Pengo: Nchi imeoza!

Pengo: Nchi imeoza!

apewe ''life-ban'' huyu!hana faida hapa jeiefu,zaidi ya udini


Hamna haja ya kumpa ban, unajua watu kama hawa wana wamafrustration kwenye maisha yao, usikute kaachika au mumewe ana-erectile dysfunction, n.k. sasa ndio hivyo hana jinsi ispokuwa kuleta mafrustration yao hapa jamvini badala ya kupata ufumbuzi wa kitabibu.

Unaweza kumsaidia kwa kumu-add kwenye ignore list, kama nilivyofanya.
 
MI naona Pengo agombee ubunge maana kaamua kuingia kwenye siasa, amesahau there must be separation of power between state and other institution though kuna check and balance lakini si kuingia ndani kiasi kwamba unaonekana unachochea malumbano kwa kigezo cha misimamo ya dini, kama mnataka kanisa kuingilia mambo ya siasa pelekeni mswada bungeni basi ujadiliwe, harakati zake can take him no where coz they lack merits
.

Maneno sawa kabisa. Kama kweli Pengo sio Mnafiki basi ajitose kama alivyofanya Dr Slaa au Mchungaji Rwekatare au awe kama Kakobe kumpigia mgombea yeyote yule debe wazi wazi
 
I am following this debate..However, if the same "tamko" of Polycap pengo was spoken by a Muslim Cleric he wold be branded as a terrrist..but christians are a privilaged lot in TZ i assume
 
I am following this debate..However, if the same "tamko" of Polycap pengo was spoken by a Muslim Cleric he wold be branded as a terrrist..but christians are a privilaged lot in TZ i assume

Sidhani kama hii ni kweli, Kila mtu ana haki sawa. Sijaona kama kuna upendeleo wa dini, Tanzania kuna tatizo moja la mgawanyo wa huduma za jamii na wapi kina nani wapo wengi. Hili linatakiwa serikali kuu ilipe kipaumbele ili kupunguza malalamiko. Na watu wengi wakiwa na elimu za juu sawa makazini watakuwa wengi wa kada mbali mbali na kupunguza hisia hasi dhidi ya dhehebu moja kwenda jingine.

Ila hapa ikumbukwe kila dhehebu, dini ina mfumo wake, kwani sio dhehebu zote za kikristo zina mfumo sawa na wakatoliki. Hawa wenzetu wanamfumo kama vile serikali kutoka chini kwenda juu. Ila ni wajibu wa kila dhehebu na dini kuangalia nini mahitaji ya kiroho ya waumini wake na kimwili kwani huwezi kuhubiria waumia wenye njaa, umasikini uliotukuka unazaa dhambi. na viongozi wezi ni baadhi ya waumini wenzenu hivyo ni wajibu wa viongozi wa dini kutoa makaripio kwani ni kazi yao kuponya roho. Wakati mwingi watu huogopa kuonekana wadhambi na mafisadi kwenye nyumba zao za ibada isipokuwa mkapa na chenge.
 
Yes but kumbuka Serikali haina dini ila walioko madarakani wana dini na wale wanaoongozwa nao wana dini zao. Na ndiyo maana kila mara baadhi ya viongozi wa kiserikali huwa wana"quote" vitabu vitakatifu. Hivi tatizo ni kilichosemwa AU aliyesema???? If we can not diferentiate the two, KILICHOSEMWA NA ALIYESEMA, we will be narrowing our minds. BY THE WAY, WHERE DO YOU DRAW THE church and state SEPARATION LINE???
Tena viongozi hao wa dola wanapoapa kutwaa madaraka wanashika vitabu vitakatifu vya dini (Biblia na Quran). Isitoshe wanaombewa na viongozi wa dini ili waweze kutenda kazi zao kwa unyoofu, busara, haki na kweli. Haya yote yanaonesha ni kwa jinsi gani Kanisa (dini) na dola zinavyokwenda pamoja. Kumbe wanapofanya vibaya wana sababu ya kuwaonya viongozi wetu kwamba wamekosea njia. Kwa nini wasionywe?

Kutenganisha Dini (Kanisa) na Dola haina maana ya Kanisa kutosema chochote kiovu kinachotendwa na dola, bali kunamaanisha Kanisa kutokuchukua mamlaka ya dola na kutawala badala ya mfumo uliowekwa na katiba; au Kanisa kuweka lenyewe viongozi wa dola badala ya wananchi. Lakini Kanisa halikatazwi kukemea viongozi wa dola, kuwasahihisha na kuwarudi pale wanapokuwa wamekwenda kinyume na maadili na amri wazi za Mwenyezi Mungu. Viongozi wa Kanisa kufanya hivyo siyo kwamba wanakuwa wanasiasa au wanakuwa wamechanganya Kanisa na dola, la hasha, bali wanakuwa wametimiza wajibu wao wa kinabii: kukemea maovu. Ndivyo walivyofanya hata manabii wa Agano la Kale. Waliwaonya na hata kuwakemea wafalme waliotelekeza raia wao na kujilimbikizia mali na kuwanyima haki wanyonge.

Kumbe siamini kama Mwadhama Pengo lengo lake ni kuwa mwanasiasa au anajaribu kuingilia dola katika mambo yake halali. Bali anachofanya ni hicho cha kukemea uozo uliokithitri katika jamii.
 
Waraka wa Katoliki juu ya kuwaelewesha wapiga kura juu ya uchaguzi wa 2010, umeonekana kama kitendawili kwa serikali. Aidha baadhi ya viongozi wa serikali hawajaomuonea aibu Pengo pamoja na wafuasi wake kumuanika hadharani na kumuomba auondoe waraka huo. Lakini hasa kulikoni ndani ya kanisa Katoliki?

Nyaraka kaama hizo si ngeni kutoka toka kuanza chaguzi za vyama vingi. Lakini hii yaonekana yaonekana kukilenga chama tawala kwa muono wa Serikali ambayo i sawa na kusema CCM kwa sasa hivi. Kwa baadhi wameenda mbali zaidi na kuona kuwa, waraka huo si tu unailenga CCM, bali ni Rais Kikwete na washabiki wake serikalini kwa kuonekana kutolisikiliza kanisa katoliki kama ilivyokuwepo kwa akina Nyerere na Mkapa.

Wataalamu wa mambo ya siasa, wameeleza kuwa nguvu au ushawishi wa kanisa katoliki ndani ya serikali umepungua sana. Na hii imetokana na Kikwete kutaka kutenganisha kabisa dini na serikali kwa vitendo kitu ambacho kitakuwa kipya kabisa toka tukiwa Tanganyika na hatimaye Tanzania. Kwa maana hali hiyo ilirithiwa toka kwa wakoloni na kupewa baraka zote na mataifa ya magharibi.

Kikwete aliweza kuwashinda kidiplomasia akina Pengo na wafuasi wake, na ndio maana wakathubutu kutamka kuwa Kikwete ni chaguo la Mungu. Rais Kikwete alijua wazi kuwa kuna gharama kubwa ya kulipa kwa kuungwa mkono na makanisa yote. Ni vipi alijiandaa na hilo, hakuna ajuaye isipokuwa waliyekaribu naye tu. Kwa vile yeye ni mkongwe wa siasa wa muda mrefu, ninahakika kabisa anaelewa Nguvu na ushawishi wa kanisa Katoliki duniani. Tena liko tayari hata kuleta vita pale ambapo linaona kuwa linapoteza umaarufu, kwa nia ya kujipanga upya.

Waraka umebabaisha toto kwa kusema imejikita katika kupinga ufisadi. Wasomi wanaona kama lugha nyepesi ya kidiplomasia waliyoitumia, lakini hasira zao ziliibuka pale Serikali ilipoanza mjadala wa OIC na Mahakama ya Kadhi. Hapa ndio ilikuwa mwisho wa urafiki kati ya kanisa katoliki na Rais Kikwete. Na hii ilimlazimu Pengo kufunga safari kwenda Vatikan na kupata ushauri toka kwa Papa. Pindi aliporudi tu, alimwita Waziri Membe na kufanya mazungumzo ya siri. Na hapo ndipo lilipochimbwa kaburi la Mjadala wa OIC na Mahakama ya Kadhi.

Hata hivyo kanisa katoliki halikurithika na hilo, ajenda kubwa ilibakia ni kumtoa madarakani Rais Kikwete kupitia wananchi (kura). Kwa katoliki hili ni suala la mpango wa muda mrefu (Long term). Hivyo si lazima Kikwete ang'oke mwaka 2010, bali hata hapo baadaye. Kwasababu nia si kumuondoa Kikwete peke yake bali ni yeye na wafuasi wake wote toka mikoani mpaka ikulu. Kazi amayo itafanyika toka kwenye vigango(ngazi ya chini ya uongozi wa kanisa) mpaka makao makuu ya katoliki.

Rais Kikwete kwa kulielewa hilo ikawatuma akina Kingunge na wafuasi wake kuupinga waraka huo hadharani. Bahati mbaya kukatokea makundi makundi ndani ya Serikali na Bungeni, huku baadhi wakiwa upande wa serikali na wengine upande wa Pengo. Moja kati ya viongozi wa juu waliokuwa upande waPengo ni pamoja na Spika wa Bunge Mh Samwel Sitta. Hili lilikuwa ni pigo kubwa kwa Serikali/CCM, hasa ukizingatia kuwa udini nao ukatawala Bunge na Serikali pia. Hapa ikaonyesha kuwa mahesabu ya Pengo yametimia.

Mpaka sakata hilo halijafika mwisho hatujui hatima yake. Lakini moja ni sahihi, kuwa michezo kama hii mwisho wake si mzuri na inaweza kuleta umwagaji damu. Ukimya wa KIngunge nyakati za hivi karibuni si dalili nzuri, kwani simba mwenda kimya ndio mla nyama.
 
Ni kweli kanisa katoliki lilitaharuki baada ya kugundua Kikwete na serekali yake walikuwa na mpango kuwaifanya Tanzania kuwa Jamhuri ya Kiislam kupitia OIC na kuanzishwa mahakama ya Kadhi.Tusisahau wakristo kwa ujumla wao [walutheri,wasabato,waanglicana na wapentecoste]hawakujua ujanja wa serekali ya kuanzishwa kwa mahakama ya kadhi ingawa ilikuwa ni sehemu ya ilani ya CCM.

Serekali inaweza ikafikiri inapambana na kanisa katoliki pekee lakini ukweli wa mambo itakuwa ikipambana na wakristo wa madhehebu yote na pengine inaweza kuitumbukiza Tanzania katika mgogoro mkubwa kuliko tunavyofikiri.Kikwete anajua hili ndiyo maana hawezi kumwona Pengo mwenyewe kwa kuwa anajua dhambi na hila za serekali yake dhidi ya kanisa.Kikwete alilitumia kanisa kufika hapo alipo,ni huyu huyu Pengo na maaskofu wa madhehebu karibu yote walikuwa wakituambia muungwana ni chaguo la Mungu.

Kikwete kwa maoni yangu anayo karata moja ya kucheza nayo ni kumtumia Mizengo Pinda ambaye ni mkatoliki safi kutuliza mambo kabla hayajaaribika kabisa.Tatizo hapa je Pinda atakubali kutumika kama daraja au naye atataka kutumia fursa hii adimu kama mtaji wake wa siasa hasa kupewa nafasi na chama kugombea urais baada ya muungwana mwaka 2015.
 
Kwa hakika kama kweli kanisa Katoliki linakusudia kufanya na kuwaelimisha waumini wao juu ya kiongozi bora ni bora kusema ukweli na pia jua kuwa siyo kanisa Katoliki lililosema kuwa JK ni changuo la Mungu bali ni makanisa ya WALOKOLE
 
Mkuu Zawadi Kingunge hana tena nafasi ya kusikilizwa na kanisa kwasababu approach yake tayari ilionyesha kejeli na dharau kwa kanisa na viongozi wake.Kikwete alimshauri vibaya Kingunge kutumia vyombo vya habari kulishambulia kanisa badala ya kuonana ana kwa ana na viongozi.

Kingunge wa leo si yule wa enzi za Mwl J K Nyerere,siku hizi hana tena heshima mbele ya jamii.Kingunge siku hizi amekuwa msemaji wa kundi la mafisadi anapojitokeza mbele ya jamii kuzungumza chote chote hata kama ni jambo la maana hakuna mtu mwenye akili timamu atakayemsikiliza.Ni dhahiri muungwana atakuwa amegundua amefanya kosa kubwa kupita kiasi kumtumia Kingunge ambeye ukatoliki umemshinda na hata ukomonisti aliouvamia pia umemshinda.
 
Kwa jinsi mjadala huu unavyokwenda ni kama wachangiaji wanakubali kuwa waraka wa wakatoliki unamaslahi ya kanisa ndani yake.Kinachotia hofu ni kitendo cha kanisa kujitosa hadharani tena kwa sura yake halisi kutetea kile inachoita maslahi yake.kwa kawaida muda utoa majibu ya maswali yote.Ngoja tusubiri tuone kwani ndo kwanza mpira uko golini kwetu.Tuombe uzima
 
Kwa jinsi mjadala huu unavyokwenda ni kama wachangiaji wanakubali kuwa waraka wa wakatoliki unamaslahi ya kanisa ndani yake.Kinachotia hofu ni kitendo cha kanisa kujitosa hadharani tena kwa sura yake halisi kutetea kile inachoita maslahi yake.kwa kawaida muda utoa majibu ya maswali yote.Ngoja tusubiri tuone kwani ndo kwanza mpira uko golini kwetu.Tuombe uzima
Sidhani kama Kanisa Katoliki lina maslahi binafsi kwenye huo waraka. Kama kuna kitu linachotetea ni maslahi ya watanzania, na hasa wanyonge. Mbona waraka uko wazi kwa hilo? Hauongelei dini bali unaongelea hali halisi ya matatizo ya jamii ya tanzania na jinsi ya kujinasua kwa kuchagua viongozi bora, nk.
 
Ni kweli kanisa katoliki lilitaharuki baada ya kugundua Kikwete na serekali yake walikuwa na mpango kuwaifanya Tanzania kuwa Jamhuri ya Kiislam kupitia OIC na kuanzishwa mahakama ya Kadhi.Tusisahau wakristo kwa ujumla wao [walutheri,wasabato,waanglicana na wapentecoste]hawakujua ujanja wa serekali ya kuanzishwa kwa mahakama ya kadhi ingawa ilikuwa ni sehemu ya ilani ya CCM.

Serekali inaweza ikafikiri inapambana na kanisa katoliki pekee lakini ukweli wa mambo itakuwa ikipambana na wakristo wa madhehebu yote na pengine inaweza kuitumbukiza Tanzania katika mgogoro mkubwa kuliko tunavyofikiri.Kikwete anajua hili ndiyo maana hawezi kumwona Pengo mwenyewe kwa kuwa anajua dhambi na hila za serekali yake dhidi ya kanisa.Kikwete alilitumia kanisa kufika hapo alipo,ni huyu huyu Pengo na maaskofu wa madhehebu karibu yote walikuwa wakituambia muungwana ni chaguo la Mungu.

Kikwete kwa maoni yangu anayo karata moja ya kucheza nayo ni kumtumia Mizengo Pinda ambaye ni mkatoliki safi kutuliza mambo kabla hayajaaribika kabisa.Tatizo hapa je Pinda atakubali kutumika kama daraja au naye atataka kutumia fursa hii adimu kama mtaji wake wa siasa hasa kupewa nafasi na chama kugombea urais baada ya muungwana mwaka 2015.
Kulikumbatia kanisa sio jibu, hasa ukitaka kuweka mipango ya muda mrefu. Hii itampa kazi hata kama Mizengi Pinda akifanikiwa mwaka 2015.

Kinachotakiwa ni kanisa Katoliki kukubai kujitune, na kuelewa kuwa Tanzania ya Nyerere si sawa na hii ya Leo. Watanzania wamekwenda shule na wanaitumia. Isitoshe vyombo vya habari viko huru, hivyo vinafikisha habari kwa wananchi kwa urahisi zaidi.

Yale maelezo kuwa ukila na kipofu usimshike mkono hayapo tena. Angali, Rais Habyarimana ALIYEKUWA RAIS WA Rwanda alilikumbatia kanisa. Na leo vyombo vyote vya west vimeligeuka.

Jibu wanalo akina Pengo. Nchi hii ni ya wote, w aislam, wakristo, wahindu na wapagani.
 
Ni kweli kanisa katoliki lilitaharuki baada ya kugundua Kikwete na serekali yake walikuwa na mpango kuwaifanya Tanzania kuwa Jamhuri ya Kiislam kupitia OIC na kuanzishwa mahakama ya Kadhi.Tusisahau wakristo kwa ujumla wao [walutheri,wasabato,waanglicana na wapentecoste]hawakujua ujanja wa serekali ya kuanzishwa kwa mahakama ya kadhi ingawa ilikuwa ni sehemu ya ilani ya CCM.

Serekali inaweza ikafikiri inapambana na kanisa katoliki pekee lakini ukweli wa mambo itakuwa ikipambana na wakristo wa madhehebu yote na pengine inaweza kuitumbukiza Tanzania katika mgogoro mkubwa kuliko tunavyofikiri.Kikwete anajua hili ndiyo maana hawezi kumwona Pengo mwenyewe kwa kuwa anajua dhambi na hila za serekali yake dhidi ya kanisa.Kikwete alilitumia kanisa kufika hapo alipo,ni huyu huyu Pengo na maaskofu wa madhehebu karibu yote walikuwa wakituambia muungwana ni chaguo la Mungu.

Kikwete kwa maoni yangu anayo karata moja ya kucheza nayo ni kumtumia Mizengo Pinda ambaye ni mkatoliki safi kutuliza mambo kabla hayajaaribika kabisa.Tatizo hapa je Pinda atakubali kutumika kama daraja au naye atataka kutumia fursa hii adimu kama mtaji wake wa siasa hasa kupewa nafasi na chama kugombea urais baada ya muungwana mwaka 2015.

Mkuu Zawadi Kingunge hana tena nafasi ya kusikilizwa na kanisa kwasababu approach yake tayari ilionyesha kejeli na dharau kwa kanisa na viongozi wake.Kikwete alimshauri vibaya Kingunge kutumia vyombo vya habari kulishambulia kanisa badala ya kuonana ana kwa ana na viongozi.

Kingunge wa leo si yule wa enzi za Mwl J K Nyerere,siku hizi hana tena heshima mbele ya jamii.Kingunge siku hizi amekuwa msemaji wa kundi la mafisadi anapojitokeza mbele ya jamii kuzungumza chote chote hata kama ni jambo la maana hakuna mtu mwenye akili timamu atakayemsikiliza.Ni dhahiri muungwana atakuwa amegundua amefanya kosa kubwa kupita kiasi kumtumia Kingunge ambeye ukatoliki umemshinda na hata ukomonisti aliouvamia pia umemshinda.
Yawezekana usemavyo i kweli, lakini ujumbe alioutoa Kingunge safari hii umewafikia wengi. Nahii haitokani eti kwa vile aliyesema ni Kingunge, bali ni kutokana na utata wa waraka wenyewe. Yabidi uhudhurie j'pili kanisani ili uusikilize waraka huo, sasa hii ni nchi gani?

Na ndio maana waislamu nao wakatoa wao. Siamini kama waislam huko nyuma walikuwa na nia ya kutoa waraka kama huo, ila hii ilikuwa ishara ya ushindani au uamsho kwa kundi jingine la imani.
 
Sidhani kama Kanisa Katoliki lina maslahi binafsi kwenye huo waraka. Kama kuna kitu linachotetea ni maslahi ya watanzania, na hasa wanyonge. Mbona waraka uko wazi kwa hilo? Hauongelei dini bali unaongelea hali halisi ya matatizo ya jamii ya tanzania na jinsi ya kujinasua kwa kuchagua viongozi bora, nk.

Kwa kuwa umesema haudhani hii ina maanisha kinyume chake pia inaweza kuwa kweli.Na kwa sababu hiyo tuwe na subra tuone mwisho wake utakuwa nini,ni suala la muda tuu.
 
Kulikumbatia kanisa sio jibu, hasa ukitaka kuweka mipango ya muda mrefu. Hii itampa kazi hata kama Mizengi Pinda akifanikiwa mwaka 2015.

Kinachotakiwa ni kanisa Katoliki kukubai kujitune, na kuelewa kuwa Tanzania ya Nyerere si sawa na hii ya Leo. Watanzania wamekwenda shule na wanaitumia. Isitoshe vyombo vya habari viko huru, hivyo vinafikisha habari kwa wananchi kwa urahisi zaidi.

Yale maelezo kuwa ukila na kipofu usimshike mkono hayapo tena. Angali, Rais Habyarimana ALIYEKUWA RAIS WA Rwanda alilikumbatia kanisa. Na leo vyombo vyote vya west vimeligeuka.

Jibu wanalo akina Pengo. Nchi hii ni ya wote, w aislam, wakristo, wahindu na wapagani.

Mkuu Zawadi imekuwa nongwa katoliki kutoa waraka mbona waislam wametoa wakwao tena kwa mbwembwe kubwa pale mnazi moja.Waraka wa kanisa katoliki hauwezi kuzuiwa na wanasiasa wanaowafuga na kuwalelea mafisadi,waraka wa kanisa katoliki ni jibu sahihi kwa serekali iliyokuwa tayari kuvunja katiba ili kuanzisha mahakama ya kadhi na kujiunga na OIC.
 
Kulikumbatia kanisa sio jibu, hasa ukitaka kuweka mipango ya muda mrefu. Hii itampa kazi hata kama Mizengi Pinda akifanikiwa mwaka 2015.

Kinachotakiwa ni kanisa Katoliki kukubai kujitune, na kuelewa kuwa Tanzania ya Nyerere si sawa na hii ya Leo. Watanzania wamekwenda shule na wanaitumia. Isitoshe vyombo vya habari viko huru, hivyo vinafikisha habari kwa wananchi kwa urahisi zaidi
Siamini kwamba kanisa katoliki limekumbatiwa na serikali au huko nyuma lilikuwa limekumbatiwa na serikali. Kanisa katoliki ni taasisi imara, yenye miundombinu ya ndani inayojitosheleza. Limekuwa mstari wa mbele kusambaza huduma mbalimbali za jamii: elimu, afya, nk. Kwa njia hii limeshiriki sana kwenye kuisadia serikali kutoa huduma kwa raia wa tanzania. Na kwa kuwa limejihusisha sana na huduma hizi za kimwili limekuwa karibu sana na serikali ambayo kazi yake si kutangaza dini bali ni kumhudumia mwanadamu kimwili (kuleta maisha bora kwa kila mtanzania).

Labda ni kutokana kushirikiana kwa karibu kati ya serikali na Kanisa katoliki katika huduma za jamii ndiyo maana baadhi ya watu kwa kutokujua wamedanganyika kwa kufikiri kwamba kanisa limekuwa likikumbatiwa na serikali. Si kweli! Dini na madhehebu yote (ya kikristo na ya kiislamu) yana nafasi sawa kabisa katika katiba ya nchi na mbele ya serikali. Sioni kivipi kanisa katoliki limetendewa kwa namna ya pekee (kupendelewa) kuliko dini au madhehebu mengine. Labda hapa tuelimishane.
 
Kulikumbatia kanisa sio jibu, hasa ukitaka kuweka mipango ya muda mrefu. Hii itampa kazi hata kama Mizengi Pinda akifanikiwa mwaka 2015.

Kinachotakiwa ni kanisa Katoliki kukubai kujitune, na kuelewa kuwa Tanzania ya Nyerere si sawa na hii ya Leo. Watanzania wamekwenda shule na wanaitumia. Isitoshe vyombo vya habari viko huru, hivyo vinafikisha habari kwa wananchi kwa urahisi zaidi.

Yale maelezo kuwa ukila na kipofu usimshike mkono hayapo tena. Angali, Rais Habyarimana ALIYEKUWA RAIS WA Rwanda alilikumbatia kanisa. Na leo vyombo vyote vya west vimeligeuka.

Jibu wanalo akina Pengo. Nchi hii ni ya wote, w aislam, wakristo, wahindu na wapagani.

usitolee mfano wa Rwanda, matatizo ya Rwanda siyo ya kidini na ulimwengu unajua hilo. Na kwa taarifa tu ni kwamba utawala wa kagame uko mashakani kwa sababu interahamwe are re-grouping now to fight back.

Hakuna nchi duniani ambapo wakatoliki waliwahi kuwa source ya vurugu, ila waislamu kwa sababu ya kuto elimika.
 
Haya mambo yanahitaji tafakuri ya hali ya juu sana ili kuyaelewa.Yawezekana wengi hatujausoma huo waraka na tunajibizana kutokana na jinsi vyombo vya habari vinavyoandika au wanasiasa wanasemaje na mbaya zaidi kila mtu anatoa hoja akitokea upande anaodhani yeye uko sahihi. Kwa kuusoma na kuujadili waraka huo kwa pamoja tunaweza kujibu Maswali mengi bila hata kuhitaji msaada wa mtu mwingine.Ninasisitiza ili tuwe analytical tuusome waraka huo kwa makini tujue Wakatoliki (AU WAKRISTO in general kama wengine wanavyosema) wana hoja gani ndani yake.

Hebu fikiria sisi tuliosogeza madarasa mbele kidogo tunashindwa kuutafsiri je wale ndugu zetu wengine tuliwaacha madarasa ya nyuma kidogo itakuwaje?Tuusome na tuwasaidie wengine kuujua vizuri kama utatusaidia tuudumishe na kama utatutgawa basi wakatoliki/Wakristo tutawauliza kwa nini wanataka kutugawa.

Mungu awe nanyi Daima
 
kwa mfano, uliwahi kuona wapi wakatoliki au wakristu wengine wanaandaa mhadhara wa kukashfu dini nyingine?? Haya utayakuta kwa waislamu, ukiwauliza ni nini kinawasukuma kuanzisha kashfa, utasikia tunaonewa na makafiri, wakati wao ndo wanaanzisha vurugu za kukashfu dini zingine, ili mradi tu ukijibu muanze mapigano.

mara OIC,..mara nini...yote hii ili labda wapapte vipesa vya bure kutoka kwa waarabu, hii ni ishara ya uvivu wa kufikiri na kufanya kazi. Ukienda uarabuni wataalamu wengi ni foreingers, vyenyewe mradi wana mafuta basi hayafanyi kazi kabisa sasa hiyo inaigwa sana na vishehe uchwara kwetu hapa, akiamka tu ni kanzu na kukaa barazani, hayo maendeleo utayapata wapi??? Mtaishia kulalama tu kila kukicha wenzenu wana kula kitabu kwa kwenda mbele.
 
Back
Top Bottom