omarilyas
JF-Expert Member
- Jan 24, 2007
- 2,130
- 151
Wewe unayejidai una akili lakini unashindwa kuelewa kwa nini all of a sudden nchi imegawanyika kidini namna hii kwenye awamu hii kuliko wakati mwingine wowote! Nyerere pamoja na mapungufu yake yote aliwafanya watz kujiona kitu kimoja! Nilimsikia anayejiita Prof Lipumba kwamba kwa asili watz ni watu wa amani bila kujua kwamba amani iliyopo imetengenezwa na haijaja yenyewe!
Unajua UDINI ni sumu mbaya sana. Yaani umeshajiona ni mtu wa kukejeli UProfessor wa Lipumba kwa kuwa yeye ni musilamu na huamini kwamba muislamu can make a qualified professor. Ninatofautiana sana na siasa za Lipumba na anaposema watanzania ni watu wa amani haina maana kuwa anadhani kuwa amani watanzania wamezaliwa nao. Imejengwa tena kwa kumwaga damu nyingi sana kwa upande wa waislam na wakristo wote. Lakini kukejeli USOMI wa Prof Lipumba mwenye rekodi iliyochukua milongo kadhaa kuvunjwa UDSM na hata kule Princeton ni upofu uliojaa prejudices.. Hizi prejudices ndio zinafanya watu wa aina yako, upande wa wakristo na waislamu pia kujenga mitizamo ambayo imejaa USISI na UWAO.....
Mnakumbuka utanzania pale tu inapoendana na maslahi yenu binafsi....
Hatujafika tulipofika all of the sudden....Huu ni muendelezo wa safari ndefu ya kubomoa utanzania ambayo wazazi wetu na sasa sisi wenyewe tunaiendeleza kutokana na prejudices tulizojazwa vichwani kuona sisi ndio wenye haki zaidi ya wengine just because either we are waislamu ama wakristo..