Mouth Beibe
New Member
- Jan 9, 2012
- 1
- 0
Kumekuwa na kijitabia kichafu tena cha siku nyingi kwa baadhi ya wanaume,kijitabia hiki ni cha kuwapa mimba mabinti na kuwakataa bila sababu za msingi,kwa mfano mtu mwingine anaweza kusema eti ana mchumba mwingine anaetaka kumuoa na siyo huyo mwenye ujauzito wake!!!!loooh hakuna neno linalouma kwetu wanawake kama hilo jamani, inaonyesha dhahiri hunithamini, hunipendi na wazi kabisa kuwa ulikuwa unanichezea...anyway malipo duniani,usipolipwa wewe basi utazaa mwanao na atafanyiwa hivyo,muwe wastaarabu jamani mkikutana na situation kama hii,majibu mengine yanaonyesha wazi kuwa ni jinsi gani huna busara na hekima wewe mwanaume usiye na hata tone la aibu, mimi ukinifanyia hivi naapa sitakusamehe daima na jua kumbuka na faham ya kuwa malipo ni hapa hapa duniani