Nyankurungu2020
JF-Expert Member
- Oct 2, 2020
- 4,086
- 6,568
Hili halina ubishi 85% ya wabunge wapo mjengoni kupitia mgongo wa Rais Magufuli, maana wengi wamechaguliwa kwa huruma za wananchi baada ya Rais kuwapigia debe majukwaani. Wao kama wao wasingetoboa hata kwa tindo na kotapini.
Napiga picha jinsi mbunge wa Geita mjini ambavyo alikuwa hakubaliki kwa wananchi mpaka akalazimishwa na Rais kuomba msamaha kwa wananchi mbele ya hadhara. Kama sio JPM huyu mbunge asingerudi mjengoni.
Sitaki kuongea mengi juu ya huyu mbunge bali wakazi wa Geita ni mashuhuda. Lakini amestaajabisha watu pale alipoamua kujitoa ufahamu na kutetea uovu ambao haustahili kutetewa hata kwa namna yoyote.
Hata kama hakuna ufisadi, unaweza kutetea manunuzi ya gari ya mil 460? Wakati wananchi wako wanaishi kwenye lindi la umaskini! Hivi huyu mbunge anapajua Shilabela? Nyankumbu na maeneo ya watu hohehae? Anajua maisha ya Geita kwa undani? Hivi Rais Magufuli alikuwa anapigia chapuo wabunge kama huyu?
Huyu ni mfano tu, nenda jimbo la Ilemela huko Mwanza. Ni kwamba wananchi hawamkubali huyu mama tena ni waziri mdogo. Lakini ukikaa maeneo ya Ilemela wananchi wana kilio kikubwa sana. Maji, barabara na miundombinu ni shida tu. Ni kama hawana mbunge kwa zaidi ya miaka mitano. Maana ni kero na shida.
Kwa ufupi Magufuli kama mwenyekiti wa CCM awe makini na wabunge ambao aliwapigia debe lakini pindi akiondoka madarakani atatuachia kilio kikubwa sana watanzania. Maana bungeni ni kama hatuna wawakilishi.
Rais anapinga matumizi ya pesa za umma yasiyofaa mbunge anatetea. Hivi hii Tanzania yetu imemkosea Mungu. Any way nimetoa mifano miwili ila tutaoumia ni sisi wanyonge ambao hatuna mbele wala nyuma.
Napiga picha jinsi mbunge wa Geita mjini ambavyo alikuwa hakubaliki kwa wananchi mpaka akalazimishwa na Rais kuomba msamaha kwa wananchi mbele ya hadhara. Kama sio JPM huyu mbunge asingerudi mjengoni.
Sitaki kuongea mengi juu ya huyu mbunge bali wakazi wa Geita ni mashuhuda. Lakini amestaajabisha watu pale alipoamua kujitoa ufahamu na kutetea uovu ambao haustahili kutetewa hata kwa namna yoyote.
Hata kama hakuna ufisadi, unaweza kutetea manunuzi ya gari ya mil 460? Wakati wananchi wako wanaishi kwenye lindi la umaskini! Hivi huyu mbunge anapajua Shilabela? Nyankumbu na maeneo ya watu hohehae? Anajua maisha ya Geita kwa undani? Hivi Rais Magufuli alikuwa anapigia chapuo wabunge kama huyu?
Huyu ni mfano tu, nenda jimbo la Ilemela huko Mwanza. Ni kwamba wananchi hawamkubali huyu mama tena ni waziri mdogo. Lakini ukikaa maeneo ya Ilemela wananchi wana kilio kikubwa sana. Maji, barabara na miundombinu ni shida tu. Ni kama hawana mbunge kwa zaidi ya miaka mitano. Maana ni kero na shida.
Kwa ufupi Magufuli kama mwenyekiti wa CCM awe makini na wabunge ambao aliwapigia debe lakini pindi akiondoka madarakani atatuachia kilio kikubwa sana watanzania. Maana bungeni ni kama hatuna wawakilishi.
Rais anapinga matumizi ya pesa za umma yasiyofaa mbunge anatetea. Hivi hii Tanzania yetu imemkosea Mungu. Any way nimetoa mifano miwili ila tutaoumia ni sisi wanyonge ambao hatuna mbele wala nyuma.