Paul Makonda: Hivi hili Taifa tutaacha lini kupenda Umbea, Majungu na Uongo?

Anaandika Paul Makonda katika mitandao ya kijamii

Hivi hili Taifa tutaacha lini kupenda Umbeya, Majungu na Uongo. Na hata kama hakuna habari mbaya bado tunalazimisha tu ziwepo. Unaambiwa kabisa siyo kweli we bado unabisha tu ulazimishe ni kweli. Ona sasa ukitumia akili kidogo tu utagundua hata safari zinazosemwa ni za Utalii na wala siyo Matibabu. Ndani ya siku mbili ameingia Kenya Nairobi hospital ndani ya siku mbili hizo hizo kafikishwa South Africa ndani ya hizo siku yuko India na sasa Germany . Haya ni matibabu au Utalii. Ebu tuombeane Mema, ebu Tamani jambo jema kwa Mwenzako, huu ni wakati wa ku share habari njema na wala siyo kuongeza hofu na taaruki. Ebu tuombee familia zetu, ebu kila Mtu atafakari mahusiano yake binafi na Mungu, ebu wajulie hali ndg zako walioko vijijini na kama unanjia ya kuwasaidia ebu fanya jambo la kuwapa faraja ikiwezekana tafuta hata watu uliosoma nao wajulie hali Badala ya kupoteza bando lako kusambaza na kuulizia uzushi.Biblia inasema Shetani ni baba wa uongo, nina wasiwasi atakuwa na Watoto TANZANIA

My Take
Nami naungana na Paul Makonda kukemea chuki na uongo. Ila kabla sijakemea nina mambo ya kuhoji.

1. Mbona mwahubiri upendo kwa baadhi ya watu tu? Humuoni kama mnaushangaza huo upendo na ndio maana umetoweka? Ulikuwa wapi upendo dhidi ya Ruge Mutahaba na Clouds Media ulioivamia na silaha za moto? Wewe Makonda umetajwa kwenye matukio mengi maovu ambapo baada ya kuondoshwa yalipungua. Ushahidi ni wewe kupigwa marufuku kuingia Marekani kwa kilichotajwa kukiuka haki za binadamu.

Upendo huo umekujia lini?
Unakumbuka kipindi cha vyeti feki, wakatumbuliwa wengi wewe ukaachwa. Upendo ikawa kwako tu. Hapo mlipanda chuki kiasi gani?

2. Mbona mwakataza uzushi kwa baadhi ya watu fulani tu. Pale anapozushiwa Mbowe kafa inakuwa sawa. Akizushiwa Lissu ni shoga inakuwa sawa,maana hatuwaoni mkikemea. Ila wakizushiwa wengine ndio noma yaani. Hamuoni kama mnaushangaza uzushi ndio maana unaamua kuwafanyia wehu? Wewe Makonda ulimzushia mtoto wa Mbowe ana korona. Nasema ulimzushia kwa sababu wewe hukuwa daktari. Unakumbuka ulipomzushia mzee Lowasa kuwa ametelekeza binti huko Kigamboni? Ukatengeneza movie kibao, hatujui ziliishia wapi.

Kabla ya hapo uliwazushia kina Mbowe madawa ya kulevya,kiko wapi?Mahakama ipi ikiwatia hatiani? Unakumbuka mlivyokuwa mnazushiana na Askofu Gwajima? Haaa haaa

Sasa imekuwa zamu ya dad kuzushiwa.

Siwatetei wazushi na wachuki ila nasisitiza Tupande amani na upendo kwa kila mtu, tupande haki na wajibu kwa kila mtu,halafu tusubiri kiangazi. Ila kwa sasa tunavuna tulichopanda. Usikute hata wewe wanakusubiri kwa hamu, ukutwe na baya wanywe bia.
Baada ya Meko kumtoa u-RC Makonda, anachoweza kuturingishia kwa sasa ni msambwanda tu. Maana baada ya Wema Sepetu kujikondesha yeye pekee ndiyo kabakia
 
My Take
Nami naungana na Paul Makonda kukemea chuki na uongo. Ila kabla sijakemea nina mambo ya kuhoji.

Yapi?
 
Roho za watu waliotangulia mbele ya haki badi zitaendelea kukulilia wewe na vitoto vyako hadi kiyama.

Bado wale ambao ulitumia cheo na ubabe wako kupora mali na fedha zao!
 
Warumi 13
1 Kila mtu hana budi kutii serikali inayotawala. Kwa maana hakuna mamlaka isiyotoka kwa Mungu; na serikali zote zilizopo zimewekwa na Mungu.
2 Kwa hiyo anayepinga mamlaka inayotawala ana pinga chombo kilichowekwa na Mungu; na watu wanaoasi watajiletea hukumu.
3 Kwa maana watawala hawatishi watu wanaotenda mema bali wale wanaotenda maovu. Kama hupendi kuishi kwa kumwogopa mwenye mamlaka, basi tenda mema naye atakusifu.
4 Maana mwenye mamlaka ni mtumishi wa Mungu kwa manufaa yako. Lakini kama ukitenda maovu, basi ogopa kwa maana hatembei na silaha bure. Yeye ni mtumishi wa Mungu anayetekeleza adhabu ya Mungu juu ya watenda maovu.
5 Kwa hiyo ni lazima kutii wenye mamlaka
Watawala hupenda sana maandishi haya katika Biblia kuhalalisha mamlaka yao, yawe ni ya halali au haramu, na pia kuwanyamazisha wale wanaotaka kujua ukweli kuhusu uhalali wa mamlaka yao.
 
Back
Top Bottom