Poor Brain
JF-Expert Member
- Jul 5, 2019
- 28,838
- 58,521
JICHO LANGU GEREZANI
“ Simulizi hii ni Ya kweli kabisa hamna mahali nitaongeza chumvi ili kunogesha stori kila ninachokiandika hapa MUNGU akawe shahidi na aniadhibu kama nitaandika UONGO au kusema kitu ambaoho si cha kweli ili kuharibu sifa ya Nchi/mtu/taasisi.
Naandika haya yawe kama somo kwa wale ambao walikua wamewaweka watu magereza hadi leo hii anaposoma haya,naandika haya kama somo kwa yeyote anaetaka mpeleka mtu magereza ili ajue anampeleka mtu kule anaenda kufanya nini na je Atakapotoka atakua ni mtu wa aina GANI.
NOTE: sina ujuzi wa uandishi jamani so ninapoandika mjaribu tu kunielewa naweza nikaanza A nikaja Z nikarudi J nikaenda K ila nitaandika kila kitu ktk njia inayoeleweka sitoacha mtu na maswali ktk kita nitakachogusia.
Nakumbuka nilikua tayari nina kesi Ya kutishia kuua kwa Maneno na kujeruhi,wakati huo nikiwa nasoma Chuo morogoro akini wazazi wangu WALITENGANA so mama akawa moro baba yupo Arusha. . .siku moja nikiwa Nimetokea zangu Moro chuo nakuja arusha kwa mshua (kumbe natafutwa hapo bila mimi kujua) basi nikafika arusha mJini kama ilivgo kawaida yangu huwa nikifika Arusha siendi direct kwa BABA nakaa zangu nakula bata hela zikikaribia kuisha ndo naenda kwa BABA.
NEXT .....................
Vishu Mtata