JIBU LANGU: Mi nadhani wewe unamchukia Kardinali Pengo. Nasema hivi kwa sababu waraka huu si wa Pengo bali ni wa wakatoliki! Pengo naye ni mkatoliki, ila kwa bahati mbaya au nzuri ametokea kuwa kardinali!
Sio kila anayepinga Waraka ama Muongozo anamchukia Pengo ama Ponda. Ni wazi ana muono tofauti na wewe unayeona kuwa waraka huo na hao wanao ona Muungozo ni muafaka.
Ilani ya Kanisa la Katoliki ama Waraka kama tulivyozeshwa kuita sio wa wakatoliki kwa mantiki ya kuwa ni wao waliotengeneza kama ilivyo muongozo sio wa Waislamu. Ni watu wachache wenye ama uhalali au wanaolazimisha uhalali wa uongozi wa kujenga maoni (influence process) ambao wanawataka Waislamu na Wakristo kufuata maoni yao wanayoamini ni makini hata kama wapo miongoni mwa waumini ama wafuasi wao wasio afiki kama ilivyo katika mengi yahusianayo na imani zao.
Kardinali Pengo ameubariki na hivyo kama ambavyo RAIS KIKWETE anavyolaumiwa na kushutumiwa kwa mambo yanayotokea ama yasiyotokea ambayo yeye hakuyafanya ama hakupaswa kufanya ila ndiye mwenye dhamana basi tuhuma na shutuma kwa Kardinali Pengo ni halali ingawa zaweza zisiwe za ukweli kama ambavyo ipo kwa RAIS KIKWETE
Sasa kuna shida gani kwa kiongozi wa dini kukemea ufisadi? Yesu aliwaambia wanafunzi wake "nendeni duniani kote mkatangaze habari njema". Ufisadi ni habari njema? Hapana! Tena hata waraka wa waislamu unasema tusichague mafisadi. Sasa mbona Waislamu hujawapinga? Ila wewe mtu unayemchukia ni Pengo tu!
Hakuna anayelalama kukemea ufisadi bali kutoa ILANI zenye kulenga zoezi la kisiasa kama uchaguzi ktika nchi ambayo misingi na vision yake ambayo sio kwa kupenda bali kwa ulazima wa mazingira tunapaswa kuepuka kufanya siasa katika religious or tribal realms.
Labda yeye imani yake inamwambia kuwa Muongozo unaotoka na wale anaoamini kuwa wana mahusiano mahususi na muumba wake hauwezi kuwa na matatizo kama ambavyo inawezekana ndivyo wewe unavyo ona. Lakini tupo wengi tunaopinga vyote vilivyotokea na vingine vinavyoendelea kutokea ambavyo ni kinyume cha misingi na ndoto zetu kama watanzania.
Halafu nadhani kwa wakatoliki, Pengo ni kiongozi wao, so yes kwa madaraka aliyopewa na wakatoliki, ana official say kwao na si kwako kama wewe sio mkatoliki. Amechaguliwa na wakatoliki. Ukatoliki hauna nchi, ila wakatoliki wana uraia wa nchi zao, naomba hilo ulielewe. Naamini vile vile kuwa uislamu hauna nchi ila waumini wa kiislamu wana nchi zao, ndio maana lugha ya kiarabu inakubalika kwenye uislamu na Vatikani inakubalika kwenye masuala ya kikatoliki. Nadhani umenipata vizuri tu!
Kuhus kuchaguliwa na wakatoliki sidhani kama ni sawa na hili ni suala muhimu pia kwa upande wa hao wanaoitwa viongozi wa waislamu. Hivyo kuchaguliwa sio sehemu inayowapa uhalali bali imani ya wafuasi wao ambayo mara nyingi haihusishi nafasi ya LOGIC kufikia maamuzi ya kipi kitokanacho na hao viongozi wao wa kiimani ni cha kufuata na kipi cha kutofuata. Na pia hakuna lugha inayoitwa Vatikan. Labda tuelimishane zaidi
Ili uweze kuuelewa waraka wa wakatoliki, nakushauri ondoa chuki zako dhidi ya Pengo. Usome na uuelewe, ndipo hapo utakapoelewa Pengo anasema nini. Tafadhali jaribu kufanya hivyo. Haina maana kumchafulia jina Kardinali Pengo kwani hajasema kitu chochote kibaya. Nathani hilo unalielewa.
Kama ni waraka suala hapa sio Pengo bali ni Kardinali Pengo aliyehalalisha WARAKA wenye malengo ya kisiasa ambao ni kinyume cha misingi, maadili na vision ya nchi yetu. Kama ambavyo RAIS Kikwete anavyobeba kila lawama ya matatizo, maovu na mapungufu ya nchi yetu ndivyo ambavyo Kardinali Pengo anavyobeba lawama, shutuma na hata kebehi zihusianazo na WARAKA uliobarikiwa na kanisa lake.
Mimi naona, waraka ni mzuri tu ila watu wanajaribu kutumia siasa kuuzika. Na nadhani hawatafanikiwa kwa hilo, kwa sababu sauti ya Mungu hupitia kwa viongozi wa dini. Hata kama mtapinga vipi, kama Mungu ametumia viongozi hawa kurekebisha jamii ya watanzania, hata kama mtatumia mbinu gani kupinga, mtashindwa tu. Hakuna anayeweza kupingana na Mwenyezi Mungu. Kama kamtumia Kardinali Pengo basi sauti yake itasikika tu, kama hakumtumia basi sauti ile haitazaa matunda. Ushauri wangu ni kuwa, tusubiri tuone! Au unasemaje ndugu yangu Mtanzania? Naomba vile vile kuuliza je wewe ni muumini wa dini gani?
Kusubiri is not an option katika kulinda mustakabali wa nchi na haswa maelewano ya kijamii katika nchi yenye mifumo legelege ya kiutawala kama yetu.
Pia ILANI ama Waraka sio matamshi ya kidini bali maagizo yao utekelezaji wa kisiasa yenye vibwagizo vya kidini hivyo watu kuufanyia siasa ni sawa tu.
Na haya ya kumsingizia Mwenyezimungu kuhalalisha maoni na mitizamo yetu ndio yaleyale yaliotuletea huyo mnayemshutumu kupelekea nchi kuoza wakati tunajua kuwa yeye ni mrithi tu wa shamba la babu lilikuwa limejaa magugu na vichaka. Kosa lake ni kuacha kuchoma moto na kuamua kutumia mbinu ya kupalilia ili kuhakikisha kuwa ana acha mboji ya kulinda rutuba (usalama) wa shamba (nchi) letu.
Na pia lazima utambue kama ambavyo Mkristo Mkapa alipotoa majengo ya serikali kuwapa Waislamu wafanye chuo kikuu ama hivi karibuni Mkatoliki Pinda alipotoa msimamo rasmi wa serikali kuhusu waraka kule bungeni hakujatokea upinzania mkali, mantiki hiyo pia inaweza kuwa tofauti pale Mkrsito Pengo anapomkosoa Rais ama Urais/Uongozi wa Muislamu/Mswahili Mrisho Kikwete.
Uongozi bora ni pamoja na kuwa makini (sensitive) na hali na mazingira kama hayo katika kushughulikia matatizo hata yawe ni yale makubwa kama lilivyo suala la UFISADI.
Pia ni lazima tukubali kuwa kitendo cha Kardinali Pengo kumfanyia sala/maombi maalumu Benjamin Mkapa mara baada ya shutuma za UFISADI kuanza kumgubika na baadae "kubariki" Kitabu cha Mke wa LOWASA ambaye ni siku chache amelazimika kujiuzulu kwa shutuma za Ufisadi, kunapunguza ama hata kuondoa uhalali wake katika kukemea UFISADI miongoni mwa wengi, haswa wale wasio wafuasi wake kiimani. Kwa hiyo kama ambavyo Kikwete anavyokosa uhalali wa kuwa na nia ya dhati kupiga vita ufisadi kutokana na kuwa ni RAFIKI zake wakubwa ambao bado yuko/inasemekana yuko nao ndio wanaoshutumiwa kuwa ni wahusika wakuu wa UFISADI mkubwa unaotumika kama mfano wa kuoza kwa nchi yetu, ndivyo ilivyo kwa upande wa Pengo.
omarilyas