Pendekezo: Prof. Abdallah Safari awe Mwenyekiti CHADEMA

bila historia mbele ni kiza- Malcom X stated.

Elewa vizuri my content.
Malcolm X was a alooser on his self.Alikuwa akiongeza kundi la Gangsters na mwishowe alikuwa hana amani wala imani hata na gansters wenzake.
 
CDM ni chama makini na ndio maana magamba wanakigwaya. kiongozi yeyote anawekwa pale na nguvu ya wanachama.wewe unaye wasikiliza magama ukadhani kwenda na wakati ni kumweka mwislamu awe mwenyekiti pole sana. halafu siyo kila professor anakipaji cha kuwa kiongozi.
 
Maoni mazuri lakini yangelenga zaidi kumshauri mwenye chama mzee Mtei kwani ndie mwenye maamuzi ya mwisho.Msije mkamshika pabaya akaanza kuwaita watu majina ya ajabu kama wakuja n.k
wewe bora ungejiita kata stimu maana naona kama una walakini .
 
Mtowa hoja anza kuonesha wewe mfano kama ni muislamu ingia kwenye ukristo na kama wewe ni mkristo silimu ili uwe Muislamu ili uwafurahishe unaowataka.

Rais Jakaya Kikwete ni Muislamu, makamu wake Dr Bilal ni Muislamu, hapa sijaelewa bado what is ur point!! Non sense.
 
alishindwa hata na Lipumba huyo.... Sio kila mtu ana kaliba ya kuwa kiongozi, wengine wabaki kama strategists tu
Mkuu Lipumba ni mwenyekiti na mgombea urais wa kudumu CUF, usitegemee hata mtume akamshinda yule.
 
Prof safari anafaa kuwa mwenyekiti au hata katibu achilia mbali ugombea uraisi kama ataamua hivyo. Tatizo lililopo ni kuzima propaganda kwa kuteua kwa kigezo cha udini badala ya uwezo, hapa ndio tutapalilia propaganda ya udini zaidi na kuwapa credit cc-harm. Kama anagombea agombee kwa kuwa ana uwezo wa kuendelea kukivusha chama kwenye madaraja ya mabadiliko sio kwa kuwa yeye ni muislamu, propaganda hazijibiwi kwa kujitibu kisaikolojia pekee, bali kuonyesha kwa matendo kuwa udini haupo na kama unaongelewa basi unaongelewa kama mtaji wa watu kadhaa kwa malengo maalum.
 
Mkuu, thread umeiweka vizuri kuonyesha uko positive towards CDM, but i doubt it.

Ushauri huo, toa kwa vyama vingine pia, say CUF, au vingine ambavyo huwezi kuchukua fomu kugombea uenyekiti.

Ila nakubaliana nawe, muda ukifika, wenye sifa wajitokeze kugombea nafasi hiyo, si yeye peke yake, ndio demokrasia.
 
Habari wakuu!

Katika tafakuri zangu nimeona ni vyema Prof. Abdallah Safari agombee kiti cha uenyekiti CHADEMA ktk kuelekea 2015, kupitia fursa hii itawezesha chama ku-overcome propaganda chafu za udini ambazo zimekuwa zikienezwa na mpinzani wa CHADEMA (CCM), kwani hoja nyingi za CCM kuhusu udini zimekuwa ziki-base ktk kunyoshea kidole structure ya uongozi wa juu wa chama kwamba upo kiparokia zaidi.

Pia tukubali tukatae ni kwamba CCM bado inanufaika sana na hii cheap propaganda ya udini na kama CHADEMA haitokubali kuneutralize structure ya uongozi CDM basi tujue kuwa out appearance ni 1 ya fact muhimu sana ktk siasa za nchi yetu.

Kwa CHADEMA: Tusibakie tu na utetezi wa kila siku bali tunatakiwa pia tusiwe conservative kama CUF bali tuendane na hali halisi ya siasa za Tz japokuwa somehow itatucost but ni vyema kwa mustakabali wa chama na ukombozi wa taifa letu.

CHADEMA NI CHAMA CHA KITAIFA

Peoples power!

kama yeye hayuko tayari, uaazimishwe? subiri muda ukifika yatajulikna tu
 
wewe mwenyewe umesema ni cheap propaganda sasa iweje mtu asumbuke na kuovercome cheap propaganda na hii ndio sababu pekee unayoiona wewe au unazo zaidi ya hizi
 
Naogopa kusema yaliyo moyoni mwangu lakini maadam mada hii imegusia uongozi wa Chadema basi sina budi kuchangia maana inatuhusu sote. Kwanza kabisa binafsi yangu sio swala la Uongozi wa chama kuwa sababu ya mwelekeo wa chama. Hizi Fikra za kugawana vyeo sawa baina ya Waislaam na Wakristu ndizo zinazotuponza sana nchini na ndizo zinazochochea Udini zaidi.

Kinachotakiwa ni Chadema kama chama kuonyesha wazi sera zake ikiwa ni pamoja na mikakati ya kuondosha UDINI nchini. Na haitajalisha kiongozi ni Mbowe au Professoer Safari au Kamuhanda. Udini sio hesabu ya watu kila upande isipokuwa UDINI ni kitendo cha kuwadhalilisha, kuwagawa na hata kuwanyima haki ya kuabudu, kushiriki waumini wa dini nyingine. Chadema hakuna mtu anayebaguliwa na wala sidhani inatokea CCM au vyama vinginevyo.

Hivyo maadam ndani ya chama watu wenye imani tofauti wanakaribishwa na wanapewa nafasi za kugombea uongozi hakuna sababu wala haja ya kuendeleza hizi habari za uuwiano..Kinachotokea ni kwamba vyama vya siasa vimeshindwa kusimamia haki za waumini wa Kiislaam iwe Chadema au CCM wote wanaogopa kugusa mabo ya kiimani isipokuwa kufuata mfumo uliopo japokuwa wanayaona mapungufu.

Mabaya ya Uuwiano ndiyo yanatukuta ktk Muungano wetu na Zanzibar, hakuna jingine isipokuwa Wazanzibar wanatazama nafasi zao ktk uongozi wa juu nchini badala ya kupima serikali ya Muungano inawafanyia nini Wazinzibar. Kuna sheria na haki zipi ambazo wanazikosa kama Watanzania. Haya ya uuwiano ndiyo yamepeleka Wabunge wa viti maalum bungeni wakati wabunge hawa hawawakilishi maslahi ya wanawake nchini. Ni bora Jumuiya za Wanawake wapewe nafasi ya viti maalum bungeni badala ya jinsia zao kuwa kigezo cha uwakilishi. Bado tutakuwa tumefikia mwisho ule ule wa kuona wanawake wengi bungeni lakini at least hapa watakuwa wawakilisha wa hoja za wanawake nchini.

tatizo liko wapi?...Kuna maswala muhimu sana ambayo waislaam wamekuwa wakiyazungumzia sana, lakini chama na wananchi hasa wanaChadema wamekuwa wapinzani wakubwa ktk maswala hayo. Na kinachowafanya Waislaam kuweka mashaka ktk uongozi wa Chadema ni pale hoja ya Waislaam kwa serikali ya CCM inapojibiwa na watu wa Chadema wakati hawakuulizwa wao. Chadema imekuwa mstari wa mbele kupinga Mahakama ya Kadhi, Kupinga OIC na hata kupinga madai kuhusu NECTA pasipo kufanya uchunguzi wa kina juu ya tuhuma hizi. sasa ikiwa hoja sio yao kwa nini wanaibebea mbeleko?.. hapa ndipo utata na hutuma zinapoanzia.

Binafsi yangu nilitegemea sana kabla ya Chadema ama wanachama wake kujibu lolote wangeliacha swala hili liwe la CCM ama wafanye uchunguzi kujua kwa uhakika faida na athari za hoja hizi badala ya kutoa majibu ya dharau na kejeri yanayoichimba dini. Kwa kila hoja inayotolewa na kingozi yeyote wa dini imekuwa matusi kwa imani nzima ya kiislaam kutokana tu na propaganda za chuki dhidi ya Uislaam. Na kikubwa zaidi chuki hizi zimepandikizwa na nchi za Magharibi ambao malengo yao ni kuzitawala nchi za Kiarabu kiuchumi hivyo Uislaam umekuwa mwiba kwao na hivyo unapigwa vita imefkia kwamba leo hii wana Mapinduzi huitwa Magaidi..

Kuna ukweli mkubwa sana ktk historia ya Uislaam kupingana na watu Kutawaliwa Kiuchumi. Na zipo hadithi nyingi zinazohalalisha vita kupigania haki yako hasa pale inapopokonywa na mgeni na kutokana na nadharia hiyo kulitokea hii kitu Revolution - Mapinduzi ambayo kwao wakoloni hawakutegemea kuwa Uzalendo na sifa ya Uraia isipokuwa huu ni Uislaam. Mahatma Gandhi aliusifia Uislaam na pengine hata kurudi India kupigania Uhuru wake ilitokana na imani hii ya kutotawaliwa..

mkuu mkandara umetoa ufafanuzi mzuri sana.
Ubarikiwe.
 
Habari wakuu!

Katika tafakuri zangu nimeona ni vyema Prof. Abdallah Safari agombee kiti cha uenyekiti CHADEMA ktk kuelekea 2015, kupitia fursa hii itawezesha chama ku-overcome propaganda chafu za udini ambazo zimekuwa zikienezwa na mpinzani wa CHADEMA (CCM), kwani hoja nyingi za CCM kuhusu udini zimekuwa ziki-base ktk kunyoshea kidole structure ya uongozi wa juu wa chama kwamba upo kiparokia zaidi.

Pia tukubali tukatae ni kwamba CCM bado inanufaika sana na hii cheap propaganda ya udini na kama CHADEMA haitokubali kuneutralize structure ya uongozi CDM basi tujue kuwa out appearance ni 1 ya fact muhimu sana ktk siasa za nchi yetu.

Kwa CHADEMA: Tusibakie tu na utetezi wa kila siku bali tunatakiwa pia tusiwe conservative kama CUF bali tuendane na hali halisi ya siasa za Tz japokuwa somehow itatucost but ni vyema kwa mustakabali wa chama na ukombozi wa taifa letu.

CHADEMA NI CHAMA CHA KITAIFA

Peoples power!

Kaka, hatuchagui mtu ili ku-overcome propaganda, nadhani unaelewa historia ya wenyeviti wa cdm. CDM imebadili wenyeviti kwa vipindi vyote bila kujali dini ya mtu. Ni kosa kubwa sana tukianza kuchagua viongozi kwa misingi ya dini.
 
Habari wakuu!

Katika tafakuri zangu nimeona ni vyema Prof. Abdallah Safari agombee kiti cha uenyekiti CHADEMA ktk kuelekea 2015, kupitia fursa hii itawezesha chama ku-overcome propaganda chafu za udini ambazo zimekuwa zikienezwa na mpinzani wa CHADEMA (CCM), kwani hoja nyingi za CCM kuhusu udini zimekuwa ziki-base ktk kunyoshea kidole structure ya uongozi wa juu wa chama kwamba upo kiparokia zaidi.

Pia tukubali tukatae ni kwamba CCM bado inanufaika sana na hii cheap propaganda ya udini na kama CHADEMA haitokubali kuneutralize structure ya uongozi CDM basi tujue kuwa out appearance ni 1 ya fact muhimu sana ktk siasa za nchi yetu.

Kwa CHADEMA: Tusibakie tu na utetezi wa kila siku bali tunatakiwa pia tusiwe conservative kama CUF bali tuendane na hali halisi ya siasa za Tz japokuwa somehow itatucost but ni vyema kwa mustakabali wa chama na ukombozi wa taifa letu.

CHADEMA NI CHAMA CHA KITAIFA

Peoples power!

Labda Mtei akifa.
 
Na Mtatiro agombee kupitia CUF kuondoa dhana ya chama cha kiislam.
 
Makamu mwenyekiti (Bara)- Said Arfi, Makamu (Zanzibar), Naibu katibu Bara (ZZK) na Naibu Katibu (Zanzibar) wote waislamu na bado mnasema ni uongozi wa Parokia? Siwezi kuelewa na Watanzania hawawezi kuwaelewa
 
Jamani labda niwakumbushe tu kuwa mtu mnayemuongelea ni Profesa katika maana zote za neno Profesa so anajua what, why ,where and when to do it. Na viongozi na wanachama wa CHADEMA tunatambua hilo. Sio mtu mrahisi wa kumpandikizia hisia. Makama mwenyeketi, makamu katibu mkuu ni waislam lakini dini haikuwa kigezo cha kuwapa nafasi hizo.
 
Prof safari anafaa kuwa mwenyekiti au hata katibu achilia mbali ugombea uraisi kama ataamua hivyo. Tatizo lililopo ni kuzima propaganda kwa kuteua kwa kigezo cha udini badala ya uwezo, hapa ndio tutapalilia propaganda ya udini zaidi na kuwapa credit cc-harm. Kama anagombea agombee kwa kuwa ana uwezo wa kuendelea kukivusha chama kwenye madaraja ya mabadiliko sio kwa kuwa yeye ni muislamu, propaganda hazijibiwi kwa kujitibu kisaikolojia pekee, bali kuonyesha kwa matendo kuwa udini haupo na kama unaongelewa basi unaongelewa kama mtaji wa watu kadhaa kwa malengo maalum.

Huyu jamaa prof .namheshimu sana si mtu wa papara kama watu wengine wanavyoweza mfanya awe.Ni simple sana na ukimsikia ktk vipindi vya Kiswahili huwezi amini kuwa yupo kwenye fani nyingi sana.

Kwa ujumla huyu prof anajua kabisa kuwa Kwa muda aliokuwa CDM kanuni za CDM haziwezi mruhusu gombea ngazi ya kitaifa.Na yeye si mtu wa kubaka sheria.Aliweza kukbaliana na CDM kwa vile lengo lake si madaraka sana zaidi ya kuwa senior.Huyu ni Mzee wa Nyumba za Serikali tuu(magufuli ajiandae kwa kushukiwa naye) na kitu anachoamini kuwa ni Haki.HIvyo tuu ndivyo vinavyomshawishi.Ndio maana alipokwenda igunga nilijua anakwenda with passion,tena magufuli aliyeuza nyumba za serikali ndie aliyechafua hali ya hewa.

Mtoa mada nataka mlazimisha kupewa madaraka ila cha ajabu anaweza hata sichukue form.Kwani kwa wanachama waliokomaa huwa wanafanya majadaliano ya ndani ili kupata view za ndani na strategic decisions wanazoweza fanya tegemeana na wagombea wa upinzani au hata mgawanyo wa majukumu.Ndio maana utasikia mtu anasema fulani akigombea mimi sigombei.Hii ni kuonyesha kuwa huyo fulani akigombea jahazi la chama litasalimika.Prof ni mmojawapo wa wanajopo imara "back grounders" amabo wanashauri amambo mengi sana hata yanayohusu nafsi ya imani za dini katk siasa na yeye akiwa kama muislam.Nadhani hapo alipo anaplay role kubwa sana kuliko uwa busy majukwaani.Nani asiyejua mchango wa CDM katik serikali inagwa hawapo madarakani?
 
Back
Top Bottom