Mratibu wa Mtandao wa Watetezi wa Haki za Binadamu (THRDC), Wakili Onesmo Olengurumwa amesema.
Pamoja na serikali inayoongozwa na Rais Dkt. Samia Suluhu kupongezwa na wadau mbali mbali wa haki za binadamu katika maeneo mengi ikiwemo kutoa uhuru wa kujieleza na kutoa maoni uhuru, sakata la kukamatwa wakosoaji wakubwa wa mkataba wa bandari Balozi Mstaafu Dkt. Willbroad Slaa, Wakili Boniface Mwabukusi na Mdude Nyagali kunaweza kutia dosari mazuri hayo pamoja na kuchafua taswira ya Rais Samia kimataifa endapo akikubali watuhumiwa hao kuwa na kesi ya uhaini.
Amesema, itakuwa ni historia katika awamu hii ya sita na pia itakuwa ni kwa mara ya kwanza baada ya miaka mingi kupata watu wanashtakiwa kwa makosa ya uhaini.
"Kwa mujibu wa Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kila mtu anao uhuru wa kutoa maoni na kueleza fikra zake, katiba imetulinda, Wakili Mwabukusi, Mdude na Balozi Dkt. Slaa walikuwa wanafanya kwa mujibu wa katiba na kama kuna mahali popote waliteleza kwa maneno ya hapa na pale isiwe ni sababu ya kuwafungulia kesi kubwa kama hii na kuwazuia wao na Watanzania wengine wasikosoe" alisema Wakili Olengurumwa na kuongeza
"Kuanza kuwakamata wote wanaopinga mkataba wa bandari kuanzia kwa Wakili Madeleka sasa Slaa na wenzake litatutia doa kama Taifa, tunawashauri viongozi wetu kabla ya kufika mbali katika hatua hii ,hawa watu wasifunguliwe jalada la uhaini.”
Pamoja na serikali inayoongozwa na Rais Dkt. Samia Suluhu kupongezwa na wadau mbali mbali wa haki za binadamu katika maeneo mengi ikiwemo kutoa uhuru wa kujieleza na kutoa maoni uhuru, sakata la kukamatwa wakosoaji wakubwa wa mkataba wa bandari Balozi Mstaafu Dkt. Willbroad Slaa, Wakili Boniface Mwabukusi na Mdude Nyagali kunaweza kutia dosari mazuri hayo pamoja na kuchafua taswira ya Rais Samia kimataifa endapo akikubali watuhumiwa hao kuwa na kesi ya uhaini.
Amesema, itakuwa ni historia katika awamu hii ya sita na pia itakuwa ni kwa mara ya kwanza baada ya miaka mingi kupata watu wanashtakiwa kwa makosa ya uhaini.
"Kwa mujibu wa Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kila mtu anao uhuru wa kutoa maoni na kueleza fikra zake, katiba imetulinda, Wakili Mwabukusi, Mdude na Balozi Dkt. Slaa walikuwa wanafanya kwa mujibu wa katiba na kama kuna mahali popote waliteleza kwa maneno ya hapa na pale isiwe ni sababu ya kuwafungulia kesi kubwa kama hii na kuwazuia wao na Watanzania wengine wasikosoe" alisema Wakili Olengurumwa na kuongeza
"Kuanza kuwakamata wote wanaopinga mkataba wa bandari kuanzia kwa Wakili Madeleka sasa Slaa na wenzake litatutia doa kama Taifa, tunawashauri viongozi wetu kabla ya kufika mbali katika hatua hii ,hawa watu wasifunguliwe jalada la uhaini.”