Part 2: Ukikaribia Miaka 40 Utagundua Vingi mojawapo ni kuwa Zawadi kubwa Zaidi ni kujaaliwa Akili na kuijaza maarifa sahihi

Dr. Zaganza

JF-Expert Member
Jul 15, 2014
1,195
1,661
1665237807732.png
1665237823434.png


1665237844650.png

1665237913916.png


Moja ya misafara nilojifunza vitu vikubwa ndani ya muda mfupi , ni huu msafara niloamua kwenda kutalii Falme za kiarabu.

Nilianza Sharjah, huko nikakuta ni magodown ya bidhaa used yamejaa. Nikaenda Abuu dhabi kule ni makazi ya matajiri wa kiarabu na ndiko balozi za nchi mbali mbali ziliko. Nikamalizia Dubai hapo ndipo penye bidhaa original. Ziara yote hii ilikuwa ndani ya siku saba .

Ndani ya siku saba hizi, ilipofika jumapili maduka mengi hawafungui ni kama mapumziko. Nami nikaona ni fursa ya kutembelea Dubai mall sambamba na Burji khalifa.

Kutoka Samaya Hoteli nilikofikia hadi Dubai mall unatumia usafiri wa treni inayopita chini ya ardhi. Ndani ya treni wameweka tangazo la wanawake kukaa upande wao ,endapo mwanaume atakaa upande wa akina mama na askari akamkuta fani ni Dirham (AED) 200 kama tzs 127,000 hivi. (Dirham moja ni sawa na tzs 635 hivi)

Niseme Dubai hawatumii sharia za kiislam kwa 100% kama wanavyotumia Saudi Arabia, ila wamejitahidi kuheshimu uislam mfano barabara wameziita majina ya maswahaba (wanafunzi) wa mtume kama bara bara ya Abuubak Swidik (Khalifa au kiongozi wa kwanza wa uislam baada ya kufariki mtume mwaka 633), Bara bara ya Umar bin Khatwab (Khalifa au kiongozi wa pili wa uislam baada ya kufariki Abuubakr Swidik mwaka 635) , na bara bara ya Khaalid bin Waalid (Komandoo hodari wa ulinzi zama za mtume na makhalifa).

Pia kwenye vyumba vya hotel kwa juu kuna mshale unakuelekeza kibla (mahali waislam wanakotakiwa waelekee wakiwa wanaswali ambako ndiko iliko makkah)na wanakuwekea muswala (kijizulia ) wa kuswalia,

Basi, Treni inatufikisha Dubai Mall ,hapo kuna screen unasearch kama google unataka kwenda wapi ,kisha inakuonesha ramani na njia ya kufika uendako, maana humu kila maduka ya brand zote maarufu duniani. Lakini kubwa lilonipeleka ni aina ya samaki na viumbe walokusanywa humu unawaona kwa kulipia. Ukitaka pia kuna eneo la kujifunza ndege za emirate ila hauruki,ziko hapo hapo ardhini.

Kuona vivutio hapa Dubai mall pekee kabla ya Burji khalifa unalipia kama Dirham 400, na kama hautaki kukaa foleni unalipia Dirham 500 unapewa beji ya fast track , Hapo wahudumu wanasubirisha watu wengine ili mtangulie kwa kila hatua ya kivutio. Hadi hapa siyo lengo la makala yangu, bali hatua inayofuata.

Baada ya kumaliza vivutio vya Dubai mali, tukakata tiketi ya kupanda Burji khalifa, hapo unalipa kwa kadri unataka uishie floor ya ngapi. Kuna hatua tatu za floor .

Tuje mpaka juu ya jengo refu kuliko yote duniani. Jengo hili wenyeji wameliita Burji Khalifa.(Khalifa Tower) Nikisema refu namaanisha ni refu, umbali wa mita 828 toka Ardhini . uunganishe viwanja nane vya mpira wa miguu kisha uvisimamishe.

Hapo kuna hisia mbili unazipata ukiwa umbali huo. Moja furaha kuouona mji mzuri wa Dubai tokea juu.

Pili unapata hofu fulani unajiuliza kama tetemeko la ardhi likitokea?

Ziara inaisha Ninarudi hotelini .

HAPA NDIYO FIKRA ZANGU NAPENDA KUSHARE NANYI

Umri huu wa kulekea miaka 40 inahitaji upate walau dakika 60 za kutafakari kila siku.Hapa Napata muda wa kutafakari na ndiyo napenda kushare nanyi tafakari zangu., naangalia picha za mchana kutwa nakutana na vuta picha ya Dubai kabla ya 1970 ilikuwa sawa na nchi nyingi zinazoendelea, Lakini imezipita ghafla . Hapa nauliza wazoefu wa huu mji kwani Dubai wana mafuta kiasi gani? Kwa kifupi anasema wanakaribiana na Nigerian. Hapa nambandika swali lingiine fikirishi kwa nini Dubai imepiga hatua kubwa? Hapo kanipa siri kubwa ya akili ya uongozi alotumia Mfalme wa Dubai ,Mohamed bin Rashid Almaktoum, kwa kuona mafuta ya UAE , 94% yapo Abuu Dhabi , 2% yako Sharjah na Dubai wana 4% tu ya mafuta yote ya UAE ,alichofanya ni kugeuza Dubai kuwa mjii wa kibiashara. Baadhi ya mambo ya mapinduzi alofanya ni :

Sheria ya usajili na uwekezaji ambapo mwekezaji toka nje ya nchi, anatakiwa kuwa partner na mwenyeji raia wa Dubai. Na hapa maduka ya jumla mengi tulopita mabosi wa kwanza ni waarabu (wanaongea kiarabu zaidi) ambao wanakuwa zao majumbani ,kisha watendaji wa kila siku wanakuwa wahindi(wanaongea kiingereza) na wasaidizi kama kukaribisha wageni na kuwatembeza wanakuwa wengi ni waafrica magharibi(Wanaongea kifaransa na kiingereza) .(Alhamdulillah, lugha zote tatu nazielewa hivyo nawatafsiria watanzania watalii wenzangu).
  • Bidhaa toka nje zimeshushwa ushuru zaidi ili kuvutia makampuni kuleta bidhaa Dubai kwa kuwa Dubai hawazalishi bidhaa ila zinaingizwa toka nje hasa Japan, Taiwan na nchi zingine.
Ufalme wa Dubai unasimamia bidhaa zinazoingia Dubai ni original tu. Tulishuhudia mtaa wa Deira ule upande wa maduka ya vipuri tunahangaika kutafuta duka la Hyundai lilokuweko mwaka jana, Ndipo wenyeji wakatujulisha wamefungiwa baada ya kuingiza bidhaa chini ya kiwango (Kibongo bongo tunaita fake au FJ)
  • Kununua bidhaa Dubai kwa wageni unarudishiwa ushuru kwa kuwa hahuuzii pale ,utauzia nje ya Dubai .Hivyo ukishanunua ,wale wenye maduka ya jumla wanakuandalia fomu ya kudai (claim back) ushuru ulotozwa kwenye bidhaa.

  • Kitaalamu kama watu wengi wanaleta bidhaa na wengi wanafuata bidhaa unahitaji usafiri, na hapo shirika lao la ndege emirate likatumia fursa hiyo kuyapiku mashirika yote ya ndege duniani na kuwa uwanja ulio busy kwa ndege duniani ni emirate (DXB)

  • Ukiwa na wateja wanakuja na usafiri wako hapo unabuni utalii hata kama hauna vivutio.Utalii wa Dubai ni majengo marefu yalojengwa mpaka majengo mengine hayana wakazi wala si ofisi , yamejengwa kufanya mji uvutie.

  • Usalama wa hali ya juu. Ndani ya Dubai ni kazi kuona bastola hadi namaliza siku 7. Pia kwenye maeneo ya watu wengi ,polisi wamepaki gari zao aina ya VX masaa 24 na juu kuna Camera wanafuatilia nani anavunja sheria
Kweli mfalme Almaktoum amejaaliwa akili na kaijaza maarifa sahihi,yanayohitajika kutatua changamoto kwenye mazingira yake

Ni usiku mwingi sasa, inabidi kulala asubuh tuwahi Baniya square (Kariakoo ya Dubai) kufunga mzigo.
 
Tanzania hakuna mwenye uchungu na nchi.

Aliywahi kuwa na VISION na nchi hii ni Nyerere tu, Sera yake ya Ujamaa ilipofeli, sasa hivi hakuna nayejisumbua kujua nchi iende vipi, Bora kumekucha tu.

Hakuna mwnye VISION.

Siku hizi kazi ya Rais ni KUTEUA, KUTENGUA, KUHUDHURIA MAKONGAMANO, KUCHONGA MADAWATI na KULINDA URAIS wake Kwa MTUTU wa BUNDUKI.
 
Tanzania hakuna mwenye uchungu na nchi.

Aliywahi kuwa na VISION na nchi hii ni Nyerere tu, Sera yake ya Ujamaa ilipofeli, sasa hivi hakuna nayejisumbua kujua nchi iende vipi, Bora kumekucha tu.

Hakuna mwnye VISION.

Siku hizi kazi ya Rais ni KUTEUA, KUTENGUA, KUHUDHURIA MAKONGAMANO, KUCHONGA MADAWATI na KULINDA URAIS wakoo Kwa MTUTU was BUNDUKI.

Jaribu uwaulize tuko kwenye ujamaa au ubepari watakueleza hatufungamani na upande wowote kiufupi tuko kwenye sera ya unafiki, ni lazima uchague rangi moja nyeupe au nyeusi mambo ya sifungamani na blah blah ni unafiki mkubwa sana.
 
Mie akili yangu Ni Kama unatuonyesha kuwa uko Dubai ama Nimekosea kujua ulichoandikia Uzi. Ila najua Kuna Ile ego ya binadamu pia ipo kazini na dopamine imekupa euphoria na endorphins.
Ama ndio wewe unakaribia 40 so kuwa Dubai Ni akili?
Ama mfalme wa Dubai alikuwa na akili kuimeki ivyo Dubai?
Siko biased sema brain iko multidimensional ku draw different ideas why.


Ila big kubwa Kama umefikia kufuata mzigo Dubai utakuwa una akili na umeijaza maarifa.


Napenda jamii tujifunze icho ulichoijaza akili yako na wengine tuijaze pia.


Ila pia Ni kawaida yetu blacks tukiwa nje tunafurahia mno kuliko hata kuwa nyumbani kwetu.
Mana unamkuta black anarusha mtandaoni kuwa am enjoying to be Poland Ila Sasa akiwa kwao inaonekana haenjoi.


Mwenyewe natafuta hela ya apartment nihamie Brunei, Luxembourg,Austria, Switzerland,Australia ,new Zealand,,nawakaribisha mnipendekezee nchi nzuri kwa blacks huko nje Mana bongo sio kabisa.
 
Tanzania hakuna mwenye uchungu na nchi.

Aliywahi kuwa na VISION na nchi hii ni Nyerere tu, Sera yake ya Ujamaa ilipofeli, sasa hivi hakuna nayejisumbua kujua nchi iende vipi, Bora kumekucha tu.

Hakuna mwnye VISION.

Siku hizi kazi ya Rais ni KUTEUA, KUTENGUA, KUHUDHURIA MAKONGAMANO, KUCHONGA MADAWATI na KULINDA URAIS wakoo Kwa MTUTU was BUNDUKI.
Kazi iendeleeeeeeeee, ukinizingua tunazinguana hakuna vision.
 
Kibongo bongo watakuambia kujifunza ni ujinga hata biashara zetu nyingi tunaamini katika ndumba
 
Tanzania kinachonitia uchungu ni uraia. Yaani hatukosi Raia wenye vitambulisho vya wazawa.

Wageni wanakula maisha na ukizingatia pesa wanazipeleka kwao.

Security haiko vzr, ukiishi unaishi bure bure yaani viza Kwa Tanzania Haina maana yyt.

Rais abuni utendaji kazi fikirishi. Mfalme amejaaliwa hekma. Rais aombe mola amjaze hekma, atow maamuzi ya matendo sahihi.

Kutwa kucha maofsini Kwa wateule ni kutetea posho,wanaita stahiki za kishria...yaani wananyanyasa Sana wahudumu, manesi,walimu,polisi nk

Kifupi Karl Marx alisema

Upper vs lower.
Poor vs rich.
Leaders vs civilian.
Governor vs governed.

Yaani Yanga vs Simba ndio maisha tunayoishi.

Ukifika maeneo

Utawakuta.
Wakongo.
Wanywarwanda.
Warundi.
Waganda.
Wakenya.
Taja utakavyo wachina balaa.

Hapa niseme hakuna security watu hatuishi kwa anayestahili ainjoi nchi na ayestahili alipe Kwa kuishi hapa.
 
Mie akili yangu Ni Kama unatuonyesha kuwa uko Dubai ama Nimekosea kujua ulichoandikia Uzi. Ila najua Kuna Ile ego ya binadamu pia ipo kazini na dopamine imekupa euphoria na endorphins.
Ama ndio wewe unakaribia 40 so kuwa Dubai Ni akili?
Ama mfalme wa Dubai alikuwa na akili kuimeki ivyo Dubai?
Siko biased sema brain iko multidimensional ku draw different ideas why.


Ila big kubwa Kama umefikia kufuata mzigo Dubai utakuwa una akili na umeijaza maarifa.


Napenda jamii tujifunze icho ulichoijaza akili yako na wengine tuijaze pia.


Ila pia Ni kawaida yetu blacks tukiwa nje tunafurahia mno kuliko hata kuwa nyumbani kwetu.
Mana unamkuta black anarusha mtandaoni kuwa am enjoying to be Poland Ila Sasa akiwa kwao inaonekana haenjoi.


Mwenyewe natafuta hela ya apartment nihamie Brunei, Luxembourg,Austria, Switzerland,Australia ,new Zealand,,nawakaribisha mnipendekezee nchi nzuri kwa blacks huko nje Mana bongo sio kabisa.
Acha wivu
 
Tanzania hakuna mwenye uchungu na nchi.

Aliywahi kuwa na VISION na nchi hii ni Nyerere tu, Sera yake ya Ujamaa ilipofeli, sasa hivi hakuna nayejisumbua kujua nchi iende vipi, Bora kumekucha tu.

Hakuna mwnye VISION.

Siku hizi kazi ya Rais ni KUTEUA, KUTENGUA, KUHUDHURIA MAKONGAMANO, KUCHONGA MADAWATI na KULINDA URAIS wake Kwa MTUTU wa BUNDUKI.
Mkuu unakata tamaa mapema.
 
Sasa kwa aina ya maraisi na viongozi tunaopata kwa taifa letu unadhani tanzania ina miaka mingapi kufikia level ya huko uliko, au unadhani kipi hasa tunafeli kwa nini tusifike huko waliko wenzetu?

Kama wao waliona fursa kupitia rasilimali chache, wakabuni mbinu za kiuchumi kwa ajili ya taifa lao, unadhani sisi wenye rasilimali nyingi tunafeli wapi?
 
Acha wivu
Sijaweza kuunganisha heading na yaliyopo na Sina wivu sema labda nawewe umekuwa biased na mtizamo wangu. Kama nje nimesomea ulaya bado nikiwa early 20s. Ila mie nilitaka Sasa kuwa niyajue maarifa ambayo inatakiwa tuyajaze kabla ya our 40s. Mie napenda vijana wapigane Mana ukiwa nje unakutana na west Africa.

Yaani east Africa hatujawahi toa jamaa wakapiga soka uko Chelsea arsenal man u.
Hatuna wasomi wanaotingisha huko ulaya.
Wenye viwanda na kuweza kutoa Ajira hata 10k kwa watanzania wenzao Ni wachache Bali sio black labda wenye ngozi ya nguruwe ama nguruwee nawaita.



Sasa naomba unielekeze Mana mtu Kama dangote ataongea alichofanya akafikia zile level sie Tanzania hatuna tajiri ndani ya top 100 ya kidunia nadhani.


Wale dollar millionaire tunao wachache,dollar bilionaire sijui tupo wawili tu. Baresa na mo Kama wapo wengine Ni wanasiasa walioiba hela za wananchi wao Ila sio kwa kupigana.



Hata wewe inatakiwa uwe tajiri utoe Ajira kwa watanzania ama Basi hata kwa familia yako tu.

.Sasa nieelezee wivu imetokea wapi. Mie nimekuuliza kuwa Ni maarifa gani tuyajaze mkuu.
 
Nyerere kang'atuka mwaka 1985.

Ni zaidi ya MIONGO MITATU sasa. Nambie Dira ya nchi hii ni nini sasa?
Mi naamini tunafanya Kwa kasi yetu japo Kuna uboreshaji wahitajika ndo maana unaona hata mtaala wizara ya elimu unaurekebisha.

Nimeleta mada kama challenge pale timu moja inapojipima na nyingine
 
Back
Top Bottom