Makamura
JF-Expert Member
- May 19, 2022
- 356
- 550
TANZIA -JIMBO KATOLIKI LA BUKOBA
Askofu Method Kilaini, anawatangazia kifo cha padre Asterius Mutegeki, kilichotokea tarehe 18 Agosti 2023 kwa jali ya pikipiki. Padre Asterius ni kijana aliyepadrishwa mwaka jana Julai 2022. Ni mzaliwa wa visiwa vya Bumbile na Padre wa kwanza kutoka visiwa hivyo. Ni majonzi makubwa. Alikuwa anafanya kazi katika Parokia ya Ishozi wilaya ya Misenyi Jimboni Bukoba.
Pole sana kwa Ta Wincheslaus Barongo baba yake Pamoja na Mama yake na wana Bumbile wote. Pole kwa mapadre, watawa na waamini wa jimbo la Bukoba na kanisa zima la Tanzania.
Sote tumwombee kwa Mungu apumzike kwa amani Amina.
RAHA YA MILELE UMPE EE BWANA NA MWANGA WA MILELE UMWANGAZIE APUMZIKE KWA AMANI.
Askofu Method Kilaini
Msimamizi wa Kitume Jimbo Katoliki la Bukoba