kinepi_nepi
JF-Expert Member
- Aug 16, 2007
- 869
- 239
Ni kweli TAKUKURU ni kimbilio la mafisadi kwani ndio wanaoficha siri za mafisadi na kuuwa upelelezi pale fisadi anapotakiwa kupelekwa mahakamani.Mkuu,
Sasa umeanza kuiita TAKUKURU kimbilio la mafisadi kwa facts zipi?
badala ya kuwashauri watanzania wenye ushahidi kuwasiliana na polisi au TAKUKURU wewe unaanza kutumia jambo la RA kwenda TAKUKURU kuifanya taasisi yote ionekane ya kifisadi?
Inaelekea hapa JF tumechanganyikiwa hata hatujui nini tunataka, hatuna msimamo mmoja unaoeleweka, tunayumba, tunatapatapa kwa kuangalia mhusika ni nani.
RA katumia haki yake kama Mtanzania mwingine, muhimu ni kuwashauri wengine wenye habari kuhusu uhalifu kuweza kuzifikisha kwenye vyombo vyetu vya usalama.
Huwezi kumlazimisha mtu aende sehemu unayotaka wewe, mtu anaweza kwenda polisi, anaweza kwenda vyombo vya habari ili viandike, anaweza kwenda mahakamani, anaweza kwenda TAKUKURU.
Kitu ambacho hutakiwi kufanya ni kuilamu taasisi yote kama TAKUKURU kwamba ni kimbilio la mafisadi. Je wale walioko mahakani baada ya kupelekwa na TAKUKURU sio mafisadi?
Ndio TAKUKURU wana matatizo na wanatakiwa kuongeza ufanisi na kupunguza kuwa tegemezi sana kwa serikali, lakini hiyo sio sababu ya kuwaita TAKUKURU kimbilio la mafisadi.
Sio kila case unaweza kupeleka mahakamani. RA anaweza kwenda mahakamani kumshitaki Mengi kwa kumkashifu lakini hawezi kwenda mahakani kumshitaki Mengi kwa kuiibia NICO au mabank. Hiyo ni kazi ya serikali kama sikosei.
Hawa jamaa watoe ushahidi walio nao ili tuwajue vizuri hawa papa na Nyangumi bila kujali ni Mengi au RA.
Tatizo la watu wengi hapa ni double standards, kama Mengi amekosea sio fisadi, kama RA ni fisadi. Hawa wote mapapa na Nyangumi ni mzigo kwa Tanzania. List haiishii hapo, wako wengi mno. Wakiumbuana ndio faida kwa sisi wananchi.
Niambie ni lini walimhoji Rostam kuhusiana na kagoda na waligundua nini??
Niambie si hao waliomsafisha mwizi Richmond kwa kumwita ni safi na mwakyembe akasema sio.
Niambie ni nani takukuru imesha toa ushahahidi dhidi yake.
je ni kweli TAKUKURU hawajui kwamba chenge alituibia baada ya SFO KUHAKIKI.
Au hawajui kwamba Chenge alikuwa na marehemu kabla hajawauwa. come on now.
takukuru ina nia ya kumsafisha RA na hii ni plan move.