Kiby
JF-Expert Member
- Nov 16, 2009
- 6,933
- 4,706
Lakini huo mstari ndio kauli ya Yesu kuhusu ndoa na talaka. Na Bwana Yesu ni absolute ya mkristo.Ukitaka kuelewa kusudio la jambo fulani kuwekwa na Mungu inabidi usome kwa mapana kile alichosema kwenye maandiko tofauti ili upate ukamilifu wa fundisho la Mungu. Mume na mke ni mwili mmoja na kama Mungu anasema ni mwili mmoja iweje tena aruhusu kuwe na sababu ya kufanya mwili huo kutengana? Mantiki tu ya mwili mmoja ni kifungo kuwa hakuna kutengana.
Pili hata Yesu wakati anawajibu waliomuuliza habari za talaka kuwekwa na Musa aliwaambia Musa aliweka sababu ya mioyo yenu migumu! Maana yake talaka si mpango wa Mungu na hapo ndipo Yesu akawa ametilimiza torati kama alivyotimiliza kwenye mengine.
Kwa ujumla hako ka mstari ndio kamekuwa kakileta ushetani wa talaka kwa baadhi ya makanisa hasa binafsi. Hakuna mstari mwingine unaounga mkono talaka na ndio maana tunapopata wanazuoni kama hawa akina Padre Amigu kufafanua tunaelewa kwanini ilikuwa ha make sense huo mstari kuwepo kama umesoma maandiko yote juu ya ndoa.
Sent using Jamii Forums mobile app
Sent using Jamii Forums mobile app