Panya road hatari maarufu Mungu Moshi waibuka halmashauri ya Mlimba-Morogoro

lukoma

JF-Expert Member
Jul 1, 2013
2,995
2,245
Maisha na mali ya wananchi wa halmashauri ya Mlimba kata ya Mngeta na Mchombe yako hatarini kutokana na kuimbuka kwa kundi hatari la panya road maarufu kwa jina la Mungu moshi yaani bangi ndiyo Mungu wao. Vijana hawa kati ya miaka 15 mpaka 25 wanajihusisha na uporaji kwa kutumia mapanga, visu na nondo nyakati za jioni na usiku hasa siku za sikukuu. Inasadikika mmoja wao ambaye ndiye kiongozi wao anamiliki bastola ambayo ameiba kutoka kwa baba yake mstaafu wa usalama wa taifa.

Siku ya Idd Mosi mwaka huu kundi hili lilijeruhi watu kwa mapanga na visu eneno la Johnson bar na kupora vitu mbalilmbali. Vijana takribani 50 walikamatwa na kituo kidogo cha polisi Mngeta lakini siku 3 baadaye wote waliachiwa kwa kutoa pesa bila kuchukuliwa hatua yeyote.

Tofauti na panya road wa jiji la Dar, hawa wanafahamika kwa majina na makazi yao. Vijana hawa makazi yao yako Mngeta centre, mara kwa mara hukamatwa na polisi wanapofanya tukio na kuachiwa baadaye. Kwa kifupi polisi pia wanawafahamu kwa majina na makazi yao ila wamegeuza kitegauchumi chao!

Wito kwa wenye mamlaka, Mkuu wa wilaya, Mkuu wa mkoa na RPC kuchukua hatua haraka iwezekanavyo ili kunusuru mali na maisha ya wakazi wa halmashauri ya Mlimba. Pia polisi wa kituo cha Mngeta ambao wengi wao ni walevi na wanajihusisha na rushwa wazi wazi wachukuliwe hatua.
 
Hao vijana wakikamatwa wapigwe na waliwe tigo zao.
Ndugu zangu Wandamba na Wasukuma wa Mngeta, Chita, Mlimba mnakwama wapi?
Pigeni mbuzi hao.!!!
 
Hii inaonekana ni ka mpango kamewekwa na watu fulani ili kudhoofisha utawala wa mama.

Muda utasema...
Sawa hata kama mpango ndio apambane sasa, ndio maana ya kuwa kiongozi...! Mlitaka aongoze kiulaini tu kama alivyoupata uraisi?
 
Hii inaonekana ni ka mpango kamewekwa na watu fulani ili kudhoofisha utawala wa mama.

Muda utasema...
Mi sidhani kama ni mpango wa kumdhoofisha huyo mama ila nafikiri ni ugumu tu wa maisha, halafu wale machinga waliotapakaa kila mahali hata kutembea kwa miguu ilikuwa ni shida! Hivi wameenda wapi wale!?

Fikiria kama tena akitokea mwanasiasa mwingine apige marufuku bodaboda bila kuwawezesha kujipatia riziki kwa namna nyingine kitafuata nn?
 
Maisha na mali ya wananchi wa halmashauri ya Mlimba kata ya Mngeta na Mchombe yako hatarini kutokana na kuimbuka kwa kundi hatari la panya road maarufu kwa jina la Mungu moshi yaani bangi ndiyo Mungu wao. Vijana hawa kati ya miaka 15 mpaka 25 wanajihusisha na uporaji kwa kutumia mapanga, visu na nondo nyakati za jioni na usiku hasa siku za sikukuu. Inasadikika mmoja wao ambaye ndiye kiongozi wao anamiliki bastola ambayo ameiba kutoka kwa baba yake mstaafu wa usalama wa taifa.

Siku ya Idd Mosi mwaka huu kundi hili lilijeruhi watu kwa mapanga na visu eneno la Johnson bar na kupora vitu mbalilmbali. Vijana takribani 50 walikamatwa na kituo kidogo cha polisi Mngeta lakini siku 3 baadaye wote waliachiwa kwa kutoa pesa bila kuchukuliwa hatua yeyote.

Tofauti na panya road wa jiji la Dar, hawa wanafahamika kwa majina na makazi yao. Vijana hawa makazi yao yako Mngeta centre, mara kwa mara hukamatwa na polisi wanapofanya tukio na kuachiwa baadaye. Kwa kifupi polisi pia wanawafahamu kwa majina na makazi yao ila wamegeuza kitegauchumi chao!

Wito kwa wenye mamlaka, Mkuu wa wilaya, Mkuu wa mkoa na RPC kuchukua hatua haraka iwezekanavyo ili kunusuru mali na maisha ya wakazi wa halmashauri ya Mlimba. Pia polisi wa kituo cha Mngeta ambao wengi wao ni walevi na wanajihusisha na rushwa wazi wazi wachukuliwe hatua.
Jina la Panya Road linatokana na vijana hawa wa. DSM Kukaba kwenye vichochoro ambavyo tunafananisha na njia za panya na walipoamua kujitokeza hadharani ndipo jina lao kikabakia hivyo hivyo sasa hao wa uko Mngeta ni Mungu Moshi ni Genge la kihalifu maana Mngeta hakuna panya road hivyo siyo sahihi kuwaita Panya Road wewe ikibidi waite Manyani pori maana huko kumejaa misitu.
 
Back
Top Bottom