Pemba: Migomo Imeanza Kushamiri CUF dhidi ya CCM

Pemba: Migomo Imeanza Kushamiri CUF dhidi ya CCM

Mkuu huko Zanzibar tangu na tangu hawategemei bidhaa za bara, mchele, ndizi, cement, sukari, labda nyanya na nyama basi.
 
Mi nadhani hizo hasira zao wangalielekeza zaidi kwa serikali hio haramu na sio wananchi. Waweke migomo kama kutokwenda makazini au kutokututii serikali haramu.

Sent from my SM-G920W8 using JamiiForums mobile app
 
Nadhani Sasa mmeamini watu wakisema hao jamaa wana akili finyu sana!!!
Kweli umsuse ndugu yako wa damu kwasababu ya CUF Na CCM???
Hiyo ni akili au matope??
 
Poleni sana kama siasa ndio inakufanya mtu muhasimiane na familia yako. Kitu kinacho nishangaza mnajiita waislam sasa hiyo dini yenu inasemaje kuhusu ndugu, jirani na hivyo mnavyotaka kuishi. Sasa huyo mzazi au kaka,au,mjomba wako akiwa ccm na Yuko Huko pemba je Ulimuangalia ukaona maisha yake bora kukushinda wewe au nyote mko sawa? Msifate mkumbo hao mnaowafata maisha yao manono. Walipo sema wazee damu nzito kuliko maji inamaana yake.

Unasahau ccm waliposema machotara hawatakiwi znz. Dhambi ya ubaguzi inawatafuna.
 
Huko Mungu yuko chini siasa iko juu, eti nimtelekeze mzazi wangu mtoto wangu ama Dada yangu kisa siasa, hiyo siasa nilizaliwa nayo ama nimeikuta tu. Kilichofanywa na CCM huko Zanzibar ikishurikiana na tume ya uchaguzi si cha kuungwa mkono, ila hunigombanishi na ndugu zangu sababu tu mapenzi yao kisiasa ni tofauti na mimi. Alafu pembeni nadai haki nada Demokrasia nini sasa maana ya haki nini maana Demokrasia, eti alafu uneanda msikitini mara tano, huku kifua kimejaa chuki, wanaojifanya wanaijua dini ndiyo watenda dhambi wakubwa.

Siasa ni kila kitu kama ulikuwa ujui. Bila Siasa hakuna nchi
 
Nimewahi kuishi Zanzibar kwa kipindi kifupi, Zanzibar dini, kujitanda ushungi ni utamaduni wala si ucha Mungu, ingawa wao hujiona wacha Mungu zaidi kuliko mtu yeyoto anaetokea bara. Zanzibar mtu aweza ingia msikitini mara tano kwa siku, akitoka hatua tano matusi yako palepale, wanaojaza kumbi za starehe ni wale wale wenye ushungi na waswali swala tano. Huwezi toka bara hata uijue vipi dini eti ukaswalishe Zanzibar no haiwezekani, ila yote kwa yote haya ndiyo matunda yake maana katika hili hakushirikishwa Mungu, wengemshirikisha wangetafuta namna nyingine ya kufikisha ujumbe. Je huko hakuna watu wasiokua na chama.
 
Kwa mujibu wa uislam ikiwa wote ndugu tena katika dini hamsemezani mkifa wote motoni, sasa hao cuf kwa kuwa wao ndio wanaoanzisha chuki hizo na kusababisha waislam kutosemezana na kusaidia wajiandae kwenye motoni, wanatoka katika uislam, katika hiloi sharifu hamadi moto wa jehanam unamsubiri kwa uroho wake unawasababishia waislam wachukiane na anabariki hizo chuki hana tofauti na kafiri,
 
Sijasikia mukiuliza kama shein na ma ccm wengine wana dini hadi wawe radhi watu hata laki wafe ila wao waendelee kunyonya,hii nchi ya kinafiki sana,wakati ma ccm wakipora hamuwaambii waogope Mungu,ila inapofika walioporwa wanadai Chao ndiyo utaona unafiki wenu
Poleni sana kama siasa ndio inakufanya mtu muhasimiane na familia yako. Kitu kinacho nishangaza mnajiita waislam sasa hiyo dini yenu inasemaje kuhusu ndugu, jirani na hivyo mnavyotaka kuishi. Sasa huyo mzazi au kaka,au,mjomba wako akiwa ccm na Yuko Huko pemba je Ulimuangalia ukaona maisha yake bora kukushinda wewe au nyote mko sawa? Msifate mkumbo hao mnaowafata maisha yao manono. Walipo sema wazee damu nzito kuliko maji inamaana yake.
 
Siasa ni kila kitu kama ulikuwa ujui. Bila Siasa hakuna nchi
Najua ila yote kwa yote nipo tayari hata kutoa uhai wangu kwa ajili ya watu wangu wa karibu, na sio nipotayari kuwapoteza kwa sababu ya siasa. Ni kweli maneno ya siasa ni kila kitu, ila usisahau maneno ya haya pia ni kisiasa. Ni nani alalae kula kwa raha pale anapopata habari, mwanae/ mzazi wake anaumwa.
 
View attachment 334432

#‎Pemba‬.
Wanachama wa CUF Wilaya ya, Majimbo yote matano (Wete, Kojani, Mgogoni, Mtambwe na Gando) leo wameafikiana ktk kikao chao kuendelea na mgomo rasmi juu ya CCM kwa mambo yote ya kijamii ikiwemo Arusi,Misiba,Biashara, Ugonjwa na hata magari na meli na kuazimana vitu/vfaa vya majumbani nk. (CUF kwa CUF na CCM kwa CCM tu mpaka kieleweke)
"Mikutano ya Matawi kwa sheiha zote za Wilaya ya Wete itafanyika kwa uhamasishaji zaidi, katika hatua hio bila kujali uzawa/udugu, din...i, kabila au tunapo toka.

Tumekubaliana kama aliefiliwa ni CUF mmoja au wawili au idadi yeyote basi kuungana nae ni kutokwenda kwenye msiba huo uliowakuta wana CCM waliomo ndani ya familia yake.
HAYO TUME KUBALIANA"
Alisema mmoja wa wafuasi hao wa CUF.

Waanze kurudisha bill ya matibabu ya Maalim Seif na gharama za Hotel alizokaa DSM, sio wanaumizana wenyewe wa chini juu wanajuliana hali na kuhurumiana.
 
aya maamzi wanayochukua wanamuuliza seif kwanz make km yuko kinyume nao kabisa
 
Je sheikh kitabu kinasemaje kuhusu ukandamizaji!wizi wa kura!kunyanganya ushindi halali?? Wanaofanya matendo hayo wanakwenda mbinguni moja kwa moja sio?
Kwa mujibu wa uislam ikiwa wote ndugu tena katika dini hamsemezani mkifa wote motoni, sasa hao cuf kwa kuwa wao ndio wanaoanzisha chuki hizo na kusababisha waislam kutosemezana na kusaidia wajiandae kwenye motoni, wanatoka katika uislam, katika hiloi sharifu hamadi moto wa jehanam unamsubiri kwa uroho wake unawasababishia waislam wachukiane na anabariki hizo chuki hana tofauti na kafiri,
 
Umesema kweli kabisa: Ila tunaomba fatwa ya watu walioandaliwa na ccm wanaovaa masoksi usoni kushambulia watu kwa silaha za moto, mapanga na visu kuwahujumu watu kisa tu ni wanacuf, lakini pia watu kubambikiziwa kesi na kulazwa ndani siku kadhaa na mateso mbali mbali, waislamu wanaofanywa matendo haya wanatakiwa kufanya nini?
Solution
Ndugu yangu fahamu ya kuwa kupigwa , kudhulumiwa, kunyanyaswa, kuteswa ,Kuibiwa Mali haya yote yanatokana na.madhila yote yanatokana madhambi ya waislam wenyewe

Allah subhanaw wataala anasema
" Na hayawapati misiba ( majanga matatizo mbalimbali) isipokuwa kwa kile ambacho mikono yenu imekichuma ( madhambi) na Allah anasamehe mengi "

Na Mtume swallallahu alayh wassallam anasema " Pindi mtakapo fanya biashara za Riba na mkashika mikia ya ng'ombe Wenu ( yaan mkaendekeza sana kilimo ) kisha mkaacha Jihad basi Allah atakusalitishieni udhalili hatoutoa udhalili huo mpaka mrejee katika dini yenu "
[Sunan Abee Dawhood ]

Kwaiyo kama mafundisho ambavyo yanajieleza inatakiwa watu wa Zanzibar warudi ktk mafundisho sahihi ya dini yao Hakuna kamwe mwanasiasa atakayetatua matatizo yao Bali Mola wao lau wakirejea kwake basi mabadiliko ni kitu chepesi mno

Allah Subhannaw wataala anasema.
" Hakika ya Allah abadilishi Yale yalikuwa kwa watu mpaka hao watu wabadilishe yaliyokuwa katika nafsi zao "


Kwaiyo Ndugu nadhani utakuwa umenielewa watu yatakikana waache Shirk, Bidaa,Maa'sia na uchafu uchafu wote ktk dini ili dini ibaki safi
 
Kwani CCM walitarajia nini? Haya mambo yalikuwepo na ndio yalipelekea kuunda Serikali ya Umoja wa Kitaifa. Kwa hiyo wasishangae yanapotokea haya kwa sababu wao (CCM) ndio wameikataa SUK kwa kusigina demokrasia huko visiwani.
Watu walitumia muda mwingi baada ya maumivu makali kufuta na kusahau yaliyopita halafu watu wachache kwa ulafi wa madaraka wanaturudisha tulipotoka!na walaaniwe!
 
kama watu wa Cuf wamekubaliana hayo basi hawajui hata madhumuni ya kuwa na hicho chama ... je askali wanaowalinda ako Cuf au wao watashughulika na yeyote... je hakuna familia ambayo imeoa kutoka kwenye familia za Cuf.... kama wanaendekeza upuuzi huo wa kuwabagua wenzao basi ni halali vyama vifutwe tubaki na tanzania isiyo na siasa wala vyama vya siasa ...
 
Hata Nabii Mussa baba yake alikuwa Firauni! Na yeye ndiye aliyesababisha kifo chake. Dhulma ipiganiwe kwa nguvu zote, hata kama atakuwa ni mzazi wako there is no exception to the rule! CCM Zanzibar sio chama cha siasa, ni mkoloni mweusi, much worse than the apartheid regime was in SA!
 
Back
Top Bottom