Osama bin Laden killed!

Osama bin Laden killed!

Status
Not open for further replies.
UMOJA wa Taifa (UN), umeitaka Marekani kueleza sababu za kumuua Kiongozi wa Kundi la Al-Qaeda, Osama bin Laden, badala ya kushughulikia suala lake kwa kufuata taratibu za kisheria.Inaelezwa kuwa wakati anavamiwa na kuuawa na makomandoo wa Marekani, katika kasri lake nchini Pakistan, bin Laden, hakuwa na silaha.

Kiongozi huyo wa mtandao wa kigaidi, aliuawa Jumatatu wiki hii.Taarifa ya Ikulu ya Marekani, jijini Washiton, ilisema mashushushu wa Marekani, walilazimika kumuua bin Laden kufuatia kitendo chake cha kukataa kukamatwa.

Hata hivyo Ofisa Mkuu wa Umoja wa Mataifa (Haki za Binadamu), Navi Pillay, alisema ingawa bin Laden alikuwa ni mtu hatari, lakini operesheni ya kukamatwa kwake, ilistahili kufuata taratibu za kisheria.

Wito huo unakuja wakati tayari Rais Barrack Obama wa Marekani, akiwa amesema "hatuwezi kumpa fursa bin Laden au mshirika wake, kulinyoshea silaha jeshi letu."

Na hivyo ndivyo ilivyokuwa, hakukuwa na komandoo yeyote wa Marekani aliyejeruhiwa katika operesheni hiyo ingawa, kulikuwa na mashaka makubwa wakati helikopta moja ilipopata hitilafu ya kiufundi na kuharibiwa na makondoo wa Osama.

Leon Panetta, Mkurugenzi wa CIA, aliliambia Shirika la Habari la NBC kuwa kikosi hicho kilipewa amri ya kumuua Osama."Lakini hii pia ilitegemea mazingira ya operesheni yenyewe. Kama angenyoosha mikono juu (Osama) na kujisalimisha kwa kikosi hicho, kwa vyovyote vile asingeuawa," alisema.

Bin Laden, (54) alikuwa mwanzilishi na Kundi la al-Qaeda na inaaminika kuwa aliamuru mashambulizi yaliyotokea katika majiji ya New York na Washington 11 Septemba 2001.Hali kadhalika mashambulizi mengine yaliyouawa watu katika nchi mbalimbali duniani.
 
Wakati kiongozi wa Iraq SADAM HUSSEIN anakamatwa na kikosi cha CIA aliteswa na kudhalilishwa na mpaka kutangaza waziwazi siku yake ya kunyongwa ambaye ilikuwa desember siku ya IDD tena,imekuwaje leo kwa gaid kama ossama wasimdhalilishe?Au ossama aliwatendea mema kiasi gani mpaka wamuheshi kiasi hicho?kwanini wamzike baharini?nafasi zimeisha nchi kavu nini?Tusidanganyane hizo ni mbinu za kisiasa 2!
 
kama kawaida ya politician sasa wameshageuza issue hii kama mtaji wa kisiasa kwenye kampeni za next election watasema ukweli
 
Unajua Kilimasera,mi mpaka leo siamini kwamba huyu jamaa kafa!! sijui hii theory nimeitoa wapi?
 
yaanimi sielewi hata kidogo hawa pakistani wanaposema eti walikuwa hawajua kama osama alikuwa nchini mwao...yaani sielewi kabisa...yaani jamaaa ananunua mpaka magazeti na mtu wa kupeleka maziwa asubuhii....hahaaa kweli kazi ipo ....obama mi na salute kwako bana hata kama hutaki kurilizi pichaz za osama
 
Hii picha inasemekana ni ya mke mdogo wa Osama aliyepigwa risasi ya mguu.

372685-bin-laden-wife.jpg
obl-wife.jpg

Geo Tv
 
Nakupenda NYANZALA wangu.........Nimgaya Sida beeh niangusage sambi si zako!!nimeipenda sana quote yako kigogo
yaanimi sielewi hata kidogo hawa pakistani wanaposema eti walikuwa hawajua kama osama alikuwa nchini mwao...yaani sielewi kabisa...yaani jamaaa ananunua mpaka magazeti na mtu wa kupeleka maziwa asubuhii....hahaaa kweli kazi ipo ....obama mi na salute kwako bana hata kama hutaki kurilizi pichaz za osama
 
mimi bado sijaelewa kwa nini wamarekani wamefanya mauaji hayo katika mazingira ya usiri sana!!!! na vile vile kama kweli wamedhamiria kumaliza ugaidi duniani kwanini wamuue??? kumkamata hai kungewawezesha kupata taarifa nyingi sana kuhusiana na shughuli za mtandao huo wa alqaeda. Hii inanifanya mimi niamini kwamba Osama hajauwawa na wamefanya hivyo ili kuepuka kelele za mataifa na mashirika mbali mbali ya haki za binaadamu za kutaka kumuona na kuzungumza nae. vile vile usiri huu utaondoa uwezekano wa wafuasi wake kujaribu kumuokoa.
 
siziga mie naamini amefariki kweli sababu hata fmilia yake imethibitisha yaani watoto wake na baadhi ya wake zake
Unajua Kilimasera,mi mpaka leo siamini kwamba huyu jamaa kafa!! sijui hii theory nimeitoa wapi?
 
Wakati kiongozi wa Iraq SADAM HUSSEIN anakamatwa na kikosi cha CIA aliteswa na kudhalilishwa na mpaka kutangaza waziwazi siku yake ya kunyongwa ambaye ilikuwa desember siku ya IDD tena,imekuwaje leo kwa gaid kama ossama wasimdhalilishe?Au ossama aliwatendea mema kiasi gani mpaka wamuheshi kiasi hicho?kwanini wamzike baharini?nafasi zimeisha nchi kavu nini?Tusidanganyane hizo ni mbinu za kisiasa 2!

Mkuu fanya kukumbuka Sadam alikuwa chini ya mikono ya nani mpaka ananyongwa.
 
hakikka atakumbukwa kwa mengi aliyoyafanya katika kupigania haki
 
Mkuu fanya kukumbuka Sadam alikuwa chini ya mikono ya nani mpaka ananyongwa.
Haa haa haaa! Huwa hawana muda wa kufanya utafiti hao! Wanakurupuka kubandika threads humu! Sasa waliopo Pakistani wanaswali kumuombea Osama, wewe upo Tandika unasema unadanganywa! Endelea kusubiri ukweli!
attachment.php
 
hakuwa mp[iganaji wala nini muoga sana huyu

Osama alikuwa mtu wa ajabu sana ..anawambia wenzake wakajilipue kumbe yeye mwenyewe ni mwoga wa kifo....halafu yale majani(bangi) inayomea pale kwenye makazi yake alikuwa anapiga msuba nini huyu jamaa?
 
haki ipi sasa?kwasababu bongo waliokufa wengi pale ubalozi walikua waislam!!mie mnaposema haki hata siwaelewi na mashambulio mengi wanayofanya hawa jamaa hayaangalii kwamba huyu mkristo au muislam!
hakikka atakumbukwa kwa mengi aliyoyafanya katika kupigania haki
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom