BAK
JF-Expert Member
- Feb 11, 2007
- 124,769
- 288,283
- Thread starter
- #261
Miye nimepoteza imani na TAKUKURU miaka mingi tu iliyopita baada ya ile kauli kwamba, "Mafisadi ni matajiri wakubwa nchi kwetu kama wakikamatwa nchi itawaka moto." Kauli hii ilitolewa na Pinda akiwa pamoja na Mkuu wa Polisi nchini na Mwanasheria Mkuu kabla ya huyu mpya na TAKUKURU hawakutia neno kupinga kauli ile na hadi sasa hivi utendaji wao unaonyesha kwamba hawana nia yoyote ya kupambana na rushwa nchini.