Olengurumwa: Uhaini waliopewa akina Dkt. Slaa unatia doa taifa na taswira ya Rais

Wewe ndiyo kilaza ,rudia kusoma tena doc uliyoweka hapa ,Dr Slaa/Mwabukusi/Mdude hawajakidhi vigezo vya kushitakiwa kwa uhaini.....Tatizo mnalazimisha kesi sizizo na kichwa wala miguu na mnaenda kudondokea pua ,Kibatala anakuja Mbeya huko ,yaani hii case hata Mtu asiyejua sheria anawadondosha mahakamani.
Wewe kwa ufahamu wako ili mtu ashitakiwe kwa kesi ya Uhaini afanye mambo gani ili uwe uhaini?
 
Wewe kwa ufahamu wako ili mtu ashitakiwe kwa kesi ya Uhaini afanye mambo gani ili uwe uhaini?

Mbona mifano ipo mingi sana humu JF ya watu waliofanya uhaini kweli,Katiba imesema wazi uhaini ni nini.

Soma kuhusu Nyerere kutaka kupinduliwa ,utajua maana halisi ya uhaini halafu linganisha na "Uhaini" wa Dr Slaa,Mdude na mwabukusi.
 
nchi haiwezi kutulia kwa mtindo huo. Hakuna anayetaka kuipindua serikali. ambacho hakitakiwi ni mkataba mbovu wa bandari. kufunga watu sio suluhisho. inatujengea chuki zaidi baina yetu, tunajichafua kimataifa. wanaomshauri Rais wanampoteza. majitu machumia tumbo ndio yanayoiharibu hii nchi.

Mkataba na DPW uvunjwe, watu waachiwe huru, maisha yaendelee! VINGINEVYO.
Mambo ya mkataba wa bandari yako Mahakama ya Rufaa. Hao wameshikwa kwa kauli zao za kuchochea maandamano ya kupindua nchi.
20230815_205708.jpg
 
Soma kesi ya Uhaini ya mwaka 1985. Kuna waliokuwa kwenye vyombo vya ulinzi na usalama na wasiokuwemo kwenye hivyo vyombo na hata serikalini ambao walikutwa na hatia.
Sasa unajipatia jibu wewe mwenyewe!
Kulikuwa mpaka makomandoo kina marehemu Mohamed Tamim na Yassin memba kaka yake na Mussa memba....

Sasa haya ya wakili mmojana Dk slaa mwanasiasa mstaafu mmoja na whistle-blower mmoja ndio uhaini?
 
nchi haiwezi kutulia kwa mtindo huo. Hakuna anayetaka kuipindua serikali. ambacho hakitakiwi ni mkataba mbovu wa bandari. kufunga watu sio suluhisho. inatujengea chuki zaidi baina yetu, tunajichafua kimataifa. wanaomshauri Rais wanampoteza. majitu machumia tumbo ndio yanayoiharibu hii nchi.

Mkataba na DPW uvunjwe, watu waachiwe huru, maisha yaendelee! VINGINEVYO.
Na hichi ndio kiini cha tatizo watu wameshakula hela za muarabu matumbo joto wapo tayari hata kuua ili mkataba upite
 
Waliowakama Dk Slaa, Mwabhukusi na Mdude ndio walioanza kuwatumia meseji za kutaka kuwaua kwa hiyo wakamataji ni majambazi dhidi ya binadamu (crime against person).
Watu watatu wanampindua nani kwa nyenzo gani?

Wamemchochea nani na akafanya kitendo gani dhidi ya yule anayedaiwa kutendewa kosa?

Mwanajeshi gani, usalama wa taifa gani au kiongozi mwandamizi wa serikali ambaye amekula njma na hao watu watatu kumpindua rais na nia hiyo ingetekelezwa na wapi?
 
Mratibu wa Mtandao wa Watetezi wa Haki za Binadamu (THRDC), Wakili Onesmo Olengurumwa amesema.

Pamoja na serikali inayoongozwa na Rais Dkt. Samia Suluhu kupongezwa na wadau mbali mbali wa haki za binadamu katika maeneo mengi ikiwemo kutoa uhuru wa kujieleza na kutoa maoni uhuru, sakata la kukamatwa wakosoaji wakubwa wa mkataba wa bandari Balozi Mstaafu Dkt. Willbroad Slaa, Wakili Boniface Mwabukusi na Mdude Nyagali kunaweza kutia dosari mazuri hayo pamoja na kuchafua taswira ya Rais Samia kimataifa endapo akikubali watuhumiwa hao kuwa na kesi ya uhaini.

Amesema, itakuwa ni historia katika awamu hii ya sita na pia itakuwa ni kwa mara ya kwanza baada ya miaka mingi kupata watu wanashtakiwa kwa makosa ya uhaini.

"Kwa mujibu wa Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kila mtu anao uhuru wa kutoa maoni na kueleza fikra zake, katiba imetulinda, Wakili Mwabukusi, Mdude na Balozi Dkt. Slaa walikuwa wanafanya kwa mujibu wa katiba na kama kuna mahali popote waliteleza kwa maneno ya hapa na pale isiwe ni sababu ya kuwafungulia kesi kubwa kama hii na kuwazuia wao na Watanzania wengine wasikosoe" alisema Wakili Olengurumwa na kuongeza

"Kuanza kuwakamata wote wanaopinga mkataba wa bandari kuanzia kwa Wakili Madeleka sasa Slaa na wenzake litatutia doa kama Taifa, tunawashauri viongozi wetu kabla ya kufika mbali katika hatua hii ,hawa watu wasifunguliwe jalada la uhaini.”

Kwann hamkulalamika wakat hao waliokamatwa walipokua wanatumia huo uhuru vibaya
Afu kukosoa bandari hakujawafanya wakamatwe acheni upotoshaji wote tumeyasikia maneno yao jukwaani .msilete siasa za chuki kwa kila jambo,hao wamepata waliostahil kwa matamshi yao ya kijinga ya kutishia usalama na kueka chuki wala c kauli za bandari
 
Ukicheka na nyani utavua mabua. Hawa kina Dr Slaa wameshindwa kutumia uhuru wa maoni ipasavyo. Wameshindwa kuuelewa uungwana wa Rais Samia wakadhani ni UDHAIFU.

Wacha wanyee ndoo na nchi itulie. Mwambieni Olengurumwa aache vyombo vifanye kazi. Kama ana utetezi aende Mahakamani

Ukweli mtupu mkuu.na wamefanya kusudi ili kumtoa rais kwenye reli aonekane ananyima uhuru
Ila hakuna uhuru usio na mipaka
 
nchi haiwezi kutulia kwa mtindo huo. Hakuna anayetaka kuipindua serikali. ambacho hakitakiwi ni mkataba mbovu wa bandari. kufunga watu sio suluhisho. inatujengea chuki zaidi baina yetu, tunajichafua kimataifa. wanaomshauri Rais wanampoteza. majitu machumia tumbo ndio yanayoiharibu hii nchi.

Mkataba na DPW uvunjwe, watu waachiwe huru, maisha yaendelee! VINGINEVYO.

Utafanyaje vinginevo? Aya kawatoe au na ww endeleza walichoanza
 
Serikali inashangaza sana ,yaani unamshitaki mtu kwa makosa ya uhaini kisa ametamka kwenye Luninga au interview au kwenye whatsapp ,hivi walifatilia mapinduzi aliyofanya Mu7 wa UG au Desire Laurent Kabila? Kwani kuna nia ovu kwenye yale matamshi? Alipanga mikakati gani ,hivi watu watatu wanaweza kumpindua rais ikulu?
Eti mhaini anajitangaza
 
Kauli zenye kuhamasisha umma, kuandamana na kuyatwaa madaraka, pengine watu wanashindwa kuelewa, mapinduzi sio lazima silaha za moto au majeshi yatumike, umma unaweza kuchochewa na kauli za kichochezi na hatimaye serakali ikapinduliwa!

Kauli, kauli, kauli..

Wanaelewa ila wanaeka emotion mbele hapo ndio wanajikuta kutumika vibaya na wanasiasa
 
Serikali inashangaza sana ,yaani unamshitaki mtu kwa makosa ya uhaini kisa ametamka kwenye Luninga au interview au kwenye whatsapp ,hivi walifatilia mapinduzi aliyofanya Mu7 wa UG au Desire Laurent Kabila? Kwani kuna nia ovu kwenye yale matamshi? Alipanga mikakati gani ,hivi watu watatu wanaweza kumpindua rais ikulu?

Uelewa wako ukoje mkuu..kauli za mtu mmoja mwenye ushawishi zinaeza pindua serikali
Kama wakiachwa waendelee na izo kauli wazani nn kitatokea?
 
Mratibu wa Mtandao wa Watetezi wa Haki za Binadamu (THRDC), Wakili Onesmo Olengurumwa amesema.

Pamoja na serikali inayoongozwa na Rais Dkt. Samia Suluhu kupongezwa na wadau mbali mbali wa haki za binadamu katika maeneo mengi ikiwemo kutoa uhuru wa kujieleza na kutoa maoni uhuru, sakata la kukamatwa wakosoaji wakubwa wa mkataba wa bandari Balozi Mstaafu Dkt. Willbroad Slaa, Wakili Boniface Mwabukusi na Mdude Nyagali kunaweza kutia dosari mazuri hayo pamoja na kuchafua taswira ya Rais Samia kimataifa endapo akikubali watuhumiwa hao kuwa na kesi ya uhaini.

Amesema, itakuwa ni historia katika awamu hii ya sita na pia itakuwa ni kwa mara ya kwanza baada ya miaka mingi kupata watu wanashtakiwa kwa makosa ya uhaini.

"Kwa mujibu wa Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kila mtu anao uhuru wa kutoa maoni na kueleza fikra zake, katiba imetulinda, Wakili Mwabukusi, Mdude na Balozi Dkt. Slaa walikuwa wanafanya kwa mujibu wa katiba na kama kuna mahali popote waliteleza kwa maneno ya hapa na pale isiwe ni sababu ya kuwafungulia kesi kubwa kama hii na kuwazuia wao na Watanzania wengine wasikosoe" alisema Wakili Olengurumwa na kuongeza

"Kuanza kuwakamata wote wanaopinga mkataba wa bandari kuanzia kwa Wakili Madeleka sasa Slaa na wenzake litatutia doa kama Taifa, tunawashauri viongozi wetu kabla ya kufika mbali katika hatua hii ,hawa watu wasifunguliwe jalada la uhaini.”
huyo masai mchumia tumbo akae kimya, hao ni vibaraka wa maadui zetu ndivyo wanavyopata kula yao, hawana uzalendo zaidi ya matumbo yao.wapuuzwe hao washenzi
 
Wewe ndiyo kilaza ,rudia kusoma tena doc uliyoweka hapa ,Dr Slaa/Mwabukusi/Mdude hawajakidhi vigezo vya kushitakiwa kwa uhaini.....Tatizo mnalazimisha kesi sizizo na kichwa wala miguu na mnaenda kudondokea pua ,Kibatala anakuja Mbeya huko ,yaani hii case hata Mtu asiyejua sheria anawadondosha mahakamani.

Kwa kauli hii yaonesha hata mahakamn ujawai simama.usipojua sheria utaona mahakama inakuonea maana wew utaleta ushahidi wa hisia wenzako wanakuja na hoja na vifungu vya sheria
 
Back
Top Bottom