Pendekezo: Prof. Lipumba awe mgombea wa upinzani Igunga

Pendekezo: Prof. Lipumba awe mgombea wa upinzani Igunga

Mimi naongelea facts hizi kwa sababu nimekaa Igunga takribani wiki mbili zilizopita, Nilikuwa pale kwa muda wa wiki tatu. Watu wa Igunga hawaisemi CUF kama mnavyosema hapa, watu wa Igunga wanamuona Leopold Maona kama a very Strong candidate, na kwa bahati nzuri jamaa anajenga hoja vibaya mno na ka vyovyote vile anaweza kuwa chaguo sahihi la wana Igunga kuliko mtu mwingine yeyote.

Hizi story tunazowekeana hapa kua CUF iko serikalini Znz kwa hiyo ni CCM B ni uzushi mtupu kwani serikali ilie iliundwa kwa matakwa ya wazanzibari na hata CHADEMA walienda kushiriki uchaguzi wa ZNZ kwa kutegemea kuwa wangepata 5% na kuingia serikalini.

Kama kuunda serikali na CCM ni dhambi mbona CHADEMA unaowatetea wameolewa na CCM Arusha? Nachoshangaa mie ni hawa CUF kutowaeleza haya wananchi. Kama ni suala la Posho mbona CHADEMA hadi leo wanazipokea? Kama ni ishu ya kuwa karibu na CCM mbona CDM ndio iko karibu na CCM na hadi inafadhiliwa na matajiri wa CCM? Mbona hatujasikia matajiri wa CCM wanaifadhili CUF? Mimi nasema hapa CHADEMA hawana hoja yoyote ya kutisha, CUF wangejipanga na kuueleza umma wa watanzania juu ya uchafu huu mngekuwa mnajificha wapi? Tatizo CUF wanapigwa tu na kukaa kimya na wamemuachia Mtatiro Mzigo wote mtu mmoja.

Kwa mantiki hiyo mimi naona CDM ndio CCM hata kwa staili ya siasa wanazofanya, siasa za kutumia pesa nyingi, kuhonga wapiga kura n.k. Chama kama CUF wana uadilifu mkubwa sana na wana dsiscipline lakini wasipojionesha kuwa wao ni akina nani mtawachafua na kuwaiita kila jina, Bado naamini kuwa CUF wana nafasi nzuri wakimtumia Leopold.
 
Dk moja kwenye siasa yaweza kubadilisha upepo,so usitumia takwimu za uchaguzi uliopita,unaweza ukakuta huyo leopod unayesema ameshakamata kadi ya cdm fasta na kujiandaa kuingia mjengoni kwa tiket ya cdm huwezi jua
 
Hapa mgogoro mwingine cuf vs chadema, ikiwa chadema hawakuona kuwa wanakubalika ni vema kufanya mpango wa kuongea na Leopord ili agombee kwa tiketi ya CDM
 
Mimi namuona LIPUMBA kama presidential material na asilani abadani sishauri aingie kwenye ubunge, he is the best Presidential candidate no matter what.
 
Nimekuwepo Igunga tangu juzi na leo nimeondoka kuendelea na safari yangu ya kuizunguka nchi na dunia, nimejaribu kuangalia uhusiano kati ya Viongozi na wananchi, nimeangalia mbinu na mapungufu yaliyopelekea Ushindi na kushindwa mwaka jana, nimelinganisha na currentsituation, ukweli ni kuwa mtu yeyote akija takwimu za mwaka jana atakuwa amekosea sana, narudia tena atakuwa amekosea sana.

Igunga walikuwa tayari kufanya mabadiliko katika nafasi ya Ubunge mwaka jana, lakini mahusiano mabovu kati ya wagombea wengine na watumishi wa Halmashauri yalipendelea upande mmoja na kuua ule mwingine, wagombea wengine walikuwa ni kama wanasema kuwa tukischukua mtatukoma, ieleweke kuwa Igunga ni moja ya maeneo ambayo watumishi wa halmashauri na waajiriwa serikalini wana ushawishi mkubwa sana kwa wapiga kura wake au wananchi wa pale.

Nimejaribu kuangalia ni chama gani kinaweza kuwa katika wakati mzuri, nimeona kuwa CHADEMA wana hali nzuri ukilinganisha na vyama vingene. CHADEMA wanaweza wakatupa taabu sana CCM, jambo ambalo CCM linaweza likatupa nguvu ni kuwa CCM tayari tuna mtaji, ila kama wote tujuavyo mtaji wa rasilimali watu hauna guarantee, unaweza ukadhani unao kumbe tayari wameshakuacha zamani.

Hivyo tuna kazi kubwa ya kuhakiki kama wale wapiga kura bado tungali nao (Japo utafiti wangu wa juu juu unaonyesha haukunjui na kuzijaza tabasamu sura zetu).

So japo mimi naweza kuwa mpinzani namba moja wa Rostam Azizi (The Gofather) na kundi lake, naomba ni kili kuwa ni mapema mno kwa CCM kumbeza au kushangilia kujiuzuru kwake kwani nguvu na ushawishi wake (Mbinu/fedha/mtandao) vinahitajika ili CCM tuweze kushinda, na hayo yote yaendane na uteuzi wa mgombea anaekubalika.

Japo sitaki tushinde kwa gharama yoyote bali kwa sifa za mgombea mwenye vigezo akikosekana nipo tayari tupoteze na kutoa ushauri kwa upinzani, ikiwa tu watakuwa na mtu mwenye vigezo.

Naionya CCM isiingie katika vita hiyo bila ya Rostam(ana mbinu/mtandao), labda kama tunataka kujipima nguvu zetu na kuona wananchi wameipokeaje hali hiyo

Hivyo upinzani usiende kwenye kinyang'anyiro wakidhani CCM tumebabaika kwa kiasi hicho.

Nikiwaweka kwenye Mizani CUF na CHADEMA, sasa hivi CDM wapo juu zaidi na hii inatokana na kutamkika sana katika vyombo vya habari, kwa mambo yanayoendelea ndani na nje ya bunge, ni lazima tukubaliane kuwa umaarufu wa CDM umeongezeka sana safari hii, wakati umaarufu wa vyama vingine vikizidi kushuka kwa sababu moja au nyingine.

Ukiangalia kwa umakini matendo ya CDM ni kama wanakifanyia Marketing chama chao na wamefanikiwa, anzia kuangalia udhaifu wa speaker, u-kasuku wa wabunge wetu wa CCM na matendo na kauli za hovyo za CDM, tabia za pande zote hizi zimeinufaisha zaidi CDM.

Hebu iangalie hali hii kulega lega kwa serikali, speaker dhaifu, migogoro ya ndani chama nguvu na umoja utatoka wapi hapa, nini kitegemewe kama matokeo?

Angalizo:
Sitalitoa sasa....
 
Wote mnaounga mkono wazo hili ni CCM.

Sihitaji kwenda Chuo kujua uhusiano wa CUF na CCM!!!

Endapo CUF wangekua wapinzani wa CCM wazo lako ni zuri, Ila kwasasa CUF ni wapinzani wa CDM. kwahiyo unalolisema halitawezekana kamwe.

Hata sisi tunaujua uhusiano wa CCM na Chadema, umesahau muafaka wa Arusha?
 
Umesomeka sana mkuu hata mimi nawashangaa wanaotaka muungano wakati huu
nafikiri hata uongozi wa Chadema utapuuza, kumbuka CUF walivyokuwa wanabeza maandamano
bora kujulikana umeshindwa kwa jitihada zako kuliko kushinda kwa muungano wa kinafiki.

Leo asubuhi bungeni Mbowe kasema anazuia maandamano. Jee, na yeye anayabeza?
 
Damu mpya zinahitajika, kwani Igunga hakuna watu wengine??? watu tumechoka kusikia haya majina ya wakongwe
kweli mkuu hata mi nawashangaa hawa wanaopendekeza! Maendeleo na mabadiliko yataletwa na vijana sio hawa wakongwe wanaojiita eti wazoefu kumbe njaa tu. Mfano mzuri ni huyu six, watu walimwamini kumbe hakuna kitu ni unafiki tu
 
Tatizo lawatanzania ni uvyama, tutachagua mtu muadilifu jamani,, CDM, UDP, CCM, NCCR, CUP vyote sawa, we need watu wa adilifu na watiifu kwa watu wao,
Ondoa magamba katika list yako ya vyama maana hamna mwadilifu.
 
chadema kama chama chenye malengo ya kukamata dola hakitakiwi kuogopa ushindani wanapaswa kusimamisha mgombea kwani hiyo ni njia mojawapo ya kukikuza na kukitangaza chama hata kama hakina wafuasi wengi huko.
 
CDM ilimshinikiza DK Slaa kuwa mgombea urais japo mwenyewe alikuwa hataki. Tumeona faida yake kuingiza wabunge wengi upinzani.

Kwa hivyo kwanini tusichukue nafasi ile kumshinikiza Mh Lipumba ili agombee ubunge Jimbo la Igunga:
  • Ni mzaliwa wa Tabora
  • Ni mwenyekiti wa Chama cha CUF ili kuongeza nguvu za upinzani akisaidiana na kina Mbowe, Lissu na wengine
  • Itaijenga Cuf kisiasa na kujenga Upinzani wenye nguvu bungeni
  • CDM haina nguvu sana kulinganisha na CUF kwa kuwa lipumba ndipo anapotoka.

Ukiiweka CUF kushindana na CCM igunga CCM itachukua jimbo...huo ni ukweli labda kama RA ataamua kuisaidia CUF. Igunga itachukuliwa ama na CDM ama CCM itategemea nani atacheza karata vizuri..Hayo ni maoni yangu
 
Wazo ni jema ila sababu ya ukabila haina mashiko halafu TZ ya sasa mtu anaye gombea lazima awe anakubalika na jamii yake hata CDM wakiweka mtu asiye kubalika jimbo hawalipati
 
Nawashauri CDM wamsimamishe Mpendazoe siku nyingi anapenda ubunge
 
Lipumba endapo ataingia bungeni na kuwa mwiba wa serekali basi hata wabunge wake watabadilika
 
tangu mfumo wa vyama vingi uingie nchini mwaka 1995 hajawahi kutaka kugombea Ubunge wa mahali popote kwanini leo aje kugombea Ubunge?
 
tangu mfumo wa vyama vingi uingie nchini mwaka 1995 hajawahi kutaka kugombea Ubunge wa mahali popote kwanini leo aje kugombea Ubunge?

uthabiti wa nia ya lipumba, ikiwa atagombea ubunge igunga, itakuwa ni kugombania ubunge, kimahesabu atania kutawanya kura kwa 3 ili ccm ifaidike na mtawanyiko huo, nayakumbuka maneno yake mwenyewe kuwa yeye ni mlima kilimanjaro na dr. slaa ni kichuguu, kwa mlinganyo wa hulka hiyo ya uprof.

nina wasiwasi anaweza jiita mungu kwa msomi wa darasa la saba hata kama ni mpiga kura mtarajiwa. inawezekana anatumia muda mwingi kushangaa uchumi unavyo poromoka anasahau kuutumia u-prof. wake kujihusisha kuukwamua uchumi wetu nasi kama taifa tukafaidika na utaalamu wake wa uchumi.
 
Back
Top Bottom