Old is Gold? Wangerudisha Rangi za Ndege Yetu...

Old is Gold? Wangerudisha Rangi za Ndege Yetu...

Niki muangalia huyo twiga na choka mwenyewe
Sidhani kama rangi ya zamani ilikuwa nzuri zaidi. Ya sasa ndiyo imekaa kileo. Tatizo liko kwenye nembo ya twiga tu. Iwe ya zamani au sasa zote siyo nzuri. Scale ya twiga mzima vs space wanayochora siyo nzuri
 
Kuna rangi zingine ni nuksi na zingine zina bahati chunguza hata nguo hahaha
 
Ndege kubwa zinapendeza na kuvutia japo sijawahi kuzipanda najiona fahari kuziona kwenye picha itapendeza Boeing itakayo kuja iwe na muonekano wa zamani zinavutia sana.
 
Yaani hadi leo sijaelewa, hizi rangi zilikuwa na ubaya gani? yaani ulikuwa hata ukipanda unajisikia 'fahari' na ndizo hizi kina Kapt. Mazula na wenzake waliziokoa kutoka kuvunjika kwa EAC... Natumaini wataona wenye kuhusika wala si jambo baya.. hakuna kitu wakati mwingine kizuri kama nostalgia..

Hiyo ndege B737 yenye usajili wa 5H-MVZ ni nembo ya makaburu baada ys shirika kubinafishwa.

Historia ya "nembo" yetu ilianza kupoteza thamani pale tulipokubali "kubinafsisha" Shirika letu la ATC kwa Shirika la Ndege la Afrika Kusini(South Africa Airways).Moja ya matokeo ya kumpa kaburu shirika letu ilikuwa ni kuondoa nembo ya twiga wetu kwenye mikia ya ndege zooote za Tanzania na kuweka nembo ya shirika la ndege la SAA.Hali iliyofanya pale penye mkia panapotakiwa kuwa na nembo ya Taifa letu,tukawapa Makaburu na wakaweka nembo yao...Twiga wetu akafichwa kwa mbele ili asionekane kwa urahisi.Hapo ndio ilikuwa mwanzo wa kupotea kwa "Twiga mwenda pole" wa Tanzania.

Tukahama toka ATC kwenda ATCL.Ndege zetu zikaanza kupeperusha nembo ya makaburu duniani,badala ya Twiga wetu.Kule ATCL ilipokuwa ikiaminika na kuwa na wateja kwa wingi,Makaburu wakateka soko kwa mgongo wa "ubia" na Tanzania.Taratibu twiga wetu akaanza kupotea na Nembo ya Makaburu ikaanza kupepea.Tukamtangaza kaburu na kumzimisha Twiga bila kujielewa.

Baada ya kuachana na makaburu,ndio tukaja na nembo hii ya kwenye jamii ya Bombadia.Siku za nyuma niliona kama unachokiona wewe leo,nikamuomba Mh.Mbarawa kupitia uzi huu,unaweza kupitia kujikumbusha Mhe. Mbarawa, turudishie Twiga wa ATC 'aliyetoroshwa' na Makaburu wa ATCL
 
Ndege kubwa zinapendeza na kuvutia japo sijawahi kuzipanda najiona fahari kuziona kwenye picha itapendeza Boeing itakayo kuja iwe na muonekano wa zamani zinavutia sana.
Yaani hata kuiona angani mtu anajua ni ndege ya wapi ile.. inajitangaza yenyewe... hizi nyingine hadi uzione kwa karibu!
 
Duh watu mna kauli kweli kweli.. eti vibajaji.. ila kuna kaukweli aisee.. yaani miaka ya themanini tulikuwa na ndege kweli.. leo hii tuna vijidege na tunataka kuona fahari


Sidhani kama Tanzania tushawahi kumiliki Ndege kuanzia kuanzishwa kwa Taifa letu, hii ndo mara ya kwanza tuna ndege zetu tulizonunua kwa fedha zetu wenyewe, someni Historia vizuri, hizo ndege zote kwenye Picha zako hatukuzimiliki tulikuwa tumezikodisha nyingine ktk Kenya Airways na mashirika mengine.

Ndo maana kwangu mimi Raisi Magufuli ndiyo raisi bora kuwahi kutokea nchi hii, hivyo hata ukituona tunasherehekea hivyo mnavyoviita vibajaji ni kwa sababu ni mara ya kwanza kwetu kumiliki Ndege, hivyo ni ,,Bajaji" ya kwanza, isitoshe kila kitu ni relative kuna wanao miliki Airbus Beluga kwa mara ya kwanza na kuna wanaomilikia ,,vibajaji" kama sisi!

Lkn Raisi Magufuli ataifikisha hii nchi mahali ambapo haijawahi kufika tangia ianzishwe!
 
....yakija majina ya ndege nafikiri ndio tutachoka zaidi, uatasikia chato1, chato 2, chato 3.... mpaka mwisho!
 
Yaani hadi leo sijaelewa, hizi rangi zilikuwa na ubaya gani? yaani ulikuwa hata ukipanda unajisikia 'fahari' na ndizo hizi kina Kapt. Mazula na wenzake waliziokoa kutoka kuvunjika kwa EAC... Natumaini wataona wenye kuhusika wala si jambo baya.. hakuna kitu wakati mwingine kizuri kama nostalgia..
Ukiangalia trend ya taasisi nyingi za umma, MACEO wanashindana kubadilisha Nembo badala ya performance. Umeshakuwa ni utamaduni.
 
Nani kakwambia hzo ni ndege zenu!!!?? kuwa makini kijana watu wanakula mapato hapo...
 
Sidhani kama Tanzania tushawahi kumiliki Ndege kuanzia kuanzishwa kwa Taifa letu, hii ndo mara ya kwanza tuna ndege zetu tulizonunua kwa fedha zetu wenyewe, someni Historia vizuri, hizo ndege zote kwenye Picha zako hatukuzimiliki tulikuwa tumezikodisha nyingine ktk Kenya Airways na mashirika mengine.

Ndo maana kwangu mimi Raisi Magufuli ndiyo raisi bora kuwahi kutokea nchi hii, hivyo hata ukituona tunasherehekea hivyo mnavyoviita vibajaji ni kwa sababu ni mara ya kwanza kwetu kumiliki Ndege, hivyo ni ,,Bajaji" ya kwanza, isitoshe kila kitu ni relative kuna wanao miliki Airbus Beluga kwa mara ya kwanza na kuna wanaomilikia ,,vibajaji" kama sisi!

Lkn Raisi Magufuli ataifikisha hii nchi mahali ambapo haijawahi kufika tangia ianzishwe!
Haifikishi nchi popote huyo..
Ukaguzi wa kwanza tu wa CAG kashaipiga Nchi 1.5Tril??
Kadanganye wajinga wenzio kijijini kwenu. .
Huyu hafai hata kidogo.
 
Ukiangalia trend ya taasisi nyingi za umma, MACEO wanashindana kubadilisha Nembo badala ya performance. Umeshakuwa ni utamaduni.
.. kana kwamba tatizo letu ni nembo tu; lakini hata nembo ya kitu lazima ufikirie impact yake... Nembo ya bidhaa ni alama inayoitambulisha sasa unaweka kitu ambacho hata hakijulikani kinamaanisha nini.. halafu unatarajia watu waone fahari kununua bidhaa hizo.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom