a. Je NSSF wamekosea wapi:- Hili swali hamjalijibu tangia muanze mjadala badala yake ni speculations tu na tuhuma zisizo na msingi.
b. Pili evidences za tuhuma:- Kuna mtu hapa ameomba mpaka financial statements za NSSF kwani asitafute ofisini mwao au katika vyama vya wafanyakazi? Until now there is no evidence whatsoever about embezzlements. Badala yake again ni speculation.
Dr Dau hajatajwa but who heads NSSF? why all the interest ziende kwa Dau wakati kimtazamo wangu this DG is just investing kupanua mfuko kwa kutake risks on investing? To me kinachoendelea PPF ni hatari zaidi kuliko NSSF maana pesa zetu zinaenda mifukoni mwa watu sio huyu anayewekeza.
Hili ni suala la 'brain storming' na si la 1+1=?.
Kama ulisoma post ya Kobello, yeye anasema mafisadi wa
wall street wamemtia hasara katika kitu kinaitwa 401K. Katika mjadala tumeona kuwa NSSF ni pesa za umma wewe na mimi tukiwemo.Anguko lake ni anguko letu kama lile la 401 ya Kobello.
NSSF imejiingiza katika mradi wenye utata, ambao mmiliki hajulikani, mara Tanpower, mara serikali mara STAMICO ilimradi tu kuna vurugu fulani za kifisadi. Unakumbuka PM Pinda alivyoliepusha jambo hili na Anne Makinda hataki kulisikia Bungeni, wewe unadhani ni nini. Hawa wanajua kuwa kuna uchafu mkubwa. Sasa NSSF inapokimbilia haraka kuwekeza pesa zetu, tena tukijua kuwa kuna utata, hapo inafikirisha.
Watu wanaonyesha wasi wasi kwanini NSSF imejiingiza kwenye sekta ya nishati hasa umeme, na ni huko huko mafisadi wameua Tanesco, kama shirika la umma litasalimika vipi na wezi hao. Ndio maana watu wanasema ingekuwa rahisi kusafisha kile kilichopo na NSSF wawekeze kwa Tanesco, tena si kiwira tu hata umeme wa dharura n.k kama wadau walivyochangia. Haya ni kwa uchache tu kukufafanulia kuwa hakuna jibu la 1+1=? katika masuala yanayohitaji analysis.
Ama kuhusu Dau, hapo ndio umekosea, eti kwasababu DG ni Dau na mada ni NSSF basi anashambuliwa! hii ni paranoia ya hali ya juu sana.Unachotaka kusema,kwa vile mkurugenzi wa ATC na Mwenyekiti wa bodi ni waislam basi ikisemwa ATC inaandwamwa. Huu ni ugonjwa hatari sana ndugu yangu, fikiri tunapoongelea Tanpower(Mkapa na Yona) wanashambuliwa wakristo! Tukiongelea Richmond ya Lowassa wanashambuliwa walutheri, tukiongelea PPF wanashambuliwa wakristo.
Mdondoaji, huu ni ugonjwa mbaya sana na unahitaji ushauri ndugu yangu.
Mimi ni ninapinga vikali sana mambo ya udini na nachukia sana hata kuandika tu kuhusu haya.
Inabidi ufikirie zaidi, NSSF ikiingia mkenge na miradi ikafa ni pesa yako. Dau hakujui wewe kama Mdongoaji bali mteja. Kobello kaonja joto 401 sasa huko nako yupo Dau!.
Madudu ya Dowans bili umeletewa wewe, madudu ya IPTL bili umeletewa na unalipa wewe, madudu ya Kiwira kodi yako imemlipa Yona na Mkapa. Ni wewe na mimi si dini zetu, watu wakichukua 10% familia zao zinaishi kwa raha kama ya Chenge, wewe mdondoaji unayetetea udini unamenyeka tu na bei kubwa ya umeme nyumbani , msikitini au kanisani.
Usitetee kitu kisichokusaidia katika maisha yako, sijui kama Dau anakujua wewe!! kama si pesa yako ya NSSF.
Hatuhitaji viongozi kwa majina au imani zao bali uwezo wao wa kuongoza. Mdondoaji maneno yako yanaidhalilisha jamii unayoiwakilisha na si amini kuwa jamii hiyo inafurahia au kukuunga mkono kwa hoja nyepesi kuwa NSSF ikisemwa ni DG ambaye anaitwa Ramadhani anaandamwa. Inferiority complex ni kitu kibaya sana, inaondoa confidence na kujenga paranoic society. Labda nikuulize kwa Ramadhani Dau kuwa muislam inasaidiaje?? na kama angekuwa mkristo ingeathiri vipi. Tusaidie kujibu haya, maana inaonekana DG kuwa dini fulani kuna mafao fulani, please tuambie.
Nimekushauri, angalia structure ya NSSF top to bottom halafu upime maneno yako kana uliyaandika kwa kufikiri au kusikia tu vijiweni.
Ukijikwaa angalia sababu iliyokuangusha!!. Wewe ni matunda ya chuki za mzee aliyeandika kitabu akashindwa kujibu hoja huku akitaka tuamini tu maandiko yake, kama unavyotaka tuamini kuwa DG anashambuliwa kwa imani na si NSSF.