewa fursa zilizopo; huduma zinazotolewa na serikali, mipango ya kusaidiana kama SACCOS, MVIWATA, vyama vya ushirika, jitihada za TASAF. Kwa nini wakristo wetu hawafanyi bidii kuanzisha vikundi/mipango ya kusaidiana? Pia parokia zetu ziwajibike vema katika kujenga ushirikiano na kujenga uwajibikaji wa kijumuiya ili kuboresha maisha.
- Kwa nini watu wetu hawaaminiani? Na tunawezaje kujenga moyo wa uaminifu miongoni mwetu?
- Kwa nini wakristo wetu wanaogopa kuzungumza na wenye mamlaka na walio katika huduma za utawala ili kupeleka malalamiko na kufuatilia utekelezaji wa maamuzi yaliyofanyika. Pia tutafakari namna ya kupambana na tabia ya uvivu.
- Tuna mali nyingi, lakini kila mara tunasubiri "wengine " au "Serikali" kufanya kitu au kutuletea fedha. Lazima tujifunze kutumia vipaji vyetu na uwezo wetu katika kutafuta ufumbuzi wa matatizo yetu. Kusaidiana kwa kuunganisha nguvu zetu na uwezo wetu ni wajibu wa kikristo. Mungu ametupa vipawa, lazima tuvitumie.
- Umaskini wa fikra, umaskini wa utashi duni na uwajibikaji ndio hasa husababisha umaskini. Ni kwa vipi jumuiya ya wakristo wanaweza kuwa mahala pa uwajibikaji ili kuweza kuboresha hali yetu.


6. HIFADHI YA JAMII

Dira
Mungu ametujalia uhai na anatupa mwaliko wa kutunza maisha na kuongeza ubora wa maisha. Mungu pia anatutaka kujali kwa namna ya pekee watu wasio na uwezo katika jamii yetu: yatima, wajane, walemavu, wagonjwa, watoto wa mitaani na wazee.

Hifadhi ya jamii maana yake ni kuweka mipango ya kuwahakikishia watu mahitaji na huduma ili wasiishi katika hali ya kukosa hifadhi/ usalama. Tunapozungumzia hifadhi ya jamii haswa tunamaanisha mifuko ya pensheni, elimu, bima ya afya na misaada ya kijamii.

Watu wengi miongoni mwetu hawafikiwi na huduma hii na familia zao zinakwama wanapoingia katika kuhitaji huduma hizo. Tunapaswa kuwa na mtazamo fikiriki ili kuweza kupata njia za kusaidiana. Mipango rasmi iliyoanzishwa na serikali au mashirika ya umma ama makampuni binafsi zinawafikia watu wachache tu ambao ni kama asilimia sita (6%) ya kundi la wafanyakazi.
- Jumuiya ndogondogo wangeweza kuwa chombo cha kusaidiana katika mahitaji ya kila siku ya wanajumuiya wao. Tunawezaje kuzifanya jumuiya zetu zitimize wajibu huu?
- Kutoaminiana ni kikwazo kikubwa katika kuwa na mipango na mifuko endelevu ya jumuiya. Tunawezaje kujenga moyo wa uaminifu? Viongozi wazuri walio tayari kuhudumia wanawezaje kupatikana na tutawawajibishaje viongozi wabovu?
- Lazima tutafute taarifa juu ya huduma na fursa zilizopo. Katika ngazi ya Parokia iundwe timu kwa ajili ya kutafuta taarifa na kuzifikisha katika Jumuiya ndogo ndogo. Taarifa hizo ni pamoja na zihusuzo mfuko wa afya ya jamii, sera ya serikali juu ya karo ya shule, sheria zinazohusu huduma ya tiba kwa mama na mtoto, wazee.
- Katika jamii yetu kuna watu walemavu wengi: Takwimu zinaonyesha kuwa walemavu ni 10% ya watu wote. Hawa ni wenye ulemavu wa namna moja ama nyingine. Kwa kawaida wahitaji hawa wanabaki kutegemea wanafamilia wao wachache, hasa mama au bibi. Kundi hili ndio maskini kupindukia kwa sababu jitihada za kuwainua ni ndogo sana.

Tatizo hili sio rahisi kulitatua. Lakini kwa kutegemea mifumo rasmi ya hifadhi ya jamii tu haitoshi na huduma hii kwao haitakuwa endelevu. Kwa hiyo tunapaswa kutafuta njia ambazo misingi yake ni katika njia za kizamani za kusaidiana, tuzitumie katika mazingira yetu ya leo kwa namna ya kisasa. Wazo hili linaweza kutekelezekaje?



 
Mimi nsons hii sio issue ya kuzungumzia watu wenye uweleo wenu. MIMI NAONA PENGO NA WENZAKE NI WANAFIKI SANA. NA KAMA WAO WAWAZI BASI WAJITOSE DHAHIRI KUGOMBEA UONGOZI WA SIASA KAMA ALIVYOFANYA DR SLAA NA MCHUNGAJI RWEKATARE AU HATA ALIVYOFANYA KAKOBE KUMPIGIA WAZI DEBE MGOMBEA MMOJA WA SIASA AWE KIONGOZI.
 
Kweli kabisa wewe ni DOGMA!Kati ya hao walioandika huo waraka na huyo Mwanya(PENGO) ni nani kila kukicha anausemea huo waraka?

Nimeamini unaweza ukamaliza madarasa hata mwalimu kufa darasani bila ya kuelimika!Maskini wee,yaani unatia aibu kutetea utumbo!Huko katoliki hakuna demokrasia leo anayetetea hiyo demokrasia atokee katoliki!Maajabu,mbona askofu Malasusa tumemchagua wenyewe hapa bongo?Na ndio maana utagundua viongozi wote wa kidini wanaoteuliwa au kuchaguliwa nje ya nchi yao ni watumwa wa mabeberu hao wa nje kwa ajili ya utashi wao binafsi.Hata ufanye vipi hutaweza kujitakasa na maji ya ******.

Umetaka ndio hivyo hukutaka ndio hivyo,huko hakuna kitu toka njoo huku lutheran au nenda anglican kwani demokrasia inapatikana na si kuletewa mamluki toka roma

maneno sawa kabisa, Huyu Pengo anafanya kazi zake zote kwa maarisho toka Vatican.

sasa apeleke waraka wake vativan na sio Tz
 
Kwa juhudi kubwa umejaribu kujadili mtu badala ya ujumbe anaouleta. Kuishiwa hoja kwako kwa namna hii kunaitwa ad hominem.

Pili unasahau kuwa msingi wa hoja zote hizi ni waraka wa wakatoliki kuelekea uchaguzi wa 2010. Waraka huu umeandaliwa na wataalamu wakatoliki, na sio maaskofu kama kichwa chako kidogo kinavyoshindwa ku-grasp, hivyo wote mnaoushambulia waraka na kuuhusisha na Pengo au yeyote kwa namna moja mnadhihirisha mlivyo na vichwa vigumu na mlivyo mahodari wa kudandia matreni kwa mbele, ila sisi wenye busara tunawaangalia tu mkipiga makasia pasipo na maji.

Acha uwongo wewe.

je unajuwa kuwa Pengo ni mkuu wa kanisa katoliki tanzania? pili unajuwa pengo amechaguliwa kushika wadhifa huo na Pope wa vatican. tatu unajuwa Pengo anamwakilisha Pope wa vatican hapa Tz.

sasa elewa kila kinachofanywa na kanisa katoliki hapa Tz lazima kipate baraka toka vatican,

sasa kama hao wataalamu wa kikatoliki wapo makini kwanza wangejadili demokrasia ndani ya kanisa lao kabla kuingilia demokrasia za nchi yetu.
 
..Waraka umepata umaarufu baada ya wanasiasa, haswa wa CCM, kuanza kuupinga.

..Muongozo wa Shura ya Maimamu naona haujaleta malumbano kama huu wa Wakatoliki kwasababu wanasiasa sasa wanaelekea kuwa wamejifunza kwa kutoupinga au kuuzungumzia.
 
Ni kweli kanisa katoliki lilitaharuki baada ya kugundua Kikwete na serekali yake walikuwa na mpango kuwaifanya Tanzania kuwa Jamhuri ya Kiislam kupitia OIC na kuanzishwa mahakama ya Kadhi.Tusisahau wakristo kwa ujumla wao [walutheri,wasabato,waanglicana na wapentecoste]hawakujua ujanja wa serekali ya kuanzishwa kwa mahakama ya kadhi ingawa ilikuwa ni sehemu ya ilani ya CCM.

Serekali inaweza ikafikiri inapambana na kanisa katoliki pekee lakini ukweli wa mambo itakuwa ikipambana na wakristo wa madhehebu yote na pengine inaweza kuitumbukiza Tanzania katika mgogoro mkubwa kuliko tunavyofikiri.Kikwete anajua hili ndiyo maana hawezi kumwona Pengo mwenyewe kwa kuwa anajua dhambi na hila za serekali yake dhidi ya kanisa.Kikwete alilitumia kanisa kufika hapo alipo,ni huyu huyu Pengo na maaskofu wa madhehebu karibu yote walikuwa wakituambia muungwana ni chaguo la Mungu.

Kikwete kwa maoni yangu anayo karata moja ya kucheza nayo ni kumtumia Mizengo Pinda ambaye ni mkatoliki safi kutuliza mambo kabla hayajaaribika kabisa.Tatizo hapa je Pinda atakubali kutumika kama daraja au naye atataka kutumia fursa hii adimu kama mtaji wake wa siasa hasa kupewa nafasi na chama kugombea urais baada ya muungwana mwaka 2015.



Kujiunga na OIC au kuwa na Mahakama ya Kadhi sio kuwa ndo nchi imeshakua ya kiislam! hapa nyie wakristo ndo mna-mis point. lakini wakiristo wenye akili wanaelewa tafauti hizi. Kuna nchi nyingi duniani zimejiunga na OIC na zina Kadhi court na bado ziko secular sasa nyie wakiristo wa Bongo mkiondoa uvivu wa kufikiri mtaelewa
 
Mkuu Zawadi imekuwa nongwa katoliki kutoa waraka mbona waislam wametoa wakwao tena kwa mbwembwe kubwa pale mnazi moja.Waraka wa kanisa katoliki hauwezi kuzuiwa na wanasiasa wanaowafuga na kuwalelea mafisadi,waraka wa kanisa katoliki ni jibu sahihi kwa serekali iliyokuwa tayari kuvunja katiba ili kuanzisha mahakama ya kadhi na kujiunga na OIC.

Ni upumbavvu kujaribu kusahau au kutokujua kwa makusudi prime reasons behind waraka wa kanisa.utawala uliopo uliingia kwa njia batili!!! viongozi wengi wa dini hawakujua hili, baada ya kujua ile disrepancy ya BOT ilivyofadhili ushindi huo,hakuna kiongozi yeyote wa dini alie makini atakaa anyamaze!!!

Reaction ya kanisa ni halali kabisa!!!sehemu zingine utawala huu ungeshatolewa siku nyingi na uchaguzi mpya ulishafanyika tayari!!!

Waandishi wengi wa tz ni illiterates na short sighted!! ndio maana wanahongwa hata plate ya ubwabwa ili kumpamba mtu!! na hasa walioko dar!!
 
Ni kweli kanisa katoliki lilitaharuki baada ya kugundua Kikwete na serekali yake walikuwa na mpango kuwaifanya Tanzania kuwa Jamhuri ya Kiislam kupitia OIC na kuanzishwa mahakama ya Kadhi.Tusisahau wakristo kwa ujumla wao [walutheri,wasabato,waanglicana na wapentecoste]hawakujua ujanja wa serekali ya kuanzishwa kwa mahakama ya kadhi ingawa ilikuwa ni sehemu ya ilani ya CCM.

Kweli tunaoelekea ni kubaya....kwa mawazo kama haya!!!!


Serekali inaweza ikafikiri inapambana na kanisa katoliki pekee lakini ukweli wa mambo itakuwa ikipambana na wakristo wa madhehebu yote na pengine inaweza kuitumbukiza Tanzania katika mgogoro mkubwa kuliko tunavyofikiri.

Mkuki kwa Mwislamu kwa Mkristo mchungu....wakati Serikali inapambana na "uchochezi" wa waislamu ilikuwa sawa na wala hakujaweza kuitumbukiza Tanzania katika migogoro lakini sasa imeshwakuwa hivi...Yaani akifanya uchochezi Sheikh PONDA serikali ina haki ya kuchukua hatua, akifanya Kadinali Pengo serikali haina haki wala wajibu wa kulishughulikia na zaidi inataka kuitumbukiza Tanzania katika migogoro..


Kikwete anajua hili ndiyo maana hawezi kumwona Pengo mwenyewe kwa kuwa anajua dhambi na hila za serekali yake dhidi ya kanisa.Kikwete alilitumia kanisa kufika hapo alipo,ni huyu huyu Pengo na maaskofu wa madhehebu karibu yote walikuwa wakituambia muungwana ni chaguo la Mungu.

Nakubaliana nawe 100%

Kikwete kwa maoni yangu anayo karata moja ya kucheza nayo ni kumtumia Mizengo Pinda ambaye ni mkatoliki safi kutuliza mambo kabla hayajaaribika kabisa.

Ni kweli PINDA ni mkatoliki mnyenyekevu lakini hili la UKATAOLIKI SAFI sijui ni vigezo gani unavitumia....unaweza kutuhabarisha zaidi?

Tatizo hapa je Pinda atakubali kutumika kama daraja au naye atataka kutumia fursa hii adimu kama mtaji wake wa siasa hasa kupewa nafasi na chama kugombea urais baada ya muungwana mwaka 2015.

Pinda kuongelea suala hili kama alivyofanya bungeni na hakuna aliyeaanz kumtukana na kumkejeli kama wanavyofanyiwa wasio wakatoliki ni jukumu lake kwa serikali na taifa lake. Kama ulivyosema, ni Pinda ndiye anaeweza kulishughulikia hili suala kwa mafanikio zaidi kuliko wengine lakini hilo ni jukumu lake kama waziri mkuu tuache kuanza kuspin mambo kufurahisha misimamo yetu iliyojaa USISI na UWAO....

omarilyas
 
Nilifikiri MWONGOZO wa waislamu ambao ulitolewa kwa mbwembwe, kwa kusema wao watapiga kura maslahi, ungepoza mjadala wa waraka wa wakatoliki kumbe wapi, kumbe alikuwa ni chui wa karatasi tu! Hata hivyo inawezekana waislamu kwa sababu walianza kuu-criticize waraka wa wakatoliki isingewezekana all of a sudden wakageuza mawazo eti kwa kuwa kuna waraka wao! Pamoja na hayo yote juhudi za mara kwa mara za marais waislamu kutaka kuisilimisha nchi zitafikia mwisho hasa pale wakristo watakapoungana wote dhidi ya islamization! Waislamu kwa upande wao huwa wakishindwa kwa hoja huwa wanatafuta njia ya mapigano! All in all viongozi wa kiislamu wasipoacha islamic agenda wakati wa uchaguzi watatufikisha pabaya: kama Lebanon alivyodai kikongwe Kingunge!
 
Sipendi kuamini ujumbe wa waraka ni wa hatari hata kidogo. Hebu soma nukuu hii kutoka katika waraka:
"...Tuna mali nyingi, lakini kila mara tunasubiri “wengine “ au “Serikali” kufanya kitu au kutuletea fedha. Lazima tujifunze kutumia vipaji vyetu na uwezo wetu katika kutafuta ufumbuzi wa matatizo yetu. Kusaidiana kwa kuunganisha nguvu zetu na uwezo wetu ni wajibu wa kikristo. Mungu ametupa vipawa, lazima tuvitumie..."

Yaani kuwaambia waumini msikae kama magolikipa ndio italeta mtafaruku wa kitaifa! Nukuu nyingi zina mwelekeo huu wa kuwahimiza waumini na naamini watanzania wote kujituma ili kuondokana na umaskini. Mleta hoja Zawadi ameogopa kunukuu waraka, anataka kuujadili kiujumla jumla, kama kawaida ya Kingunge.
 
Kujiunga na OIC au kuwa na Mahakama ya Kadhi sio kuwa ndo nchi imeshakua ya kiislam! hapa nyie wakristo ndo mna-mis point. lakini wakiristo wenye akili wanaelewa tafauti hizi. Kuna nchi nyingi duniani zimejiunga na OIC na zina Kadhi court na bado ziko secular sasa nyie wakiristo wa Bongo mkiondoa uvivu wa kufikiri mtaelewa
Fumbo mfumbie mjinga mwenye akili huling'amua!! Wakristo siyo wavivu wa kufikiri kama unavyotaka kutusadikisha.
 
Pamoja na hayo yote juhudi za mara kwa mara za marais waislamu kutaka kuisilimisha nchi zitafikia mwisho hasa pale wakristo watakapoungana wote dhidi ya islamization! Waislamu kwa upande wao huwa wakishindwa kwa hoja huwa wanatafuta njia ya mapigano! All in all viongozi wa kiislamu wasipoacha islamic agenda wakati wa uchaguzi watatufikisha pabaya: kama Lebanon alivyodai kikongwe Kingunge!

Ukumbuke kuwa hao unaowaita viongozi wa waislamu bila ya kutaja makundi yao nao pia wapo wenye fikira punguwani kama zako kuwa Nyerere na viongozi wengine wakriso wamekuwa wakichristianize Tanzania lakini hadi sasa bado hatujafika kama walipo hao wa Lebanon. Kitu ambacho kitawezekana kabisa kufikiwa hivi karibuni kama tutaendelea na huu ujinga wa hao tunaowaona kuwa wapo sawa kutua hizo Waraka na Miongozo yao na matamshi ya kinafiki kama yanayoendelea.

Tusipoangalia kuna kila uwezekano watanzania wakapiga kura kufuata makundi yao ya kidini katika uchaguzi ujao kama ambavyo wabunge wao wameshaanza kuonyesha mifano....

omarilyas
 
Yawezekana usemavyo i kweli, lakini ujumbe alioutoa Kingunge safari hii umewafikia wengi. Nahii haitokani eti kwa vile aliyesema ni Kingunge, bali ni kutokana na utata wa waraka wenyewe. Yabidi uhudhurie j'pili kanisani ili uusikilize waraka huo, sasa hii ni nchi gani?

Na ndio maana waislamu nao wakatoa wao. Siamini kama waislam huko nyuma walikuwa na nia ya kutoa waraka kama huo, ila hii ilikuwa ishara ya ushindani au uamsho kwa kundi jingine la imani.



Zawadi una kazi kubwa sana kupambana na kanisa wewe na watu wako . Kwanza naomba unijibu haya maswali .

1.Utata wa waraka uko wapi kiasi kwamba wewe na Kingunge na Kikwete muanze kuhaha namna hii ?

2.Je una uhakika kwamba issue hii ni ya Pengo na JK ? Waraka kauandika Pengo ? Na JK anakujaje kwa upande wa pili ?
 
Ni kweli kanisa katoliki lilitaharuki baada ya kugundua Kikwete na serekali yake walikuwa na mpango kuwaifanya Tanzania kuwa Jamhuri ya Kiislam kupitia OIC na kuanzishwa mahakama ya Kadhi.Tusisahau wakristo kwa ujumla wao [walutheri,wasabato,waanglicana na wapentecoste]hawakujua ujanja wa serekali ya kuanzishwa kwa mahakama ya kadhi ingawa ilikuwa ni sehemu ya ilani ya CCM.

Serekali inaweza ikafikiri inapambana na kanisa katoliki pekee lakini ukweli wa mambo itakuwa ikipambana na wakristo wa madhehebu yote na pengine inaweza kuitumbukiza Tanzania katika mgogoro mkubwa kuliko tunavyofikiri.Kikwete anajua hili ndiyo maana hawezi kumwona Pengo mwenyewe kwa kuwa anajua dhambi na hila za serekali yake dhidi ya kanisa.Kikwete alilitumia kanisa kufika hapo alipo,ni huyu huyu Pengo na maaskofu wa madhehebu karibu yote walikuwa wakituambia muungwana ni chaguo la Mungu.

Kikwete kwa maoni yangu anayo karata moja ya kucheza nayo ni kumtumia Mizengo Pinda ambaye ni mkatoliki safi kutuliza mambo kabla hayajaaribika kabisa.Tatizo hapa je Pinda atakubali kutumika kama daraja au naye atataka kutumia fursa hii adimu kama mtaji wake wa siasa hasa kupewa nafasi na chama kugombea urais baada ya muungwana mwaka 2015.

Huu ni unafiki na uzushi usio mfano! Jee, Tanzania kujiunga na OIC na kuwa na Mahakama ya Kadhi ndio imeshageuka kuwa Jamhuri ya Kiislam? huo ni upumbavu wa hali ya juu.

Nchi ngapi duniani zina hizo Mahakama za Kadhi na wamejiunga na OIC mbona hazijawa Jamhuri za KiIslam?

Jirani zetu, Uganda na Msumbiji ni memba wa OIC na Kenya kuna Mahakama ya Kadhi, Jee ni lini ulizisikia zikawa Jamhuri za kiIslam?

Wacha upumbavu!
 
Mimi nsons hii sio issue ya kuzungumzia watu wenye uweleo wenu. MIMI NAONA PENGO NA WENZAKE NI WANAFIKI SANA. NA KAMA WAO WAWAZI BASI WAJITOSE DHAHIRI KUGOMBEA UONGOZI WA SIASA KAMA ALIVYOFANYA DR SLAA NA MCHUNGAJI RWEKATARE AU HATA ALIVYOFANYA KAKOBE KUMPIGIA WAZI DEBE MGOMBEA MMOJA WA SIASA AWE KIONGOZI.

Porojo tu hapa umeandika ili usogeze muda.
 
Ukumbuke kuwa hao unaowaita viongozi wa waislamu bila ya kutaja makundi yao nao pia wapo wenye fikira punguwani kama zako kuwa Nyerere na viongozi wengine wakriso wamekuwa wakichristianize Tanzania lakini hadi sasa bado hatujafika kama walipo hao wa Lebanon. Kitu ambacho kitawezekana kabisa kufikiwa hivi karibuni kama tutaendelea na huu ujinga wa hao tunaowaona kuwa wapo sawa kutua hizo Waraka na Miongozo yao na matamshi ya kinafiki kama yanayoendelea.

Tusipoangalia kuna kila uwezekano watanzania wakapiga kura kufuata makundi yao ya kidini katika uchaguzi ujao kama ambavyo wabunge wao wameshaanza kuonyesha mifano....

omarilyas


Nina kila mara maongezi yako upande wa waraka wa wakatoliki pekee na ule mwingine si waraka kwamba nao uongelewe hapa ?halafu naona tuna lalamika na kuulaumu waraka hivi jamani yaliyo andikwa mle kwenye waraka hayako Tanzania ?

Je kama vyama vya siasa havikuweza kuyasema cauase hawayaoni ina maana kwamba watu wengine wasiseme ?

Nimewah kusoma hapa hapa JF ikisemwa kwamba Waislam ni majority Tanzania kama ndiyo hivyo sasa kelele za nini si watakuwa overwhelmed kweney uchaguzi na kuwachagua CCM ugumu uko wapi ?
 
Huu ni unafiki na uzushi usio mfano! Jee, Tanzania kujiunga na OIC na kuwa na Mahakama ya Kadhi ndio imeshageuka kuwa Jamhuri ya Kiislam? huo ni upumbavu wa hali ya juu.

Nchi ngapi duniani zina hizo Mahakama za Kadhi na wamejiunga na OIC mbona hazijawa Jamhuri za KiIslam?

Jirani zetu, Uganda na Msumbiji ni memba wa OIC na Kenya kuna Mahakama ya Kadhi, Jee ni lini ulizisikia zikawa Jamhuri za kiIslam?

Wacha upumbavu!

nadhani ulisikia ushauri uliotolewa na balozi wa Kenya nchini Tanzania kuhusu mahakama za kadhi na jinsi zilivyo waletea matatizo. Halafu issue siyo mahakama, issue ni kwa nini waislamu walazimishe kwamba mahakama hizi ziendeshwe kwa kodi za wananchi ambao wengine siyo waislamu?? Hili ndo tunalolipinga.

Sasa hivi mmeruhusiwa muanzishe wenyewe na mziendeshe wenyewe mnaanza kulalama, sijui mnataka msaidiweje, na mmezidi kupenda vitu vya bure. Chuo kikuu mmepewa bure, huku wenzenu wanajenga kwa pesa ya sadaka na michango kidogo.
 
Ukumbuke kuwa hao unaowaita viongozi wa waislamu bila ya kutaja makundi yao nao pia wapo wenye fikira punguwani kama zako kuwa Nyerere na viongozi wengine wakriso wamekuwa wakichristianize Tanzania lakini hadi sasa bado hatujafika kama walipo hao wa Lebanon. Kitu ambacho kitawezekana kabisa kufikiwa hivi karibuni kama tutaendelea na huu ujinga wa hao tunaowaona kuwa wapo sawa kutua hizo Waraka na Miongozo yao na matamshi ya kinafiki kama yanayoendelea.

Tusipoangalia kuna kila uwezekano watanzania wakapiga kura kufuata makundi yao ya kidini katika uchaguzi ujao kama ambavyo wabunge wao wameshaanza kuonyesha mifano....

omarilyas

Wewe unayejidai una akili lakini unashindwa kuelewa kwa nini all of a sudden nchi imegawanyika kidini namna hii kwenye awamu hii kuliko wakati mwingine wowote! Nyerere pamoja na mapungufu yake yote aliwafanya watz kujiona kitu kimoja! Nilimsikia anayejiita Prof Lipumba kwamba kwa asili watz ni watu wa amani bila kujua kwamba amani iliyopo imetengenezwa na haijaja yenyewe!
 
Back
Top Bottom