Padre Godfrey Jackson Mwasekaga ateuliwa kuwa Askofu Msaidizi Jimbo Kuu la Mbeya

Chachu Ombara

JF-Expert Member
Dec 11, 2012
5,897
10,358
Mwasekaga.jpg

Baba Mtakatifu Fransisko amemteua mheshimiwa sana Padre Godfrey Jackson Mwasekaga wa Jimbo Kuu katoliki la Mbeya kuwa Askofu Msaidizi wa Jimbo kuu la Mbeya , leo tarehe 09.03.2024

Mhashamu Askofu mteule Godfrey Jackson Mwasekaga alizaliwa Machi 17 mwaka 1976 Kyela, jimbo kuu Katoliki la Mbeya.

Baada ya Masomo yake ya upadre, alipata daraja takatifu la upadre Julai 14 mwaka 2005 jimboni Mbeya , kuhudumu katika nafasi mbalimbali za utume ndani ya jimbo Kuu la Mbeya. Hadi uteuzi wake Askofu Mteule Mwasekaga alikuwa Makamu Askofu wa Jimbo kuu la Mbeya.

photo_2024-03-09_14-45-55.jpg
 
IMG_20240309_144739_733.jpg

Baba Mtakatifu Fransisko amemteua Mheshimiwa sana Padre Godfrey Jackson Mwasekaga wa Jimbo kuu Katoliki la Mbeya kuwa Askofu Msaidizi wa Jimbo kuu la Mbeya, leo tarehe 09.03.2024.

Mhashamu Askofu mteule Godfrey Jackson Mwasekaga alizaliwa Machi 17 mwaka 1976 Kyela, Jimbo kuu Katoliki la Mbeya.

Baada ya masomo yake ya upadre, alipata daraja takatifu la upadre Julai 14 mwaka 2005 jimboni Mbeya, na kuhudumu katika nafasi mbalimbali za utume ndani ya Jimbo kuu la Mbeya. Hadi uteuzi wake Askofu mteule Mwasekaga alikuwa Makamu Askofu wa jimbo kuu la Mbeya.

Imetolewa na Baraza la Maaskofu Katoliki Tanzania.
 
Ashakum si matusi Ndio kumanisha ipo juu ya uwezo wako.
Kuna wakati mwingine kukaa kimya ni bora kuliko kuongea.Kanisa limebahatika kupata watu wengi sana watakatifu na wengine wameleta majanga makubwa.

Ukiona sifa nyingi sana mitandaoni na kwenye media, basi fikiri mara mbili mbili.
Mfano, aliyebadili au kufanyia reforms Catholic Mass, during Vatican II alikuwa msomi, thinker and above all, trustworth in the human eyes. Baada ya kufanya yote, ikajulikana ameharibu misa sababu alikuwa Freemasonry, aliyepewa kazi maalumu ya kuharibu mambo. Ndio maana leo taratibu tunaanza kucheza mdundiko kanisa. Jina lake alikuwa Askofu Annibele Bugnini(What Bugnini Was Thinking When He Destroyed the Catholic Mass)

Baadae pia ilijulikana hayo yaliwezekana sababu aliyekuwa anapendekeza Cardinals and Bishops, Cardinal Sebastiano Baggio naye alikuwa Freemasonry na wana nzengo wengi wanamuhusisha yeye na Cardinal Jean- Marrie Villot kuhusika na kifo cha Pope John Paul I.

Kwahiyo pengine unafikiri ipo juu ya uwezo wangu...lakini kumbe ipo kwenye uwezo wa chini kuliko wangu
 
Back
Top Bottom