Salaam, Shalom!!
Niliwahi kuandika thread isemayo, Wabunge wafanyabiashara matajiri wanasimamia Maslahi ya nani bungeni?
Haijaisha miezi SITA tangu kuandikwa thread hiyo, tayari Kuna tetesi kuwa Wabunge wamejiongezea posho na marupurupu Yao Kutoka ml 13 Hadi ml 15 Kwa mwezi.
Mbunge anayeona posho na marupurupu ya ml 13 kuwa haitoshi, huyo hawezi kamwe kutosheka. Na watu Hawa, lazima ni matajiri wakubwa walioacha biashara zao na kwenda bungeni wakidhani bungeni Pana maslah binafsi ya kiuchumi.
KAZI ya ubunge ni KAZI ya season, Si ajira ya kudumu, lazima uwe na KAZI Yako ,bungeni unaenda kutetea Maslahi ya wananchi, wabunge wanaodhani kuwa ubunge ni ajira ndio wanatuletea shida.
Pale Uingereza, mbunge anapanda treni ya umma kwenda bungeni, gari yake binafsi anatumia akiwa jimboni kwake na umma hawajibiki kumlipia mambo lukuki kama huku.
Mshahara na marupurupu usizidi ml 5 Kwa mwezi, na mbunge lazima awe na KAZI yake, bungeni pasifanywe ajira.
Wabunge wapande mabasi kama raia wengine waendapo Dodoma, Kodi zetu zisitumike kulipa mshahara wa dereva, mbunge akitaka gari, akopeshwe na alipe Yeye mwenyewe na ajigharamie gharama za mafuta.
Tunachagua wabunge Ili wasaidie wananchi tupate bima walau za watoto chini ya miaka mitano iliyofutwa Ili kujazia pesa za kulipa wabunge ml 18 Kwa mwezi na kulipa wake wa wastaafu.
Wabunge oneni Aibu na muwe na huruma Kwa wananchi.
FAIDA ZA KULIPA MISHAHARA YA WABUNGE CHINI YA ML 5 KWA MWEZI.
1. Itasaidia wabunge wazalendo kuingia bungeni.
2. Itapunguza wizi wa kura.
3. Itasaidia kujipunguzia Serikali Mzigo kuhudumia wabunge, Badala yake, pesa hizo zitasaidia kulipa posho walimu mashuleni Ili wafundishe Kwa Ari na morali zaidi.
Hivi wabunge jiulizeni, bodaboda, matching guys ,wakulima, wavuvi ambao Kwa mwezi hawapati hata laki 5 Kwa mwezi, wamepata wapi uwezo kuwalipeni wabunge 399 , milioni 18 Kwa mwezi=7 bilion?
Mkiendelea na uroho huo, tutasusia mikutano yenu na hatutowapigia kura!!
KATIBA mpya na Tume huru ya Uchaguzi kabla ya Uchaguzi wowote ni sasa, wabunge wamedhihirisha wazi kuwa hawaangalii maslah ya Wananchi maskini, wanajiangalia wao na familia zao.
Pia wabunge wazuiwe kujiongezea mshahara bila kupata ridhaa ya walipakodi.
Karibuni 🙏
Niliwahi kuandika thread isemayo, Wabunge wafanyabiashara matajiri wanasimamia Maslahi ya nani bungeni?
Haijaisha miezi SITA tangu kuandikwa thread hiyo, tayari Kuna tetesi kuwa Wabunge wamejiongezea posho na marupurupu Yao Kutoka ml 13 Hadi ml 15 Kwa mwezi.
Mbunge anayeona posho na marupurupu ya ml 13 kuwa haitoshi, huyo hawezi kamwe kutosheka. Na watu Hawa, lazima ni matajiri wakubwa walioacha biashara zao na kwenda bungeni wakidhani bungeni Pana maslah binafsi ya kiuchumi.
KAZI ya ubunge ni KAZI ya season, Si ajira ya kudumu, lazima uwe na KAZI Yako ,bungeni unaenda kutetea Maslahi ya wananchi, wabunge wanaodhani kuwa ubunge ni ajira ndio wanatuletea shida.
Pale Uingereza, mbunge anapanda treni ya umma kwenda bungeni, gari yake binafsi anatumia akiwa jimboni kwake na umma hawajibiki kumlipia mambo lukuki kama huku.
Mshahara na marupurupu usizidi ml 5 Kwa mwezi, na mbunge lazima awe na KAZI yake, bungeni pasifanywe ajira.
Wabunge wapande mabasi kama raia wengine waendapo Dodoma, Kodi zetu zisitumike kulipa mshahara wa dereva, mbunge akitaka gari, akopeshwe na alipe Yeye mwenyewe na ajigharamie gharama za mafuta.
Tunachagua wabunge Ili wasaidie wananchi tupate bima walau za watoto chini ya miaka mitano iliyofutwa Ili kujazia pesa za kulipa wabunge ml 18 Kwa mwezi na kulipa wake wa wastaafu.
Wabunge oneni Aibu na muwe na huruma Kwa wananchi.
FAIDA ZA KULIPA MISHAHARA YA WABUNGE CHINI YA ML 5 KWA MWEZI.
1. Itasaidia wabunge wazalendo kuingia bungeni.
2. Itapunguza wizi wa kura.
3. Itasaidia kujipunguzia Serikali Mzigo kuhudumia wabunge, Badala yake, pesa hizo zitasaidia kulipa posho walimu mashuleni Ili wafundishe Kwa Ari na morali zaidi.
Hivi wabunge jiulizeni, bodaboda, matching guys ,wakulima, wavuvi ambao Kwa mwezi hawapati hata laki 5 Kwa mwezi, wamepata wapi uwezo kuwalipeni wabunge 399 , milioni 18 Kwa mwezi=7 bilion?
Mkiendelea na uroho huo, tutasusia mikutano yenu na hatutowapigia kura!!
KATIBA mpya na Tume huru ya Uchaguzi kabla ya Uchaguzi wowote ni sasa, wabunge wamedhihirisha wazi kuwa hawaangalii maslah ya Wananchi maskini, wanajiangalia wao na familia zao.
Pia wabunge wazuiwe kujiongezea mshahara bila kupata ridhaa ya walipakodi.
Karibuni 🙏