Naamini kabisa kuna watu wanatumiwa humu ndani kwa makusudi mazima ya kuhakikisha Zitto Kabwe anakuwa mchafu daima ndani ya CDM, na haiishii hapa tu hata baadhi ya magazeti yanafanya juhudi hizo pia
Na Zitto hachafuliwa kwa bahati mbaya, HAPANA..... huu ni mpango mkakati baada ya kuonekana Zitto amekuwa tishio kwa ''wenye'' CDM yao.Maana kwa kadiri mambo yanvyozidi kwenda ndivyo ninavyo shindwa kutofautisha sakata la marehemu Wangwe na CDM kwa ujumla na hili analoandamwa nalo Zitto Kabwe
Toka Zitto amechukua na kugombea uenyekiti wa CDM na sakata zima hadi kuja kuzimwa basi amejitengenezea maadui wakubwa ndani ya CDM, na kama una akili timamu basi pasi na shaka utaelewa ni kundi la uongozi wa juu ndilo hasa lenye uhasama na zitto kabwe
Hivi sasa Zitto anatengenezewa picha ya msaliti, mroho wa madaraka nk nk kwasababu tu naamini ndani ya CDM ni wachache sana wanaoweza kusimama na kusimamia hoja zao ndani ya chama na si matakwa ya "wenye chama" wanavyotaka
Na hii ndio kila chaguzi ndani ya chama wele wenye kufuata matakwa ya wenye chama huwa tofauti na wenye fikra huru za kidemorasia ndani ya chama(akina zitto) na kufanya makundi ya Mbowe(wenye chama) na Zitto(fikra huru)
Tuhuma zote anazotuhumiwa Zitto humu kama kula bata na mukulu na kutooneka kwenye M4C nk hazina ukweli wowote, kwa kadri nijuavyo chama kinapanga kila kitu na si watu wanajipeleka kama unakwenda sokoni, safari zote za Zitto zinajulikana CDM na zinakwenda kwa mujibu wa nafasi zake.
Kama madai hayo yanaukweli mbona makao makuu au viongozi hawasemi chochote juu ya hilo
Wale wote mnaotumiwa katika hili mnatakiwa kufahamu kitu kimoja muhimu sana, mnajenga na kuyapa uhai na nguvu madai ya wapinzani wa CDM kuwa wadini na wakanda
Kwamba wale wote wanaoonekana wanakuwa tishio dhidi ya wa watu wa ukanda fulani basi wanapikiwa zengwe kama inavyotoke kwa mh Zitto Zuberi Kabwe
Just my opinion