Mnaonaje Uchaguzi wa Serikali za Mtaa Ufanywe Siku Moja na Uchaguzi Mkuu na Usimamiwe na Tume Huru ya Uchaguzi? Samia Atabarikiwa Sana!

Pascal Mayalla

Platinum Member
Sep 22, 2008
50,506
113,626
Wanabodi,
Kama kawaida yangu, kila nipatapo fursa, huja na makala zangu za kwa maslahi ya taifa.

Hili ni swali la pendekezo uchaguzi wa serikali za mitaa mwakani, usogezwe na kufanyika 2025, ufanyike siku moja na uchaguzi mkuu wa 2025, na usimamiwe na Tume huru ya uchaguzi, by that time pia ile dhulma ya kipengele batili ndani ya Katiba yetu iwe imeondolewa na sheria ya uchaguzi kurekebishwa ili haki za Watanzania kuchagua na kuchaguliwa, zilizoporwa kiubatili, zirejeshwe?

Nimekuwa inspired kupandisha bandiko hili, baada ya kumsikia Rais Samia, akikizungumzia kitu fulani alicho kiita kivumbi hivyo amemteua mtu mwenye kifua pale Tamisemi!
Msikilize Rais Samia
Nikimnukuu Rais Samia "mwakani kuna kivumbi, mimi nakujua, najua unaweza, kivumbi kile kinafanana na kifua chako, najua unaweza, mwakani ni kazi kazi, ili tu sail vizuri".

Japo hapa hakikusemwa ni kivumbi cha nini, ila waelewa tumeisha elewa hiki ni kivumbi cha uchaguzi wa serikali za mitaa!.

Ushauri huu wa leo, niliwahi kuutoa kabla ya uchaguzi wa serikali za mitaa wa mwaka 2019, nilitoa ombo maalum na nilishauri Ombi Maalum, Uchaguzi wa Serikali za Mitaa na Uchaguzi Mkuu wa 2020, Uendeshwe kwa Ceteris Peribus, Sio Kwa Mutatis Mutandis. Tutabarikiwa!

Katika bandiko hilo, nilishauri
Wanabodi,

Tanzania sio nchi ya watu fulani tuu au chama fulani tuu, Tanzania ni nchi ya Watanzania wote, wa vyama vyote, wa dini zote, wa makabila yote, wa jamii zote, wa jinsia zote, wa rangi zote, wa hali zote za maisha, matajiri na masikini na Watanzania wa circumstances zote.

Mimi nikiwa mwandishi wa habari, nimeshuhudia chaguzi zetu zote za vyama vingi, zimekuwa zikiendeshwa kwa mtindo wa "Mutatis Mutandis"

Hivyo sasa tunapokwenda kwenye uchaguzi, naomba kutoa ombi maalum na angalizo muhimu kwa wahusika wakuu wa uchanguzi wa Serikali za Mitaa 2024 na Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2025, uendeshwe kwa kutumia kanuni ya Kilatini ya "ceteris paribus" na sio kutumia zile kanuni zetu za kawaida za "Mutatis Mutandis"!.

Nimesikia sauti, "voices from within" kuwa tukiendelea kufanya chaguzi zetu kwa Mutatis Mutandis, kuna janga fulani litatokea.

Wahusika wakuu wa uchanguzi huu, wakikubali uchaguzi wa serikali za mitaa wa 2024 na uchaguzi Mkuu ujao wa 2025 kuendeshea kwa ceteris paribus , taifa Letu litabarikiwa, na viongozi wetu wabarikiwa, na sisi wananchi wa kawaida pia, tutabarikiwa na kupata neena na mafanikio makubwa, na nchi yetu kupata ustawi mkubwa wa kisiasa, kiuchumi na kijamii, lakini tukiendelea kutumia ule mtindo wetu wa mutatis mutandis, taifa tutalaaniwa na viongozi wetu watalaaniwa na kuadhibiwa!, and you never know ni adhabu gani viongozi wetu wakuu wataadhibiwa!.

Mungu Mbariki Rais Samia na watendaji wake wapate uwezo, watumie "Ceteris Peribus" kwa vyama vyote na sio kuendeleza "Mutatis Mutandis"

Mungu ibariki Tanzania.

NB. Sijaweka ufafanuzi wa maneno "Ceteris Peribus" na "Mutatis Mutandis" sio kwa bahati mbaya, nimefanya hivi kwa makusudi mazima, kwa sababu ujumbe huu ni ujumbe maalum na mahsus kwa watu maalum na mahsus ambao mimi nawajua huwa wanatembelea sana jf, kwa vile watu hao, wanayajua maneno hayo. Wengine wasio husika hayawahusu, hivyo sikufafanua ili ujumbe huu uwafikie walengwa tuu.

Hata Mungu alipotaka kumfikishia ujumbe maalum mfalme Belshaza, alimtumia kiganja cha mkono kikaandika kwenye ukuta wake, "Mene Mene Tekeli na Peresi", tukiendelea kufanya chaguzi zetu kwa Mutatis Mutandis badala ya kutumia
Ceteris Paribus, then kuna siku Mene Mene Takeli na Peresi itakuja kuishukia Tanzania na kumshukia kiongozi wetu!.

Nawatakia Weekend Njema,

Paskali.
Mene Mene Tekeli na Peresi imeisha wahi kutushukia, tusikaribishe tena Mene Mene!.

Hivyo sasa nauliza na kushauri, mnaonaje kama uchaguzi wa Serikali za Mtaa Ufanywe Siku Moja na Uchaguzi Mkuu usimamiwe na Tume Huru ya Uchaguzi?

Naombeni tusilete excuse ya chaguzi 4 kufanyika siku moja, yaani uchaguzi wa Rais, Mbunge, Diwani, Mwenyekiti wa Serikali za Mitaa, wenzetu Zanzibar wanafanya chaguzi 5 kwa siku moja, Rais wa JMT, Rais wa Zanzibar, Mbunge wa Bunge la JMT, Mwakilishi wa BLW, na Shehia!.

Hili likifanyika, Rais Samia na taifa Letu litabarikiwa, na viongozi wetu wabarikiwa, na sisi wananchi wa kawaida pia, tutabarikiwa na kupata neena na mafanikio makubwa, na nchi yetu kupata ustawi mkubwa wa kisiasa, kiuchumi na kijamii.

Mungu Ibariki Tanzania.

Paskali
 
Hivi binadam wengi awawezi kuishi kabisa kwenye wanacho kiamini. Kaka mleta post ulikua mmoja ya wale walioshangiria makosa yaliyofanyika kwenye uchaguzi wa serikali za mitaa wakati wa utawala wa JPM. Tupo tuliopinga hiyo tabia na hayo matuimizi mabaya ya dola na katiba ingawa wewe na genge lako mlikua mstari wa mbele kusema kinachofanywa ni sahihi kabisa. Nataka kusema nini hapa? Wewe na genge lako una moral authority na legitimacy kusema wala kushauri hilo ingawa una legitimacy with due legal loophole.
Kuchanganya au kufanya uchaguzi wa serikali za mitaa na uchaguzi mkuu kwasasa aiwezekani na inabiti isiwezekane maana italeta usumbufu amabo mwisho wa siku unaweza kutuelekeza kwenye machafuko nk. Pia kufanya hivyo ni kujenga mazingira ya kusababisha vurugu na kuharibu uchaguzi wote.
 
Chaguzi zote CCM huishia kuiba kura, sioni sababu hata kwanini hizo chaguzi zenyewe huwa zinafanyika, wanachezea pesa za walipa kodi bure, na kupotezeana muda tu kwa maigizo ya kijinga.
 
Nakumbuka kuna mikoa CCM iliishinda Mkoa mzima bila chàama kingine kupata hata mtaa/kijiji chochote. Huenda wakihamia Tu kutangaza. Wakurugebzi ni walewalenaVEO/MEO ni walewale ambao Hadi SASA nafsi zao zipo kwenye masononeko makubwa sana kuhusiana na chaguzi zile.

Sent from my SM-G977B using JamiiForums mobile app
 
Honestly i was hoping by this time sheria ya uchaguzi ingekuwa imerekebishwa, uchaguzi wa serikali za mitaa usimamiwe na NEC na ufanyike kwa wakati mmoja na uchaguzi mkuu.

Apparently, SSH is all talk no action. Very sad.
 
Hivi binadam wengi awawezi kuishi kabisa kwenye wanacho kiamini. Kaka mleta post ulikua mmoja ya wale walioshangiria makosa yaliyofanyika kwenye uchaguzi wa serikali za mitaa wakati wa utawala wa JPM. Tupo tuliopinga hiyo tabia na hayo matuimizi mabaya ya dola na katiba ingawa wewe na genge lako mlikua mstari wa mbele kusema kinachofanywa ni sahihi kabisa. Nataka kusema nini hapa? Wewe na genge lako una moral authority na legitimacy kusema wala kushauri hilo
Mkuu Bishweko , asante kwa mchango wako, ila kuna watu ukishawajua ni makada wa kile chama chetu pekee, unadhani wote ni wa kereketwa au wafurukutwa, wengine ni makada wazalendo, wanasimama na haki bin haki, kada mimi ni mmoja wapo, angalia mada zangu hizi kuhusu uchaguzi wa serikali za mitaa 2019.
P
 
Back
Top Bottom