Ombi Maalum, Uchaguzi wa Serikali za Mitaa na Uchaguzi Mkuu wa 2020, Uendeshwe kwa Ceteris Peribus, Sio Kwa Mutatis Mutandis. Tutabarikiwa!

Pascal Mayalla

Platinum Member
Sep 22, 2008
50,494
113,590
Wanabodi,
Hili ni ombi maalum kwa watu maalum, hivyo hii thread sio thread ya watu wote bali ni thread maalum kwa watu maalum na lengo maalum la
kutuma ujumbe maalum kabisa kwa watu maalum kabisa.

Tanzania sio nchi ya watu fulani tuu au chama fulani tuu, Tanzania ni nchi ya Watanzania wote, wa vyama vyote, wa dini zote, wa makabila yote, wa jamii zote, wa jinsia zote, wa rangi zote, wa hali zote za maisha, matajiri na masikini na Watanzania wa circumstances zote.

Mimi nikiwa mwandishi wa habari, nimeshuhudia chaguzi zetu zote za vyama vingi, zimekuwa zikiendeshwa kwa mtindo wa "Mutatis Mutandis"

Hivyo sasa tunapokwenda kwenye uchaguzi, naomba kutoa ombi maalum na angalizo muhimu kwa wahusika wakuu wa uchanguzi huu wa Serikali za Mitaa na Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2020, uendeshwe kwa kutumia kanuni ya Kilatini ya "ceteris paribus" na sio kutumia zile kanuni zetu za kawaida za "Mutatis Mutandis"!.

Nimesikia sauti, "voices from within" kuwa tukiendelea kufanya chaguzi zetu kwa Mutatis Mutandis, kuna janga fulani litatokea.

Wahusika wakuu wa uchanguzi huu, wakikubali uchaguzi wa serikali za mitaa wa 2019 na uchaguzi Mkuu ujao wa 2020, kuendeshea kwa ceteris paribus , taifa Letu litabarikiwa, na viongozi wetu wabarikiwa, na sisi wananchi wa kawaida pia, tutabarikiwa na kupata neena na mafanikio makubwa, na nchi yetu kupata ustawi mkubwa wa kisiasa, kiuchumi na kijamii, lakini tukiendelea kutumia ule mtindo wetu wa mutatis mutandis, taifa tutalaaniwa na viongozi wetu watalaaniwa na kuadhibiwa!, and you never know ni adhabu gani viongozi wetu wakuu wataadhibiwa!.

Mungu Mbariki Rais Magufuli, na watendaji wake wapate uwezo, watumie "Ceteris Peribus" kwa vyama vyote na sio kuendeleza "Mutatis Mutandis"

Mungu ibariki Tanzania.

NB. Sijaweka ufafanuzi wa maneno "Ceteris Peribus" na "Mutatis Mutandis" sio kwa bahati mbaya, nimefanya hivi kwa makusudi Maxima, kwa sababu ujumbe huu ni ujumbe maalum na mahsus kwa watu maalum na mahsus ambao mimi nawajua huwa wanatembelea sana jf, kwa vile watu hao, wanayajua maneno hayo. Wengine wasio husika hayawahusu, hivyo sikufafanua ili ujumbe huu uwafikie walengwa tuu.

Hata Mungu alipotaka kumfikishia ujumbe maalum mfalme Belshaza, alimtumia kiganja cha mkono kikaandika kwenye ukuta wake, "Mene Mene Tekeli na Peresi", tukiendelea kufanya chaguzi zetu kwa Mutatis Mutandis badala ya kutumia
Ceteris Paribus, then kuna siku Mene Mene Takeli na Peresi itakuja kuishukia Tanzania na kumshukia kiongozi wetu!.

Nawatakia Weekend Njema,

Paskali.
 
Mkuu, ingawa umeweka huu ujumbe maalum kwa watu maalum na kutoa sababu ya kutofafanua maana ya hayo maneno ya kilatin, nadhani kulikuwa na haja ya kututoa matongotongo nasi pia kwa sababu watu hao maalum watatuhitaji sisi ili kulitekeleza jukumu lao in one way or the other.

Naamini tukidokezwa walau tutajua kama wanatumia lipi kati ya hayo mawili (naogopa kuyaandika au kukopi nisije nikakosea ninaposoma)
 
Bila kujali hao uliowalenga maadamu mada iko hapa jukwaani tutachangia tunavyoona, na watakaotuelewa ndio walengwa. Kwa sasa ukweli umedhihirika kuwa wananchi wameshabadilika, wanajitambua na hawako tayari kumchagua yoyote bila ridhaa yao kisa katekeleza sehemu fulani ya wajibu wake. Haya yanayoendelea sasa ya kupika idadi ya wapiga kura yamedhihirisha ccm imeishiwa na ushawishi, hivyo namna pekee ni kutumia njia ya hujuma kuendelea kubaki madarakani. Hata hiyo 2020 wanaweza kutumia mbinu hizi hizi chafu kubaki madarakani, ila ifahamike sio kwa ridhaa ya wananchi bali mabavu ya dola fullstop.
 
Ceteris paribus or caeteris paribus is a Latin phrase meaning "other things equal"; English translations of the phrase include "all other things being equal" or "other things held constant" or "all else unchanged".



Mutatis mutandis is a Medieval Latin phrase meaning "having changed what needs to be changed"
Mkuu, ceteris paribus meaning other factors affecting the current scenario remaining constant. You must maintain the status quo of present circumstance.
 
Pascal anaomba fair play kwa washiriki wote.

Fair play ni ngumu maana walioko madarakani hawawezi kushinda, na hilo kwao ni bonge ya aibu kwani wametengeneza propaganda kuwa wanakubalika halafu wakaamini propaganda yao. Hatimaye imefika muda wa uchaguzi wa kudhibitisha kukubalika kwao, watu wamegoma kujiandikisha mpaka imebidi ipikwe idadi ya wapiga kura kuficha aibu. Katika mazingira hayo fairness inatoka wapi? Paskali kaleta huu uzi baada ya kuona uhayawani unaondelea kwenye mchakato huu wa uchaguzi hivi sasa.
 
Serikali inafeli pakubwa sana kutaka viongozi wa serikali za mitaa wawe wana ccm, ingeacha uku chini wanainchi wamue wenyewe leo hii uhuni uhuni tu unafanyika wagombea wanapewa form feki eti wakirudisha zikataliwe nawasihi wana CHADEMA hakikisheni wagombea wenu wanaangalia hizi form kuna feki na original sasa akienda mgombea wa upinzani anapewa form feki ili akirudisha akataliwe na abanwe katoa wapi hiyo form so ni ujinga ujinga tu unafanyika
 
Back
Top Bottom