n00b
JF-Expert Member
- Apr 10, 2008
- 1,006
- 2,667
Wakuu,
Kama mlifuatilia hii thread - https://www.jamiiforums.com/jukwaa-...m/301102-papaa-musofe-mbaroni-kwa-mauaji.html basi hii leo jamaa anapandishwa kizimbani Kisutu kuhusiana na sakata hili.
Kama mlifuatilia hii thread - https://www.jamiiforums.com/jukwaa-...m/301102-papaa-musofe-mbaroni-kwa-mauaji.html basi hii leo jamaa anapandishwa kizimbani Kisutu kuhusiana na sakata hili.
Papaa Musofe alikamatwa kwa tuhuma za mauaji ya aliyekuwa mfanyabiashara mwenzake, Onesphor Kituri, mkazi wa Magomeni Mapipa, jijini Dar es Salaam.
Inadaiwa kuwa kabla ya mauaji hayo, Papaa Msofe alikuwa na mgogoro na marehemu wa kugombea nyumba ambayo ilikuwa imewekwa rehani kwa Shilingi milioni 30 ambazo Msofe alimpa marehemu kwa makubaliano kwamba akishindwa kuzilipa atachukue nyumba yake.
Papaa Msofe inadaiwa walikuwa wakimtishia maisha marehemu huyo.
Kwa mujibu wa taarifa za polisi, kutokana na vitisho hivyo, marehemu alifungua kesi mahakamani, lakini siku ya hukumu alikutwa akiwa amekufa mbele ya mlango wa nyumba yake huku kukiwa hakuna mali yeyote iliyochukuliwa.