JIBU LANGU: mi naona kuwa unachanganya mambo. Kardinale na maaskofu walibariki waraka wa dini yao na si wa serikali. Naomba hili ulielewe. Waraka ule si wa waislamu wala wapagani. Ni waraka wa wakatoliki, sasa kama wewe si Mkatoliki waraka ule unakuhusuje? Mbona wakatoliki hawaujadili ila watu wasio wakatoliki wanauvalia njuga kama wao?
Na hapo ndio kwenye tatizo. Asasi ama uongozi wa kidini kutoa misimamo, maelekezao ama matamshi yanayohusu SIASA tena uhcaguzi wa viongozi wa kuwawakilisha watanzania wote kwa ujumla wao, wawe waislamu ama wakristo ni kuvunja, kukiuka ama kudharau misingi ya taifa letu na zaidi kuhatarisha mustakabali wa taifa letu haswa katika swala la maelewano, mepenzi na kuaminiana miongoni mwa watanzania....
Ahaaa! UFISADI! Je wewe unapenda Mafisadi? Kama unawapenda basi naona una kila sababu ya kuupinga waraka ule maana umegusa mioyo ya mafisadi zaidi. Kama si fisadi, naomba vilete vipengele vya waraka unavyovipinga ili tuvijadili!
Nakushauri usome hotuba ya Mwalimu Nyerere inayoitwa TUJISAHIHISHE aliyoitoa mwaka 1962 akihutubia bunge la Tanganyika. Hii tabia ya kukimbilia kuwatuhumu watu wanaoipingana ama kutofautiana na mitizamo na hoja zenu kuwa sio wazalendo, wana chuki na dini za wengine ama watu wengine, wajinga, wanafiki, mafisadi ama wanapenda au kutetea ufisadi, ni tabia mufilisi ambayo haisaidi taifa kuondokana na madhila na hatari tunazokumbana nazo. haina tofauti na wale wana CCM wanaofikiri kuwa watu wote wasiokubaliana na utawala wao ni wapinzani, wasio wazalendo, wana choyo, wana uchu wa madaraka, wakorofi n.k
Ni lazima TUJISAHIHISHEili tuweze kuondokana na huo Uozo tunaoushutumu. Ama sivyo tutafanikiwa kuondoa uozo mmoja na kuingiza UVUNDO mwengine.
Ninapinga zaidi mantiki, uhalali na mazingira ya utolewaji wa WARAKA na MUONGOZO zaidi ya yaliyomo ndani yake. Hata kama yaliyomo ndani yake yanaweza kuwa yanahitajika sana lakini kushindwa kuheshimu MISINGI YA UTAIFA WETU na kutambua mazingira ya kisiasa na kijamii tuliyo nayo sasa kunaondoa uhalali wote wa kilichoandikwa ndani ya ILANI cum WARAKA ama MUONGOZO ......
omarilyas