Indian
JF-Expert Member
- Oct 27, 2012
- 821
- 710
View attachment 334432
#Pemba.
Wanachama wa CUF Wilaya ya, Majimbo yote matano (Wete, Kojani, Mgogoni, Mtambwe na Gando) leo wameafikiana ktk kikao chao kuendelea na mgomo rasmi juu ya CCM kwa mambo yote ya kijamii ikiwemo Arusi,Misiba,Biashara, Ugonjwa na hata magari na meli na kuazimana vitu/vfaa vya majumbani nk. (CUF kwa CUF na CCM kwa CCM tu mpaka kieleweke)
"Mikutano ya Matawi kwa sheiha zote za Wilaya ya Wete itafanyika kwa uhamasishaji zaidi, katika hatua hio bila kujali uzawa/udugu, din...i, kabila au tunapo toka.
Tumekubaliana kama aliefiliwa ni CUF mmoja au wawili au idadi yeyote basi kuungana nae ni kutokwenda kwenye msiba huo uliowakuta wana CCM waliomo ndani ya familia yake.
HAYO TUME KUBALIANA"
Alisema mmoja wa wafuasi hao wa CUF.
Nadhani nitakaposema kuwa hii hoja sio kweli mtanikubali, hili jengo lipo Wete Pemba, kwenye hayo maduka moja wapo Ni duka la rafiki yangu jina lake la Utani Anaitwa key, upande wa Pili kuna Makao makuu ya Cuf kwa Pemba Ndio kubwa.
Pemba Na Wapemba wameshajifunza siasa Na sasa wanaielewa sio tena wale wa miaka ya 90, tusitegemee kusikia tukio lolote tena kutoka Pemba litalofanywa na wananchi.
Kama una Swali lolote niulize kuhusu Pemba yote nitakuambia.