Omary Jumanne Salum, mkurugenzi mpya wa SIDO

Mkuu tupe walau wasifu wake kidogo, alikua anafanya wapi amewahi kushika nyadhifa gani, elimu yake n.k. SIDO ni shirika muhimu sana kwa uchumi wa Tanzania lakini limeshindwa kufanya majukumu yake kama matakwa sheria ya kuanzisha shirika yalivyoanisha. So tungependa kufahamu umakini wa mdau aliyepewa shirika hilo.
TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete amemteua Eng. Omari Jumanne Bakari kuwa Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Maendeleo ya Viwanda Vidogovidogo (SIDO).

Kulingana na Katibu Mkuu Kiongozi (KMK) Balozi Ombeni Y. Sefue, uteuzi huo umeanza Desemba 04, mwaka huu, 2013. Eng.

Omari Jumanne Bakari ni Mtafiti Mwandamizi katika Tume ya Sayansi na Teknolojia, Dar es Salaam.

Eng. Omari Jumanne Bakari ni Mtanzania mwenye elimu, weledi na uzoefu ambao umemfanya Mheshimiwa Rais aamini kuwa atakapoongoza SIDO, atasaidia kukidhi matarajio ya taifa kwa kueneza ujasiriamali, uwekezaji,uzalishaji na kutoa nafasi za ajira katika ngazi ya viwanda vidogo na vya kati kama msingi imara wa uchumi wa Tanzania, ikiwemo kwa kuingiza sayansi, teknolojia na ubunifu katika viwanda vidogo vidogo.

“Mwisho”

Imetolewa na:

Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais,
Ikulu.
DAR ES SALAAM.

16 Desemba, 2013
 
Someni kwa bidii sana ili muache kulalamika,elimu ya madrasat haiwezi kukuvusha hata mpaka wa burundi, Alafu msipende sana upendeleo na misaada! Hata oic mnayoitaka ni kwa ajili ya misaada si lingine... Jifunzeni kujitegemea.

Non sense!
 
Udini dot com
tutazoea tu na watu wa upande wa pili kuongoza. sisi tumeongoza tangia uhuru wa nchi hii tumelifanyia nini taifa zaidi ya kuiba tu? waachwe tu waongoze na wao ili tuone upande wa pili kama kuna maendeleo ya maana.
 
Rais Jakaya Kikwete amenteua Omary Jumanne Salum kuwa mkurugenzi mpya wa SIDO.

Tahadhari:
Ameteua kwa kuzingatia uwezo wa mteuliwa na si sababu nyingine.

Kwanini umejihami mapema? Sisi tuliopo kwenye hiyo system ya Kikwete tunajua kuna mkakati wa kuwainua jamaa zetu kimadaraka.Wapo wengi walioteuliwa kwenye nafasi kwa mfano za ukurugenzi wa wilaya hawana sifa na baadhi yao hawakuwahi hata kushikilia nafasi yoyote kubwa lakini ghafla wamepewa vyeo hivyo.Wala usije ukajihami kwani tunajua hili na wala halitupi shida.Muda utasema ukifika.
 
TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete amemteua Eng. Omari Jumanne Bakari kuwa Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Maendeleo ya Viwanda Vidogovidogo (SIDO).

Kulingana na Katibu Mkuu Kiongozi (KMK) Balozi Ombeni Y. Sefue, uteuzi huo umeanza Desemba 04, mwaka huu, 2013. Eng.

Omari Jumanne Bakari ni Mtafiti Mwandamizi katika Tume ya Sayansi na Teknolojia, Dar es Salaam.

Eng. Omari Jumanne Bakari ni Mtanzania mwenye elimu, weledi na uzoefu ambao umemfanya Mheshimiwa Rais aamini kuwa atakapoongoza SIDO, atasaidia kukidhi matarajio ya taifa kwa kueneza ujasiriamali, uwekezaji,uzalishaji na kutoa nafasi za ajira katika ngazi ya viwanda vidogo na vya kati kama msingi imara wa uchumi wa Tanzania, ikiwemo kwa kuingiza sayansi, teknolojia na ubunifu katika viwanda vidogo vidogo.

"Mwisho"

Imetolewa na:

Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais,
Ikulu.
DAR ES SALAAM.

16 Desemba, 2013

Hapo blue sidhani kama kulikuwa na haja ya kuandika hivyo.Ni kama kinga mvua fulani ili watu tuamini hilo na si kuhoji hoja ya upande wa pili kwanini umemteua.Jazaneni tu lakini muda utafika.
 
Rais Jakaya Kikwete amenteua Omary Jumanne Salum kuwa mkurugenzi mpya wa SIDO.

Tahadhari:
Ameteua kwa kuzingatia uwezo wa mteuliwa na si sababu nyingine.
Kama zipi ambazo unahisi watu wangeziangalia.
 
Kwa hali ilivyo hapa nchini na maendeleo tunayotarajia ili kufikia dira ya maendeleo 2025, ni matumaini yangu uteuzi huu umezingatia mtu mwenye sifa (irregardless ya dini yake, mahali alipotoka, etc). SIDO inahitaji mtu mwenye uelewa,weledi na mapenzi na viwanda vidogo vidogo. Kama nchi, na kama ilivyokuwa azimio la TANU kuhusu viwanda vidogo vidogo, bila shaka yote yamezingatiwa. Tujue wazi kuwa hakuna mzungu au taifa lolote la magharibi linapenda nchi yeyote ya Kiafrika ifanye mageuzi katika sekta ya viwanda. Mimi simjui Omary, lakini najua katika usahili wa nani achukue nafasi ya Laizer kuna watu waliokuwa na uwezo mkubwa kieleimu na passion kwenye sekta ya viwanda vidogo vidogo. Tungoje tuone maana tunachohitaji ni maendeleo na si urafiki au udugu kwenye maswala mazito ya kitaifa.
 
Kwa hali ilivyo hapa nchini na maendeleo tunayotarajia ili kufikia dira ya maendeleo 2025, ni matumaini yangu uteuzi huu umezingatia mtu mwenye sifa (irregardless ya dini yake, mahali alipotoka, etc). SIDO inahitaji mtu mwenye uelewa,weledi na mapenzi na viwanda vidogo vidogo. Kama nchi, na kama ilivyokuwa azimio la TANU kuhusu viwanda vidogo vidogo, bila shaka yote yamezingatiwa. Tujue wazi kuwa hakuna mzungu au taifa lolote la magharibi linapenda nchi yeyote ya Kiafrika ifanye mageuzi katika sekta ya viwanda. Mimi simjui Omary, lakini najua katika usahili wa nani achukue nafasi ya Laizer kuna watu waliokuwa na uwezo mkubwa kieleimu na passion kwenye sekta ya viwanda vidogo vidogo. Tungoje tuone maana tunachohitaji ni maendeleo na si urafiki au udugu kwenye maswala mazito ya kitaifa.
Baba Tunde, afadhali umekiri kwamba humjui Mhandisi Omari Bakari. Tunaomjua tunajua kwamba hana weledi wala uwezo wa kuongoza SIDO. Pia wapo waliofanya naye kazi pale COSTECH wamo humu natumaini watajitokeza na kuongea bila woga wala upendeleo. Wenye mamlaka ya uteuzi waache kufanya majaribio na maendeleo ya nchi yetu. Leo tunajuta kwa teuzi nyingi tu ambazo hazikuzingatia weledi na uwezo wa wateuliwa. Tuko hapa tulipo kwa kujitakia sio kwa bahati mbaya. Nafasi za aina hiyo ni muhimu watu waombe na wachujwe ili kumpata kweli anayefaa sio kuacha mamlaka mapana na yasiyodhibitiwa na kanuni kwa mamlaka ya uteuzi.
 
Hiv hii hali ya kuanza ku uliza uliza dini ya mtu imetoka wapi hii? Kuzimu tuikemee au? Tena mara nyingi hao wanaoquestion udini ndo hata makanisani na misikitini kwenda ni kwa nadra, wamebaki uislam juma na ukristo john bhaasi! Hakuna cha zaid.
Juz ameteuliwa mkurugenz mkuu wa tanesco eng yule mlokole,waislaam wakakaa kimnya ,leo hii kachagulia eng musislaam wakristo mayowe !! He kwa hyo ina maana akichaguliwa mkristo ndo kwa uwezo ,muislam kabebwa??. Kwa nini wasipewe muda wa kuonesha ujembe wao ndo tujue kama alibebwa na udini au lah?.
Ni ujinga sana,na upumbavu kuwa na mijadala kama hii ktk forum hii inayoitwa ya magreat thinker. Na kama mathink tank wa TZ ndo wapo hivi bhaasi tena ,ndo maana nchi ipo nyuma na itaendelea kuwa nyuma kama hautaamua kubadilika. Yes wewe hapo!.
 
Baba Tunde, afadhali umekiri kwamba humjui Mhandisi Omari Bakari. Tunaomjua tunajua kwamba hana weledi wala uwezo wa kuongoza SIDO. Pia wapo waliofanya naye kazi pale COSTECH wamo humu natumaini watajitokeza na kuongea bila woga wala upendeleo. Wenye mamlaka ya uteuzi waache kufanya majaribio na maendeleo ya nchi yetu. Leo tunajuta kwa teuzi nyingi tu ambazo hazikuzingatia weledi na uwezo wa wateuliwa. Tuko hapa tulipo kwa kujitakia sio kwa bahati mbaya. Nafasi za aina hiyo ni muhimu watu waombe na wachujwe ili kumpata kweli anayefaa sio kuacha mamlaka mapana na yasiyodhibitiwa na kanuni kwa mamlaka ya uteuzi.
Umenena kweli na ndio imekuwa wasi wasi wangu juu ya uwezo wa mtu aliyepewa nafasi kubwa kama hii ya kuongoza SIDO. Kama ni mtu aliyepewa nafasi hiyo kwa lobbying au kwa upendeleo bila kujali sifa, basi SIDO imefikia mwisho. Wachina, Wahindi na Wazungu wataizika kabisa. We have a long way to go. Ninachojua raisi huwa anapelekewa majina matatu ili achague moja. Kwenye process ya usahili pale wizara ya viwanda kulikuwa na ujanja ujanja kwa kuengua baadhi ya watu waliokuwa na sifa za kweli na nashangaa kama huyu ambaye unasema hana uwezo ndio kawa mkurugenzi.
 
Back
Top Bottom