Teko Modise
JF-Expert Member
- May 20, 2017
- 1,914
- 6,033
Usiku wa leo ni fainali ya uefa champions league kati ya manchester city dhidi ya inter milan kuanzia milango ya saa 4:00 usiku
Ninapata mashaka pengine leo tunaweza kushuhudia fainali mbovu zaidi katika historia kwasababu mbalimbali.
Mosi, man city wapo katika fomu ya hatari sana anatoa dozi nzito na hana huruma.
Pili, man city ana kikosi imara sana, anayeanza na ayekaa benchi wote sawa. Anaweza akaanza bernardo silva kwenye wing ya kulia huku Mahrez akianzia sub, akiingia lazma akusababishie madhara.
Tatu, ni mbinu za guardiola, amekuwa akibadilika kila uchao na mabadiliko hayo ya mbinu yamekuwa yakimpa matokeo mazuri.
Nne, uzee wa wachezaji wengi wa inter milan wakiingozwa na akina Dzeko, Mkhytarian, Brozovic na wengineo ambao itakuwa ngumu kwao kukimbizana na akina KDB na Gundogan muda wote.
Mwisho wa siku man city anaweza akashinda kuanzia goli 3 na kuendelea na kuondoa ladha ya fainali kama ile fainali mbovu ya spurs na liverpool mwaka 2019.
Ninapata mashaka pengine leo tunaweza kushuhudia fainali mbovu zaidi katika historia kwasababu mbalimbali.
Mosi, man city wapo katika fomu ya hatari sana anatoa dozi nzito na hana huruma.
Pili, man city ana kikosi imara sana, anayeanza na ayekaa benchi wote sawa. Anaweza akaanza bernardo silva kwenye wing ya kulia huku Mahrez akianzia sub, akiingia lazma akusababishie madhara.
Tatu, ni mbinu za guardiola, amekuwa akibadilika kila uchao na mabadiliko hayo ya mbinu yamekuwa yakimpa matokeo mazuri.
Nne, uzee wa wachezaji wengi wa inter milan wakiingozwa na akina Dzeko, Mkhytarian, Brozovic na wengineo ambao itakuwa ngumu kwao kukimbizana na akina KDB na Gundogan muda wote.
Mwisho wa siku man city anaweza akashinda kuanzia goli 3 na kuendelea na kuondoa ladha ya fainali kama ile fainali mbovu ya spurs na liverpool mwaka 2019.