Ole wako Tanzania, viongozi vijana ni wanafiki haswa Zitto: Posho alisema hivi...

Pro Zitto na wale Against endeleeni kuumana lakini mjue Posho ndiyo zimeshapanda hivyo!!
 
Binafsi nilikuwa namwona kama nuru miongoni mwa vijana viongozi wa kisiasa nchini ,ila tangu jana nimesema ntakuwa namsikiliza kwa masikio mawili na kumtizama kwa macho mawili , nitapima kauli zake kwa kina sana .
Hufai kuwa Mbunge kama kweli wewe ni Mbunge. Umeshindwa kuelewa hoja ya Zitto kuhusu utofauti wa posho na maslahi mengine kama mshahara? Zitto amesema hapo hapendi hilo neno posho kwa vile ni la kiujanja ujanja katika ulipaji kama ni malipo ya kiutumishi yawekwe hivyo maana yatakuwa wazi zaidi na yatahusisha vyombo vingi vya umma kujadili hivyo kuongeza uhalali wake sio hayo maposho ya kusinzia yanayojadiliwa gizani.
 
Hivi wewe ndiyo umejua kuwa kwamba zitto ni mnafiki????????!!!!!!!! Nakushangaa sana, Ulikuwa wapi muda wote!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!
 
Nashukuru umewaeleza wazi kuwav ni kweli jana ulisema kuwa hupingi suala la maslahi zaidi kwa wabunge , ila tatizo ni hayo masilahi kuitwa posho.

kwa hiyo unaeleza nini hapo kuwa ni sisi wabunge tuu ndio maisha yamepanda ?
Mhe Zitto kajitaja jina na ww jitaje basi maana hakuna mbunge anaitwa Mwongozowaspika,pili mimi nina wasiwasi utakuwa ni mwandishi wa Mtanzania au Jambo leo?Sasa kama alitoka nje na kuwaambia they think small kwa nini walikasirika?Kumbe hizo hela mnazitumia majimboni maana mnalalamika ya kuwa mmekimbia majimboni?Zitto ni mfuasi wa anachokiamini na sio mshabiki kama wewe!
 
Mwongozo wa spika,asante kwa taarifa,huo ni mkuki mwingine kwa makamanda wa ukweli.

Mungu tusaidie.

cjakuelewa!!!!!kwa mbali kama vile humpendi Zitto!!!hii nchi bwana afadhali nisingezaliwa,maana ni vituko tupu!!!!!!sasa nikueleje mama Padri!!msaada pls!
 
Naomba msiwe distracted na watu. Msimamo upo wazi kabisa. Hakuna posho za vikao (sio tu nyongeza bali mfumo mzima wa posho za vikao twataka ukome. Watu wameamua kutwist nilichosema bungeni jana. Narudia, lazima tupinge posho hizi. Kwa nini wabunge walipwe kwa kukaa kitako? Huyu anayesema mie mnafiki yeye aseme anaunga mkono posho za kukaa au la. Wapiganaji msiwe distracted.

itisha maandano ya amani ambayo utayaongoza kupinga mfumo mzima wa posho, ili tusimtishe jk maandamano yaanzie viwanja vya jangwani tuishie manzese atupokee katibu mkuu wa chama chako. sisi tutakuandalia bango la kubeba, kinyume chake you might become a victim of friendly fire to the front line.
 
naomba msiwe distracted na watu. Msimamo upo wazi kabisa. Hakuna posho za vikao (sio tu nyongeza bali mfumo mzima wa posho za vikao twataka ukome. Watu wameamua kutwist nilichosema bungeni jana. Narudia, lazima tupinge posho hizi. Kwa nini wabunge walipwe kwa kukaa kitako? Huyu anayesema mie mnafiki yeye aseme anaunga mkono posho za kukaa au la. Wapiganaji msiwe distracted.

tupo pamoja mkuu!!!!
 
kwasababu mimi nimeshachoka na huu upuzi wa Posho, basi kamateni huo mchanganuo wa Posho hapa.

Biya + ugali + usingizi = 80,000
Kujamba = 200,000
Nauli from kujamba to biya+ugali to mchetuko = 50,000
Total biya+ugali+mchetuko 330,000
 
Binafsi nilikuwa namwona kama nuru miongoni mwa vijana viongozi wa kisiasa nchini ,ila tangu jana nimesema ntakuwa namsikiliza kwa masikio mawili na kumtizama kwa macho mawili , nitapima kauli zake kwa kina sana .

Macho mawili na masikio mawili hayatoshi sababu ulikuwa navyo toka siku nyingi
unatakiwa umuangalie kwa macho na masikio zaidi ya mawili mawili.

Lakini naomba tuwekane sawa, ni mategemeo yangu kwamba umewaka hapa taarifa
za kweli bila kuongeza wala kupunguza, Sitegemei kesho na kesho kutwa habari hizi
zije kuonekana ni za kutunga na hivyo hazistahili kuaminiwa. utakuwa umeniumiza
sana.

Nakutakia kila kheri kwenye matumizi ya posho zako..
 
hii ni sehemu ya gazeti la Mwananchi leo,


JK abariki posho mpya za wabunge

Send to a friend
Monday, 30 January 2012 20:54
0diggsdigg



kikwete-akisaini.jpg
Rais Jakaya Mrisho Kikwete

KILA MMOJA KULIPWA 330,000 KWA SIKU, ZITTO, MAKAMBA, KIGWANGALA WASULUBISHWA KWA KUZIPINGA


Waandishi Wetu, Dodoma

WAZIRI Mkuu, Mizengo Pinda amesema tayari Rais Jakaya Kikwete amesaini kuidhinisha ongezeko la posho za vikao (sitting allowance) kwa wabunge kutoka Sh70,000 hadi Sh200,000 kwa siku. Kupitishwa kwa posho hizo ambazo ziliandikwa kwa mara ya kwanza na gazeti hili, kunafanya sasa mbunge kupokea Sh330,000 kwa siku; Sh200,000 zikiwa ni posho ya kikao, Sh80,000 posho ya kujikimu na Sh50,000 nauli.


Taarifa za uhakika kutoka ndani ya kikao cha utanguzi cha wabunge jana, zilidai kuwa baada ya Pinda kutoa taarifa hiyo, wabunge walishangilia huku Mbunge wa Kigoma Kaskazini (Chadema), Zitto Kabwe, akisimama na kudai kuwa taarifa alizonazo ni kwamba Rais Kikwete alikuwa hajasaini kuidhinisha posho hizo.


Hatua hiyo ilisababisha Mbunge wa Kondoa Kaskazini, Juma Nkamia (CCM), kusimama na kuhoji iwapo Zitto ni miongoni mwa wasemaji wa Rais kabla ya Pinda kusimama na kuthibitisha kusainiwa kwa posho hizo akisema siyo ajabu kwani hata watumishi wa Serikali wanalipwa kati ya Sh150,000 na Sh200,000. Hata hivyo, Zitto alitetea msimamo wake kwamba alitarajia baada ya kusainiwa kwa posho hizo na Rais, angepewa masharti mapya ya kazi za ubunge.


Katika kikao hicho baadhi ya wabunge wanadaiwa kuwashambulia Zitto, Mbunge wa Bumbuli (CCM), January Makamba na Mbunge wa Nzega (CCM), Dk Khamis Kigwangwala kwamba wamekuwa mstari wa mbele kupinga posho hizo hadharani. Spika wa Bunge, Anne Makinda ambaye anadaiwa kwamba aliungana na Pinda kuthibitisha kwamba Rais Kikwete ameidhinisha posho hizo mpya, pia aliwashambulia wabunge wanaozipinga akisema kwamba wanafuta umaarufu wa kisiasa.



“Wanachotafuta ni umaarufu wa kisiasa tu, mimi ninavyojua umaarufu wa kisiasa unakuja kwa kufanya kazi za kibunge za wananchi lakini siyo kupinga posho,” chanzo chetu cha habari kilimnukuu Makinda.



Mbunge wa Gando (CUF), Khalifa Suleiman Khalifa anadaiwa kwamba alitumia mafumbo kuwashambulia wabunge hao ambao wamejitokeza kupinga nyongeza hiyo ya posho. Kauli hiyo inadaiwa kuungwa mkono na Mbunge wa Sikonge (CCM), Said Nkumba ambaye alidai kuwa hawezi kumsemea Zitto kwa sababu ni kawaida yake kupinga, lakini akaelekeza shutuma zake kwa Makamba kwamba ameanza kupinga baada ya kugharamiwa na CCM. “Januari anapinga posho hizo kutokana na CCM kumpa gari, nyumba na analipwa na chama,” kilisema chanzo chetu kikimkariri Nkumba.



Pia, Mbunge wa Kilindi, Beatrice Shelukindo (CCM), anadaiwa kumshambulia Zitto kuwa lazima apinge posho hizo kwa sababu, anapewa fedha na wafadhili kutoka nchi za nje. “Shelukindo anasema amefanya ziara nje na kuhakikisha kuna wahisani wanamfadhili Zitto kwa hiyo ana haki ya kupinga posho hizo,” chanzo chetu hicho kilimkariri Shelukindo.


Hata hivyo, inadaiwa kuwa baada ya mashambulizi hayo, Dk Kigwangwala alisimama kutetea msimamo wake kwamba ongezeko hilo halina ‘mashiko’ na haliwezi kuelezwa mbele ya umma likaeleweka, lakini alizomewa na wabunge wengi huku wakimtaka kukaa chini.



Hatua hiyo ilisababisha Zitto kusimama na kueleza kuwa tatizo la wabunge kwamba wana fikra finyu, kauli ambayo alitakiwa na wenzake kuwaomba radhi kuwa amewatukana. “Zitto ametumia Kiingereza kuwa tatizo la wabunge ‘we think small’, Shelukindo na (John) Komba wakaja juu wakitaka kuwaomba radhi kwa kuwatukana,” chanzo chetu kilieleza. Zitto anadaiwa kusema wabunge walitakiwa kujenga hoja ya kuongeza fedha za mafuta ya gari wanayolipwa hivi sasa Sh2.5 milioni kwa mwezi, kutokana na kupanda kwa nishati hiyo, lakini siyo posho



Wewe ni mpumbavu kabisa!!!!! wote tumesoma hilo gazeti so kulikuwa hakuna haja ya ku-quote hilo gazeti. Cha msingi ni wewe kuuambia umma wa watanzania ni nini msimamo wako! Yaani wewe kama kweli ni mbunge basi ndio wale wanaosinzia bungeni kisha mnaamka na kusema.........."hiyo imepita mh. spika" hata kama haujacikia huo muswada. Wewe ni mjinga sana............unakera tu watu humu ndani, ni heri ungekaa kimya au ukakojoe ukalale kama ci kucinzia bungeni.

Tueleze nini MSIMAMO wako kat hilo swala............kenge we.
 
nafikiri alikuwa na nia kuwa malipo wanayopata wabunge yabakie kama MSHAHARA NA SI VINGINEVYO
 
Nimesoma hiyo habari ktk gazeti la Mwananchi nimeelewa hoja ya Zito. Mimi naona mwongozowaspika ana chuki kwa Zito ama uelewa wake na uchambuzi wake ni wa chini sana. Hii ni aibu kama watunga sheria wetu ni wachovu kiasi hiki.
 
Hivi unajua kuwa Mbunge analipwa shilingi milioni 2.5 kwa ajili ya mafuta kwa mwezi na maana yake ni kuwa kila siku anapewa shilingi 83,333 sawa na lita 37.87 kwa bei ya shilingi 2,200 kwa lita , hata siku ambazo tunakaa Dodoma?

Kuna haja gani ya Mbunge wa Viti maalum kupewa hizo fedha wakati hana hata jimbo la kutembelea? Kuna haja gani wabunge wa majimbo ya mjini kupewa hizo fedha kila mwezi? kwanini pasiwe na ratiba kuwa kwa wakati wote wa vikao vya kamati na vile vya bunge hawatalipwa mafuta? Kwanini Zitto anataka kusema kuwa waseme wanahitaji fedha kwa ajili ya mafuta?

Naomba kuishia hapo , ntarejea baadae kidogo.

nadhani unajitafutia matusi ya nguoni. yaani unakuja kulalamika hapa na huoni aibu. umefanya nini wewe.. nadhani unastahili kupigwa kibao cha usoni!!
 
msimamo wangu upo hapo juu kwani nimesema wengine kutokana na sababu mbalimbali hatuwezi kusema hadharani , ila tunawaunga mkono wenye uwezo wa kusema .

Mimi hata kama hakutakuwa na posho nina uwezo wa kuendelea kuishi kutokana na pension yangu ni nzuri tuu kwa wastani wa maisha ya kitanzania .



Unajitia aibu wewe binafsi kwa kuonyesha wazi kwamba huko kwa maslahi binafsi na chama chako na wala sio kwa maslahi ya nchi na wananchi. Nilitegemea kiongozi mwandamizi kama wewe (kama unavyojitambulisha) kuwa mstari wa mbele katika kutetea kile unachoamini kwa uwazi na ukweli bila kujali matokeo yake. Ni aibu na fedheha kubwa sana kwa nchi kwamba umeweza kukaaa madarakani kwa kipindi chote hicho huku ukitimiza matakwa binafsi kwa malipo makubwa kutoka fedha za walipa kodi. Sitashangaa kwamba wewe ni mmoja kati ya wabunge wengi sana huko ambao mmekaa miaka kibao bila kutoa mchango wowote wa maana bungeni na kwenye majimbo yenu, lakini ni wa kwanza kusign form za mahudhurio ili tu upate posho yako ya siku. Huyo Zitto ana makosa kama amesema hayo unayosema hapa, lakini na wewe ni MNAFIKI MKUBWA kwa kushindwa kusema na kusimamia kile unachoamini kama ulivyoeleza mwenyewe hapo juu....ni vema kama utajiuzulu au kustahafu mapema ili kuipunguzia mzigo Tanzania, watu kama HAWAHITAJIKI kwenye uongozi wowote ule wa nchi.
 
Naomba msiwe distracted na watu. Msimamo upo wazi kabisa. Hakuna posho za vikao (sio tu nyongeza bali mfumo mzima wa posho za vikao twataka ukome. Watu wameamua kutwist nilichosema bungeni jana. Narudia, lazima tupinge posho hizi. Kwa nini wabunge walipwe kwa kukaa kitako? Huyu anayesema mie mnafiki yeye aseme anaunga mkono posho za kukaa au la. Wapiganaji msiwe distracted.
ZITTO naomba nikujibu in person.
Kama ni kweli, umefungua kinywa kinywa chako huko bungeni na kutamka maneno yanayomaanisha
kwamba unapinga posho za wabunge lakini unakubaliana na hoja ya kuongeza maslahi ya wabunge,
basi haufai.

Kama ni kweli, basi naomba nichukue fursa hii rasmi kukueleza kwamba wewe na Lowasa mnatofautiana
Umri tu.unatumia fursa hadhimu ya kuweza kusisika na majority tanzanians kutoa kauli, misimamo na hoja
ambazo una uhakika kwamba vitakufanya uonekane unapigania maslahi yao kumbe hakuna lolote, no wonder
masikio yangu yalikusikia ukisema wanasiasa wote wanatafuta umaarufu.Umaarufu wenu hautusaidii
watanzania kitu chochote.

Wapo watu hapa watakimbilia kusema tujadili hoja ya Posho, kama wewe mwenyewe unavyojaribu kuendelea
kutughiribu kwamba tusiwe distracted. NO. tutakujadili, kwa mapana, marefu, ukubwa, uzito na kina. Misingi
ya kukujadili ni kwamba, Kutokana na kauli yako tunalazimika kufunga brake na kuangalia upya kwamba,
malengo yako ya kuleta hoja ile yalikuwa ni nini? Umaarufu? for whose benefits?

Wewe ni mchumi, you well know kwamba TZS 250 earned through hard working and TZS 250 earned through
begging will surfice a transport fair from Ubungo to Kariakoo.

Acha kupotosha UMA wa watanzania, tena nyote wewe na wabunge wote wa CHADEMA acheni mara moja
kutufanya watanzania ni wajinga kwa kujifanya nyie ni wajinga. Yes. Mtu yeyote anayepinga masilahi yake
yasiongezwe ni mjinga. Ni wanasiasa wenye akili kama zenu ndio wanaopinga
Madakitari na waalimu wasiongewe Maslahi yao, YES, ni nyinyi, tatizo ni kwamba watanzania wengi hawajaamua
kufikiria.

Msimamo wangu ni kwamba Wabunge waongezewe maslahi yao, kama yatakuwa in the name of posho
au Mshahara ama vyovyote vile, I wish them earn more so that they are contented and do their Job right.
Tofauti ya hapo Rostamu atawaweka wabunge wote Mfukoni. na tutakuhoji how will you cover up the lost
income posho zikifutwa kweli, usiwakwaze wabunge wageni na network zako chafu.
 
Unafiki wa Zitto uko wapi? Zitto anapinga posho za vikao. Anasema kazi ya Mbunge ni vikao sasa posho ya vikao ya nini? Anasema ni bora basi mshahara wa mbunge uongezwe hata ukifika millioni 12 yeye yuko radhi lakini si posho ya vikao. Mshahara na posho ni vitu viwili tofauti kabisaaa! Posho kwa watumishi wa serikali huwa haiwi counted kwenye kuinuliwa mgongo. Hivyo ni bora kupandisha mishahara.

Namuelewa Zitto kwamba kwa nini ukae na kulipwa kwa kukaa? Hiyo ndio centre ya hoja yake na wala hakuna siku nimemsikia akisema hataki maslahi ya wabunge yaongezwe. Nimetafuta uanafiki siuoni. Nadhani aliyeandika ndiye mnafiki.
 
Back
Top Bottom