Ogopa sana kifaa kinachoitwa “Wireless Speaker”

Ogopa sana kifaa kinachoitwa “Wireless Speaker”

Habalini Wanajanvi.

Zamani zile kabla Tekinolojia haijakua sana hakukua na hizi Wireless Spika zenu za sasa, yaani ili mziki usikike basi Mitambo ilikua ni lazima iunganishwe na Spika kwa kutumia Nyaya.

Sasa siku hizi Spika za kisasa Haziunganishwi kwa Nyaya tena, zinaunganishwa kwa mifumo ya Wireless kama vile mfumo wa Blutooth, au Wi-Fi n.k.

Tatizo la hizi Wireless Spika ni kua zinaweza kuingiliwa na Mitambo tofauti na hivyo Msikilizaji akajikuta anasikiliza mziki usio wa Mitambo yake. Kwa mfano, Spika inaweza kua Dodoma lakini ikaingiliwa ki Blutooth au Ki Wi-Fi na Mitambo iliyopo Dar na hivyo Msikilizaji akajikuta anacheza Mziki wa Dj wa Dar.
Zamani haikua hivyo yaani kama Spika ipo Dodoma basi Msikilizaji atausikia Mziki wa Mitambo ya Dodoma, maana hakukua na njia ya ki Wireless kuunga Mitambo ya Mbali kama ilivyo Leo.

Zamani ilikua Spika ya Dodoma, Mitambo ya Dodoma na Mziki wa Dodoma.

Leo hii ni Spika ya Dodoma, Mitambo ya Dar na Mziki wa Dar.

Kweli Tekinolojia inakuja na Mambo Mapya.
Akili kubwa sana hii ya kiuandishi

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Sasa ujue kwamba kwa umbali uliopo kati ya Dodoma ma Dar teknolojia za Bluetooth na WiFi haziwezi kufanya kazi kwa kuifanya wireless speaker ifanye kazi.
Streaming unajua hufanyaje kazi?
 
Isee hatari sana unaweza kuta sasa speker zenyewe za kichina ila mziki wake unapasua ngoma za masikio na pia dj unakuta hana uteuzi mzuri wa playlist basi kila ngoma inaparamia juu kwaju uvuluvululu

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Zamani hizo Spika tulikuwa tunaweka kwa mtungi mkubwa basi hiyo sauti inakuwa ya kufa mtu. Siku hizi ni Wireless tu!!! Ha hah haha . Advance in Technology na bado tutaona na kusikia mengi ya Sayansi na Teknolojia.
 
Shida ni kwamba spika ya Dodoma ina matatizo ya kiufundi na mafundi wataalam wako Ilala Dar Es Salaam hasa hasa karibia na Muhimbili au Ocean Road



Sent using Jamii Forums mobile app
 
Pia kuna muda inaweza changanya miziki tofauti tofauti adi AC zikaungua kama ni technology india inabidi ipelekwe huko haraka kabla ya coil kuunguwa! Sema jambo zuri zina muda wa kudum za india hazikai Sana sishauri watu wazi nunuwe! Kuna moja brand ya IAGNUDN-003 ukinunuwa hii imekula kwako lifespan ni fupi sana!!
 
Utakuwa umekulia lumumba huku ni mpenzi wa yanga!
Kadi yao kwa nyuma imeandikwa kwa mandishi madogo sana bisha kila jambo hata kama hulijuwi!! Viumbe hatari sana hawa mkuu!!
 
Dahh! Watanzania wengine bwana!! Mkuu, naona Umesahau kuwa huwezi kujiunga katika kifaa chenye Bluetooth bila ya "password"..hii theory uliyoliongea haiwezekani labda mtu aruhusu vifaa viwili vyenye BLUETOOTH au WIFI viwasiliane kwa kutumika namba za Siri (password)..

Acha kuongopea watu
Zipo ambazo hazina password inategemea na mmiliki na ndie mwenye maamuzi!!! Lumumba bana kila kitu bisha ata kama hukijuwi!!!!
 
Zamani zile za Spika za zamani hakukuwa na hizi wireless Spika.
Hizi Spika za Kisasa - Karaoke Portable Spika haziunganishwi na Nyaya za Wachumia tumbo
 
Zipo ambazo hazina password inategemea na mmiliki na ndie mwenye maamuzi!!! Lumumba bana kila kitu bisha ata kama hukijuwi!!!!
Hahaha, Watanzania kila wafanyalo au watendalo lazima waweke siasa, sasa hapa mambo ya Lumumba yamekujaje??

Hizo zisizo kuwa na password zitatoa sauti ya kukujuilisha kuwa kuna kifaaa kinataka kuongea(comunicate) na kifaa chako, yote hayo ni kwasababu ya kuzuia mambo uliypyazyngumza yasitokee

Acha kuongopea watanzania..
 
Hiyo spika ya dodoma ndio wasikilizaji wanasema ni dhaifu?.
 
Back
Top Bottom