OMARI OMARI afariki dunia

OMARI OMARI afariki dunia

Viumbe hai wafananao (ndege, wadudu, wanyama, na binadamu) hutembea pamoja na hufanana!!! Aghalabu, kukuta njiwa anatembea na siafu!! R.I. P Omari. Mwenye mali ametwaa na jina lake libarikiwe
 
JK ni Rais wa misiba ya Wasanii.

Anapenda kwenda kwenye majanga kama haya lakini kwenye matatizo mfano ya kuchomwa kwa makanisa na uharibufu wa mali, kujeruhiwa na mauaji ya watumishi wa Kanisa, hapo JK yupo kimya kabisa, na ikizingatiwa ni Waumini wenzie wanaotenda mambo hayo.

Ushauri kwa JK abadilke asifikiri kushiriki misiba ya wasanii ni kujidanganya kwa kujiweka akribu na vijana akijua kuwa atapendwa na vijana.

HATUDANGANYIIIIIIII.

Akitaka tumuelewe ashughulikie matatizo yanayogusa vijana mfano Ajira kwa vijana, vitendo vya unyanyasaji vya askari wa jiji na manispaa kuhusu Wamachinga, na kudhibiti mfumuko wa bei nchini.

Labda labda tutamuelewa!!!!!!!!!!!!!!!



MIZAMBWA
INANIUMA SANA!!!!!

Kumbukumbu zinaonyesha hata kwenye msiba wa mwanasiasa(sio msanii) Rejia Mtemanyenje alikwenda kule ifakara,nadhani labda ni mtu wa watu tu sio wasanii peke yao,ni hulka tu ya mtu,mfano slaa yeye hana muda wala hulka ya kuhudhuria hudhuria maziko,amebanwa na shughuli nyingi za chama!
 
hv mbona vijana tunakosa adabu kwa mheshimiwa,mbona kejeli, lugha za matusi na dharau au matusi mnayoyajua ninyi ni ya nguoni tu! angekuwa mzazi wako ungeandika hayo uliyoyaandika! heshima waungwana.
 
Jk hakwenda kumjulia hali yule padri wa znz?
Jk hakwenda mbagala kwenyenuchomaji wa makanisa?
Sometimes tuwe tunafikiria vya kuongea wakuu tutakua lini?

Asante sana Mkuu;

Je, ni hatua gani amechukua yeye pamoja na serikali yake katika kudhibiti vitendo hivi, ambavyo vinatia hofu na kuharibu mali za Makanisa. yaani utadhani kama hakuna vyombo vya Dola!!!!!!!!

Kama ni kwenda kumuona Padri au kutembelea makanisa Mbagala hata mimi kote huko nilienda lakini sina la kufanya katika kudhibiti vitendo hivi.

Hivyo kwenda na kutembelea si dawa, kinachotakiwa ni kudhibiti, tena Serikali haionyeshi kuguswa na vitendo hivi hata kidogo na ndio maana wamekaa kimya nawahalifu wanaendelea.

Mwaka uliopita ni mwaka wa kukumbukwa kwa Mapadri na Kanisa nchini kwani ni jumla ya mapadri watatu wamepigwa, wamejeruhiwa.

Je, ni jambo la kuchekeachekea hili??????

Ingelikuwa ni Misikiti imechomwa na kuharibiwa mali za Misikitini ambapo Wakristo wamehusika. Hivi Tungepumua kweli hapa Tanzania???

Sometimes fikiria kabla ya kuongea. mkuu tutakua lini??




MIZAMBWA
INANIUMA SANA!!!
 
hv mbona vijana tunakosa adabu kwa mheshimiwa,mbona kejeli, lugha za matusi na dharau au matusi mnayoyajua ninyi ni ya nguoni tu! angekuwa mzazi wako ungeandika hayo uliyoyaandika! heshima waungwana.

Kwa nini umebadilisha ID???

Tumia ile ile ya zamani, unaogopa nini??
 
Chonde chonde tuache masikhara na kifo,sisi sote waja mbele ya Mwenyezi Mungu,leo ni Omar kesho ni Bishanga,RIP Omar.
 
JK ni Rais wa misiba ya Wasanii.

Anapenda kwenda kwenye majanga kama haya lakini kwenye matatizo mfano ya kuchomwa kwa makanisa na uharibufu wa mali, kujeruhiwa na mauaji ya watumishi wa Kanisa, hapo JK yupo kimya kabisa, na ikizingatiwa ni Waumini wenzie wanaotenda mambo hayo.

Ushauri kwa JK abadilke asifikiri kushiriki misiba ya wasanii ni kujidanganya kwa kujiweka akribu na vijana akijua kuwa atapendwa na vijana.

MIZAMBWA
INANIUMA SANA!!!!!
Mmmh, mnyonge mnyongeni, haki yake mpeni. Yalipochomwa makanisa Mbagala alienda kutembelea makanisa yote yaliyochomwa na ndipo akatoa amri ya akina Ponda kukamatwa. Tafuta lingine mkuu. R.I.P Omar. Asante kwa ujumbe uliotuachia - kupata majaliwa.
 
Last edited by a moderator:
Moja ya Maneno yake katika Wimbo wa KUPATA MAJALIWA

"..kwa Mungu hauna hisa ila umetunukiwa, nduguyo kuninyanyasa ukae ukielewa hautozikwa na pesa au gari ulilonunua, hizo nyumba za kisasa wapo watakaochukua.."

R. I. P OMARY OMARY
 
atakuwa yule aloimba "kazi yangu ya dukani inaniweka matatani". r.i.p omar. mia


Hapana mkuu!
Alioimba huo wimbo ni Dogo mfaume.

Huyo marehemu ameimba wimbo ambao una kibwagizo kinachosema ''Ndevu amepewa Mbuzi lakini Ngombe kanyimwa''
 
Aliyeimba kazi yangu ya dukani ni Dogo Mfaume, nyimbo zake ni maharufu ktk miaka ya 90 kama Kinyago msela (shamba langu), Baba Asha (Sungusungu hakulinda), Hereni, Upo wapi mama, na baadaye kuibuka tena miaka 2000 kwa kibao kupata ni Majaliwa.


Mkuu walioimba ''upo wapi Mama'' ni kundi la Hisani ama Gari kubwa.
nyimbo zao nyingine ni Mola, Ally Mwinyi, Dunia, sikuoni, wala si mkweli, wasiopenda hisani na nilipoamua...
 
atakuwa yule aloimba "kazi yangu ya dukani inaniweka matatani". r.i.p omar. mia[/QU mia mwenyewe mana toka umeijua hyo mia imekuwa tabu.we nawe mzaramo wa wapi hufahamu hata waimbaji wenu,huyo wa kaz ya dukan anaitwa dogo mfaume,alokufa anaitwa omari omari.
 
Kwa sisi wapenzi wa mchiriku miaka hiyo omary omary alikua zaidi ya diamond kwa kizazi cha dotcom. RIP omary2
 
yeah nikweli mkuu. kaimba ng'ombe amekosa ndevu lakini mbuzi kapewa, usinione mnyonge kupata ni majaliwa. Gobore kathibitisha kifo chake. mazishi yatafanyika leo pale kwa baba yake mikoroshini maeneo ya mwembe yanga temeke. ukifika pale kisumu bar ulizia tu utaelekezwa coz pale mwembe yanga ndo kijiwe chake cha nyumbani. R.I.P. Mia

haaa unamjua utadhan ndo ulimzaa
 
Aliyeimba kazi yangu ya dukani ni Dogo Mfaume, nyimbo zake ni maharufu ktk miaka ya 90 kama Kinyago msela (shamba langu), Baba Asha (Sungusungu hakulinda), Hereni, Upo wapi mama, na baadaye kuibuka tena miaka 2000 kwa kibao kupata ni Majaliwa.

ok! thanx. mia
 
Back
Top Bottom