Pengo: Nchi imeoza!

Pengo: Nchi imeoza!

Huu waraka sio mara ya kwanza kutolewa, ule wa mwanzo haukuleta matatizo kama inavyosemekana yatakuja kusababishwa nao. Zawadi kama ungetaka kubalance story ungezungumzia hatari ya MWONGOZO wa waislamu hata kama umekuja baada ya waraka wa wakatoliki. MWONGOZO huo umeji-isolate zaidi kwamba wafuasi wake watapiga "kura maslahi." Sasa linganisha na waraka ambao unataka watu wachague viongozi waadilifu! Usipobalance story hata kama una pointi nzuri namna gani huna tofauti na wale ambao unawalaumu kimakosa kwenye thread hii huku na wewe unayafanya yaleyale, kwa maana hiyo unajihukumu mwenyewe!
Kimsingi mimi sitaki Taasisi, Jumuiya, mtu binafsi au NGO yeyote ile kutoa waraka au Muongozo juu ya kuwaelimisha wananchi kupiga kura. Nikifahamu wazi kuwa suala hili lipo very sensitive, bila ya kuangalia maudhui yaliyomo kwenye waraka au muongozo.

Katika hili suala la kwanza linalojitokeza ni nani kautoa huo waraka au muongozo. Lazima tufahamu kuwa kama Katoliki na waislam wanaweza kutoa waraka basi hata mtu binafsi akiwa na pesa zake anaweza kufanya hivyo. Hali kadhalika kwa NGO.

Hapa ni lazima ikumbukwe kuwa kila mmoja ana mawazo yake juu ya nani ni kiongozi mzuri. Kama waraka ungeandikwa na Mchungaji Mtikila angeandika waraka wake, basi ni wazi kuwa kigezo No 1 angeseama kuwa MAGABACHORI msiwachague kuwa viongozi. Tusingeweza kumkataza kwa sababu hivyo ndivyo afikiriavyo.

Ukiliona tatizo hili utakubaliana nami kuwa jukumu la kuwaelimisha wananchi kuwachagua wagombea waadilifu ni la serikali. Lazima tukumbuke kuwa hili ni jambo la kudumu na inabidi liwafikie wananchi wote kwa fedha ya walipa kodi.

Pamoja tuaendelea, tusikimbilie utatuzi wa harakaharaka. Dalili ya mvua ni mawingu.
 
hata kama waraka wao ungekuwa mzuri kiasi gani nitaupinga mbaka kufa,wao ni watu wa dini hivyo wanatakiwa kuwaandaa watu kiroho,wawaelimishe waumini wao namna ya kuishi ili wafike mbinguni na si vinginevyo ndio maana hata yesu alikataa kushugulikia mambo ya duniani hata kama utawala wa kiyahudi ulikuwa mbovu ingawa watu walijua yeye ndiye mfalme lakini yeye alisema hana shida ya ufalme wa duniani yeye ni mfalme wa mbinguni,sasa nyie mnaohangaika na mambo ya dunia ndo biblia ya wazungu ilivyowaagiza hivyo?
Uko sahihi kabisa, na hii ndio hatari ambayo wanaopinga waraka wa wakatoliki waliiona. Nafikiri wenzengu hapa JF mtamuelewa huyu mtoa hoja.

Tatizo si maudhui yaliyomo katika waraka. Tatizo ni imani ya mpokeaji kwa yule mtoa waraka. Hapa sizungumzii tu huu waraka wa katoliki au muongozo wa waislam, bali wowote ulr utaotoka nje ya serikali.
 
Kimsingi mimi sitaki Taasisi, Jumuiya, mtu binafsi au NGO yeyote ile kutoa waraka au Muongozo juu ya kuwaelimisha wananchi kupiga kura. Nikifahamu wazi kuwa suala hili lipo very sensitive, bila ya kuangalia maudhui yaliyomo kwenye waraka au muongozo.

Katika hili suala la kwanza linalojitokeza ni nani kautoa huo waraka au muongozo. Lazima tufahamu kuwa kama Katoliki na waislam wanaweza kutoa waraka basi hata mtu binafsi akiwa na pesa zake anaweza kufanya hivyo. Hali kadhalika kwa NGO.

Hapa ni lazima ikumbukwe kuwa kila mmoja ana mawazo yake juu ya nani ni kiongozi mzuri. Kama waraka ungeandikwa na Mchungaji Mtikila angeandika waraka wake, basi ni wazi kuwa kigezo No 1 angeseama kuwa MAGABACHORI msiwachague kuwa viongozi. Tusingeweza kumkataza kwa sababu hivyo ndivyo afikiriavyo.

Ukiliona tatizo hili utakubaliana nami kuwa jukumu la kuwaelimisha wananchi kuwachagua wagombea waadilifu ni la serikali. Lazima tukumbuke kuwa hili ni jambo la kudumu na inabidi liwafikie wananchi wote kwa fedha ya walipa kodi.

Pamoja tuaendelea, tusikimbilie utatuzi wa harakaharaka. Dalili ya mvua ni mawingu.

Serikali ni nini? labda tuanzie hapo
 
Kikwete alitumia kila mbinu kuupata uraisi wake!!!! Haikujalisha kama alikuwa anakiuka maadili tuliojijengea ya kuwa taifa moja!!!! Alitumia makanisa, misikiti, ukabila, rushwa, ghiriba za kila aina ili mradi tu aende magogoni.

Alikwenda makanisani kuzindua kanda za wanakwaya, aliwanunua waandishi wahabari wawaandike vizuri, maaskofu wakaibuka na chaguo la mungu!!!!! wamembadilikia sasa anataka kutafuta mchawi!!!!!

Waliposifiwa Wakinakingunge hawakupiga kelele, ila Mrema.....sasa wanawakosoa ndo wanang'aka.

Kanisa limeona mbali na kwakuwa lina mtandao mkubwa limeona lielimishe waumini wake, kwani vyama vya hiari, tume ya uchaguzi, na serikali yenyewe iko kimya kuwaelimisha wananchi jelimu ya urai na demokrasia kwa ujumla

Mwaka mmoja kabla ya uchaguzi kule Kenya, kampeni ya kuelimisha wapiga kura yalipamba moto mpaka mwezi mmoja kabla ya uchaguzi...sisi huku ni kutishiana na mapolisi, manajeshi na kadhalika...... wapo hao wanajiita usalama wa taifa but in real sense wao wanatetea chama cha kijani basi..wanashiriki kuiba kura, kuhujumu vyama vyenye mawazo tofauti na wao


Acha Pengo aelimishe wapiga kura ......
 
Hamukujibu hoja yangu.

Nimesema wapi ndani ya vitabu vyake 73 ameamrishwa kukemea maovu na munakimbilia logic, common sense, haki kama Raia. Nimedai reference ya kitabu nikiamini kwamba anaongozwa na Kitabu chake kwa kuwa yeye amezungumza kama kiongozi wa dini.

Kukwepa hoja yangu nadhani ni ushahidi kwamba hakuna linalomwarisha akemee uovu, kama lingekuwepo lingeletwa.

Kama majibu na misimamo ya viongozi wa dini yanatokana na common sense sasa muongozo wa vitabu una faida gani?

Kesho akija mwingine na common sense ikimwambia jibu ni kupindua Serikali kwa mtutu wa bunduki itakuwaje?

Umeuliza swali zuri. Kuna maxim inasema: "He who alleges must prove." Sasa wapi imeandikwa kwamba maovu yasikemewe? Kwa kuuliza swali lako, una maana kwamba kwenye hivyo vitabu 73 ulivyotaja hakuna sehemu hata moja inayosema maovu yakemewe na ndio maana unahoji kwa nini kakemea hayo maovu. Sasa lete mstari au aya kwa aya kwenye hivyo vitabu ututhibitishie kuwa maovu hayapaswi kukemewa!
 
- CCM wanapaswa kuukumbatia waraka, kwanza ni mzuri sana kwao kama wakiutimiza kama unavyoshauri, kama ni kushindana viongozi wao wangetumia muda huu wanaoupoteza kushidana na huu waraka kushindana na matatizo mengine sugu kwa taifa, kama usalama kwa wananchi.

- yaani sasa Tanzania imekua ni nchi ambayo huwezi tena kutembea usiku kama zamani utaishia kukabwa na majambazi, mimi ninakumbuka enzi zetu tulikuwa tunatoka Msasani Beach Disco kwa Ma-DJ John Peter Pantalakis na Choggy Sly usiku kwa mguu kurudi majumbani mwetu baada ya Disco, sasa haiwezekani tena maana utaishia kukabwa tu,

- Sasa hawa viongozi badala ya kuelewa kwamba taifa lenye wananchi wanaoishi maisha ya wasi wasi na productivity yao kwa taifa itakuwa ni ya wasi wasi pia, wao wako busy kushindana na waraka wa kanisa na huku wakiwa hawana hoja kabisaa, labda tuwakumbushe tu hawa viongozi wetu, ni kwamba kukosekana kwa uongozi imara wa taifa siku zote hupelekea hata makanisa kuingilia kati kujaribu kurekebisha udhaifu,

Sasa kama tuna viongozi wasiotaka kukosolewa basi watoke sasa wawaaachie wengine, maana haiwezekani wakaziba midomo ya kila mwanachi, wameanza kule NEC, na sasa wanajaribu tena kuyaziba midomo makanisa, sasa nani atakaye waongelea wananchi, nasema hivi viongozi wote waliochoka na wasiofaa wakumbushwe na kanisa au hata misikiti, kama hawataki kusikia watoke sio lazima tuongozwe nao wao tu, get out of there now waachieni wengine, au just shut up! we had enough already na serikali dhaifu!

- And yes I said it, serikali dhaifu!

Ahsante.

William.
 
Umeuliza swali zuri. Kuna maxim inasema: "He who alleges must prove." Sasa wapi imeandikwa kwamba maovu yasikemewe? Kwa kuuliza swali lako, una maana kwamba kwenye hivyo vitabu 73 ulivyotaja hakuna sehemu hata moja inayosema maovu yakemewe na ndio maana unahoji kwa nini kakemea hayo maovu. Sasa lete mstari au aya kwa aya kwenye hivyo vitabu ututhibitishie kuwa maovu hayapaswi kukemewa!

Sikusema imeandikwa maovu yasikemewe. Nimesema hakuna sehemu inayomuamuru muumini wa Biblia akemee maovu na ndio maana nimesema the one who can prove me wrong alete ushahidi.ia nimesema Paul ameamuru ndani ya Romans kwamba 'hakuna tena sheria ya righteousness'. Biblia pia inasema 'deeds are filthy rags' sasa kama wema na uadilifu ni filthy rags mbele ya Mungu kuna umuhimu na uhalali gani wa kuhubiri uadilifu?

Huwezi kuleta ushahidi wa kisichikuwepo, ushahidi huletwa kwa lililopo sio kwa kisichopo.

Kwenye thread nyingine kuna mchangiaji mwenye signature ya quotation ya Biblia ambaye pia amesema kwamba Yesu hakuhubiri worldly affairs. Anakiri kwamba the scope does not cover hayo ya Pengo na kuna dalili kwamba huyo ni muumini wa kitabu hichohicho.

Sasa wewe prove me wrong kwa kuleta amri ya kukemea maovu na kwamba aliyyoyakemea ni maovu kwa mujibu wa maandishi. Nipe maandishi yanayowapa waumini sifa za uongozi ili tuone kama hizo sifa katoa ndani ya kitabu ama maoni binafsi.

Kama hakuna Biblical writings zinazo support aliyoyasema kuna tofauti gani kati ya maneno yake na maneno ya Mrema, ama Slaa, ama Lowassa, ama Kingunge?
 
- CCM wanapaswa kuukumbatia waraka, kwanza ni mzuri sana kwao kama wakiutimiza kama unavyoshauri, kama ni kushindana viongozi wao wangetumia muda huu wanaoupoteza kushidana na huu waraka kushindana na matatizo mengine sugu kwa taifa, kama usalama kwa wananchi.

- yaani sasa Tanzania imekua ni nchi ambayo huwezi tena kutembea usiku kama zamani utaishia kukabwa na majambazi, mimi ninakumbuka enzi zetu tulikuwa tunatoka Msasani Beach Disco kwa Ma-DJ John Peter Pantalakis na Choggy Sly usiku kwa mguu kurudi majumbani mwetu baada ya Disco, sasa haiwezekani tena maana utaishia kukabwa tu,

- Sasa hawa viongozi badala ya kuelewa kwamba taifa lenye wananchi wanaoishi maisha ya wasi wasi na productivity yao kwa taifa itakuwa ni ya wasi wasi pia, wao wako busy kushindana na waraka wa kanisa na huku wakiwa hawana hoja kabisaa, labda tuwakumbushe tu hawa viongozi wetu, ni kwamba kukosekana kwa uongozi imara wa taifa siku zote hupelekea hata makanisa kuingilia kati kujaribu kurekebisha udhaifu,

Sasa kama tuna viongozi wasiotaka kukosolewa basi watoke sasa wawaaachie wengine, maana haiwezekani wakaziba midomo ya kila mwanachi, wameanza kule NEC, na sasa wanajaribu tena kuyaziba midomo makanisa, sasa nani atakaye waongelea wananchi, nasema hivi viongozi wote waliochoka na wasiofaa wakumbushwe na kanisa au hata misikiti, kama hawataki kusikia watoke sio lazima tuongozwe nao wao tu, get out of there now waachieni wengine, au just shut up! we had enough already na serikali dhaifu!

- And yes I said it, serikali dhaifu!

Ahsante.

William.

Ahsante sana WJM, tunahitaji watu wengi ndani ya chama tawala ambao siku zote watausema ukweli kama ulivyo na bila kutaka kuleta unafiki wa kuonyesha kwamba Kikwete na Serikali yake inafanya kazi nzuri. Hastahili huyu kupewa awamu nyingine, tuwe na utamaduni kuanzia 2010 vyama vya siasa viwe tayari kumwambia kiongozi aliyekuwa madarakani kazi imekushinda hivyo hustahili tena awamu nyingine badala ya kutaka kuleta za kuleta, "CCM tuna utamaduni wetu ndani ya chama ambapo mgombea wetu ni lazima akae madarakani kwa awamu mbili." Huu ni utamaduni wa kuupiga vita kwa nguvu zetu zote. Anayestahili kukaa madarakani kwa awamu mbili awe ni yule ambaye he/she has something to show off from his/her achievements during the 1st term in office and Kikwete has nothing to show off.
 
Last edited:
Wakuu, Dini ya kweli daima itahubiri binadamu kuwa mwema na kutotenda dhambi (uovu). Dini yatufundisha, "Mpende Bwana Mungu wako kwa moyo wako wote na kumpenda jirani yako kama unavyojipenda nafsi yako". Ukimpenda jirani yako huwezi kumwibia, huwezi kumsingizia uwongo na huwezi kumfanyia lolote lile kinaloweza kumdhuru au kumletea mateso.

Dini ya kweli inahubiri upendo katika jamii na upendo ni mwanga na ukiwepo, giza (dhambi) hutokomea na hata siku moja huwezi kuvichanganya hivi vitu viwili. Dini inayokaa kimya uovu ukitendeka katika jamii ni dini ya giza na kwa kufumbia macho vitendo hivyo, yenyewe inakuwa mshirika na haiwezi tena kuwa safi mbele ya Mwenyezi Mungu - ni dini ya kishetani.
 
Kwa mijadala kama hii inavyoshabikiwa, bado kuna watu wanaamini kuna siku tutakuwa na mijadala yenye tija kwa maendeleo ya taifa.

Inaonekana tulishapigwa muhuri.
 
Hamukujibu hoja yangu.

Nimesema wapi ndani ya vitabu vyake 73 ameamrishwa kukemea maovu na munakimbilia logic, common sense, haki kama Raia. Nimedai reference ya kitabu nikiamini kwamba anaongozwa na Kitabu chake kwa kuwa yeye amezungumza kama kiongozi wa dini.

Kukwepa hoja yangu nadhani ni ushahidi kwamba hakuna linalomwarisha akemee uovu, kama lingekuwepo lingeletwa.

Kama majibu na misimamo ya viongozi wa dini yanatokana na common sense sasa muongozo wa vitabu una faida gani?

Kesho akija mwingine na common sense ikimwambia jibu ni kupindua Serikali kwa mtutu wa bunduki itakuwaje?

Mzanganyika. Mbona katika vitabu hivyo unavyosema hakuna sehemu inayosema viongozi hao wasijenge SHULE,HOSPITALI NK mambo mengine ya kijamii lakini wamejenga vitu kama hivyo. Sasa hujui kuwa swala la ufisadi linahusu jamii vile vile. Jalibu kuwa OBJECTIVE ndugu yangu
 
Wakuu, Dini ya kweli daima itahubiri binadamu kuwa mwema na kutotenda dhambi (uovu). Dini yatufundisha, "Mpende Bwana Mungu wako kwa moyo wako wote na kumpenda jirani yako kama unavyojipenda nafsi yako". Ukimpenda jirani yako huwezi kumwibia, huwezi kumsingizia uwongo na huwezi kumfanyia lolote lile kinaloweza kumdhuru au kumletea mateso.
.

Sasa hii inamaanisha kwamba ni amri ya kupiga vita maovu?

Hiyo ilishabadilishwa na mengi yameandikwa kwamba sheria does not count anymore.

Romans 10:4 Christ is the end of the law so that there may be righteousness for everyone who believes.

Kama unaaamini tafsiri yangu sio sahihi nijulishe nilete ushahidi wa tafsiri niliyoitaja kwa mujibu wa wahubiri wenyewe.
 
Mzanganyika. Mbona katika vitabu hivyo unavyosema hakuna sehemu inayosema viongozi hao wasijenge SHULE,HOSPITALI NK mambo mengine ya kijamii lakini wamejenga vitu kama hivyo. Sasa hujui kuwa swala la ufisadi linahusu jamii vile vile. Jalibu kuwa OBJECTIVE ndugu yangu

Inategemea unazungumzia kitabu kipi.
 
Wakuu, Dini ya kweli daima itahubiri binadamu kuwa mwema na kutotenda dhambi (uovu). Dini yatufundisha, "Mpende Bwana Mungu wako kwa moyo wako wote na kumpenda jirani yako kama unavyojipenda nafsi yako". Ukimpenda jirani yako huwezi kumwibia, huwezi kumsingizia uwongo na huwezi kumfanyia lolote lile kinaloweza kumdhuru au kumletea mateso.

Dini ya kweli inahubiri upendo katika jamii na upendo ni mwanga na ukiwepo, giza (dhambi) hutokomea na hata siku moja huwezi kuvichanganya hivi vitu viwili. Dini inayokaa kimya uovu ukitendeka katika jamii ni dini ya giza na kwa kufumbia macho vitendo hivyo, yenyewe inakuwa mshirika na haiwezi tena kuwa safi mbele ya Mwenyezi Mungu - ni dini ya kishetani.

Romans 3:28 'A man is justified by faith without the deeds of the law.' Sasa kuhubiri mema na kukataza mabaya yawe kwa faida ya nani na kutii amri ya nani?Kama ni out of context pls put it in the right context and give me an opportunity to prove that my context is from preachers themselves.
 
Wakuu, Dini ya kweli daima itahubiri binadamu kuwa mwema na kutotenda dhambi (uovu).

Ni dini ipi unadhani waumini wake wameamriwa 'wakumbushane mema na kukatazana maovu'?

Ni dini ipi unadhani waumini wameambiwa wakiona maovu wayaondoe kwa mikono yao, ama wa condemn maovu ama kama wakishindwa basi wayachukie?
 
Ndugu yangu mzanganyika mi nadhani unachanganya mambo. Wewe umeisoma biblia na hukuielewa vizuri. Biblia inakataza matendo mabovu. Inatuongoza ili tutende mema. Hivyo, kukemea mabaya si tu suala la aya za biblia, bali ni kazi ya kila binadamu, awe ni mkatoliki au la, mwislamu au la, mlokole au la. Sasa nikuulize swali, je biblia haipingi ufisadi? Naomba unijibu.

Kuhusu Kardinali Pengo, mimi sio msemaji wake lakini naona kwamba walaka huu ni wa wakatoliki, je wewe ni mkatoliki? Kama sio sasa unaupingaje? Yaani pilipili ya shambani ambayo wewe haujaila inakuwashia nini? Unatakiwa uwe mkatoliki ili uelewe Kardinali alisema nini. Maana kanisa lina sheria na mafundisho yake. Halafu waraka ule si wa Kardinali peke yake ni wa wakatoliki wote. Sasa usimwonee tu Kardinale maana umepewa baraka na maaskofu wote wa kanisa katoliki.

Swali kwako ndugu yangu, nitajie ni sehemu gani ya waraka inayotishia amani, au iliyovunja sheria ya nchi? Halafu sasa tutafahamishana tu kwa kiustaarabu pale tunapotufautiana kati yetu.

Asante mdau, nasubiri hoja yako!
 
Last edited:
Swali kwako ndugu yangu, nitajie ni sehemu gani ya waraka inayotishia amani, au iliyovunja sheria ya nchi? Halafu sasa tutafahamishana tu kwa kiustaarabu pale tunapotufautiana kati yetu.

Asante mdau, nasubiri hoja yako!

Asante kwa changamoto.

Labda kwanza nianze kwa kukuomba ulete quote ya hapo niliposema waraka unatishia amani.

Nirudie tena msingi wa hoja yangu.
Mtu anaweza kuzungumza katika capacity tofauti. Angekuwa amezungumza kama Raia wa kawaida hapo angekuwa Raia kasema kama vile wewe, mimi, mwanasiasa na kadhalika.

lakini hapo kazungumza kama Kiongozi wa kanisa. Ninahoji, je aliyoyasema anaweza kuya support na maandishi?Nimeuliza wapi ameamriwa kupiga vita yale anayoyaona ni maovu.

Kama hana ulazima wa kuamriwa ili apige vita maovu kama walivyoashiria wengine pia haina tatizo, ili mradi 'isemwe wazi' kwamba maelekezo na mafundisho ya anayoyasema kama Kiongozi wa kanisa hayana ulazima wa kuwa supported na maandishi yake matakatifu. Kwa maana nyingine imani zake zinampa mamlaka ya kusema lolote hata kama anachosema hakina mwongozo huo ndani ya vitabu vyake.

Sina tatizo na content za waraka, nina question process and scope of what he can say and cannot say in his offcial capacity.

Angekuwa Rais tungesema katiba inamdhibiti. Kama Kiongozi wa Kanisa ni kipi kinachodhibiti matamshi yake?
 
Last edited:
Ndugu yangu mzanganyika mi nadhani unachanganya mambo. Wewe umeisoma biblia na hukuielewa vizuri. Biblia inakataza matendo mabovu. Inatuongoza ili tutende mema. Hivyo, kukemea mabaya si tu suala la aya za biblia, bali ni kazi ya kila binadamu, awe ni mkatoliki au la, mwislamu au la, mlokole au la. Sasa nikuulize swali, je biblia haipingi ufisadi? Naomba unijibu.

Na aya nilizoleta zinazosema kwamba righteousness does not count hazipo ndani ya Biblia ama nimetafsiri vibaya?

Nimeshasema niko tayari kuleta ushahidi wa tafsiri ninayoilelewa mimi na tafsiri hiyo imeandikwa na wahubiri wenyewe. Ukitaka nilete ushahidi unaweza kusema.
 
Serikali ni nini? labda tuanzie hapo
Serikali ni Watu, au Watanzania wote. Na ili kuwepo kwa utaratibu maalum wa watanzania wote kusikika kumewekwa utaratibu wa kuwachagua viongozi.

Uchaguzi wa viongozi toka madiwani, wabunge mpaka Rais ni muhimu sana, kwa maana hawa ndio wawakilishi wa wananchi katika maswala yote yanyohusu matatizo yao kwa kipindi cha miaka mitano.

Na Rais huchagua mawaziri ambao nao ni wabunge kwa nia ya kushirikiana nao katika kutatua matatizo ya wananchi. Hivyo kwa ujumla kiutendaji, hii ndio Serikali. Kwa vileimechaguliwa na watanzania wote ni muhimu kiustaarabu tuiheshimu na tuivumilie katika kipindi cha miaka mitano.

Kama tunadhani utaratibu huu wa kuchagua viongozi kwa njia hii ya Demokrasia sio mzuri, basi tuwe wazi na tueleze bayana ni utaratibu gani tunaupendelea. Au tuwe na viongozi waliochaguliwa Kanisani na Misikitini ndio wawe wabunge na maraisi ni uchaguzi wetu. Lakini lazima tuelewe kuwa nchi zetu za Afrika zinamchanganyiko tofauti wa kiimani, wakristo, waislam, wahindu wapagani n,k. Usije ukadhani kuwa watu wa imani yako ni zaidi ya 50%, basi unahaki zaidi ya kuongoza nchi. Hilo ni kosa kubwa.

Demokrasia yahitaji uvumilivu, na ni safari ndefu. Rome haikujengwa kwa siku moja...
 
Hawa jamaa wao mgomvi wao ni Pengo kama mtu na si issues.Nchi kuoza haijasemwa na Pengo pekee hata Sitta anasema ina way kwamba Nchi imeoza ila wao wanakuja mahubiri ya nabii muongo hapa .Chuki zenu bure kabisa
 
Back
Top Bottom