Ofisa JWTZ ahofiwa kutorokea Rwanda

Mkuu Nicholas ni kweli kabisa kuna jamaa wakati tunapiga shule chuo mwaka 2002 akanishangaza sana baada ya kuniambia yeye alishiriki vita ya kumwingiza Museveni mwaka 1986 (lazima alikuwa mdogo sana,lazima Museveni alitumia watoto kipindi hicho)Leo yuko Tanzania kila ukipiga story za Rwanda jamaa anamtetea Kagame mpaka utashangaa.Huyu ni raia wa Tanzania mwenye mafunzo ya kijeshi ninavyoelewa mimi mjeshi hapati uraia wa nchi nyingine zaidi ya ile aliyozaliwa na kuitimikia kijeshi.TISS wanashughulika na CDM,Mwanahalisi,Dr Ulimboka hawajui kuna kitisho cha toka nje na ndani ya mipaka yetu.

Wakati tunapigana vita na Idd Amini Tanzania ilikuwa na umoja leo hatuna umoja,udini umetugawanya,ukanda umetugawanya,ufisadi umetugawanya vyama vimetugawanya.Umoja umetoweka !!!!!.Ukiwaamba leo hii wananchi wa kawaida tukapigane vita nchi yetu imevamiwa wengine watauliza kwanza waliochota fedha za meremeta watakuwa mstari wa mbele,waliochota fedha za EPA watatangulizwa msatari wa mbele,waliokula fedha za Radar wana nafasi gani katika kuitetea nchi ?.wanaovuruga amani huku wameshika vitabu vya dini wana nafasi gani katika kuitetea Tanzania.

Ukweli ni kwamba Kikwete na serekali yake wamechezea tunu ya taifa kwa muda mrefu sana.Ni wakati muhafaka sasa nchi ikarejesha misingi ya taifa linaloitwa Tanzania.


Kama siku moja niliwahi waambia watu kuwa kipindi ch avita rwanda.. wapo wanafunzi wa secondary na vyuo walirudi kwako kupigana vita na baadaye kurudi kuendelea na shule...ni wazi vijana hao wengi walifikia ktk mafunzo mazuri ya kijeshi.Wakipewa mbinu na waliporudi kusoma walikuja na mikakati mingi tusiyoijua.


Vichwa vya lumumba km akina Ritz, hammy, na wengine wanajita wazalendo number moja, sijui nini na nini ,wameishia kutoa matusi mengiii..na kujigamba na jeshi ambalo lipo very porous...wanapiga raia tuu kujipima.Sijui km kupiga raia kunasaidia sana jeshi ambali linahitaji sana inteligentia ya raia.
 
Last edited by a moderator:
mwamunyange%20davis.jpg


Mkuu wa JWTZ, Meja Jenerali Davis Mwamunyange

*Adaiwa kutoweka na nyaraka nyeti
OFISA wa cheo cha juu katika Jeshi la Wananchi (JWTZ), anayeaminika kuwa na asili ya Rwanda, ametoweka katika mazingira ya kutatanisha, huku akiacha wingu la mashaka kwamba, hatua yake hiyo inaweza ikawa imeambatana na kupotea pia kwa baadhi ya taarifa muhimu za kijeshi.

Taarifa za kutoweka kwa ofisa huyo mwenye cheo cha luteni kanali, zinalihusisha tukio hilo na hatua za makachero wa JWTZ kufuatilia nyendo zake na zililifikia gazeti la MTANZANIA Jumapili kwa mara ya kwanza katikati ya wiki hii.

Vyanzo vya habari vya kuaminika vinaeleza kuwa, tayari maofisa wa JWTZ wameshaanza kufuatilia kwa karibu tukio la kutoweka kwa ofisa huyo, ambalo pia limezusha hali ya sintofahamu kwamba, huenda akawa ameondoka na nyaraka nyeti za kijeshi.

Kabla ya kutoweka ofisa huyo, ambaye nyendo zake zimekuwa katika darubini kali za makachero wa JWTZ, alikuwa akifanya kazi katika kitengo cha teknolojia ya mawasiliano ya kijeshi (IT).

Hatua ya kutoweka kwa ofisa huyo wa juu wa JWTZ anayetajwa kwa jina moja la Selumbo, imekuja siku chache tu baada ya kuibuka kwa msuguano wa kauli baina ya Ikulu ya Dar es Salaam na ile ya Kigali.

Chanzo cha msigano huo wa maneno uliogeuka na kuwa mzozo wa kidiplomasia, ni ushauri uliotolewa na Rais Jakaya Kikwete kwa Rais Paul Kagame wa kumtaka awe tayari kukaa meza moja na waasi wa kundi la FDLR wanaopigana Rwanda, kutoka mashariki ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC).

Tayari msigano huo wa Kikwete na Kagame umeanza kutajwa na baadhi ya wadadisi wa mambo kuwa tishio kubwa la kwanza la ustawi, uimara na misingi ya mshikamano ndani ya Jumuiya ya Afrika Mashariki, ambayo mataifa hayo mawili ni wanachama wake.

Siku chache baada ya ushauri huo, Kagame alinukuliwa na vyombo mbalimbali vya habari nchini Rwanda akimkejeli Kikwete, hata kufikia hatua ya kutoa kauli zenye mwelekeo wa vitisho dhidi yake.

Kauli hizo za Kagame zilisababisha Rais Kikwete, kupitia katika hotuba yake ya mwishoni mwa Julai, kujibu mashambulizi, huku akieleza bayana kushangazwa na kushtushwa na kejeli na matusi yaliyokuwa yakielekezwa kwake.

Akitumia maneno ya kidiplomasia ambayo yametafsiriwa na baadhi wa wachambuzi wa masuala ya diplomasia na sayansi ya siasa kuwa yanabeba ujumbe mzito, Rais Kikwete alisema alikuwa amesikia yote yanayosemwa kutoka Rwanda na alikuwa hakusudii kuyapuuza.

Kauli hiyo ya Kikwete ambayo ilitanguliwa na ile aliyoitoa siku chache mkoani Kagera ya kuwataka wahamiaji haramu kuondoka nchini, ilifuatiwa na matukio ya kuondoka nchini kwa Wanyarwanda wanaokadiriwa kuzidi 5,000.

Wakati hali ikiendelea kuwa ni ya mashaka na kutoaminiana kati ya Tanzania na Rwanda, katikati ya wiki hii, gazeti dada la MTANZANIA Jumatano, lilikuwa na habari kubwa yenye kichwa cha habari kisemacho; ‘Nini kinamtia Jeuri Kagame?’ ambayo pamoja na mambo mengine, ilieleza namna watu wenye asili ya Rwanda walivyojipenyeza katika taasisi mbalimbali nyeti za umma.

Kuvuja kwa taarifa za kurejea Rwanda kwa maelfu ya wahamiaji haramu sambamba na hizi za sasa za kutoweka kwa ofisa wa juu wa JWTZ kunathibitisha kuhusu kuwapo kwa mwelekeo huo wa mambo.

Vyanzo vya habari vya gazeti hili, vinamtaja ofisa huyo kuwa ni mmoja wa makachero wenye asili ya Rwanda waliokuwa wakifanya kazi ndani ya JWTZ na ambao wanahofiwa kuwa watu wenye mawasiliano ya karibu na serikali ya Rwanda, kwa malengo ambayo bado hayajawekwa bayana.

“Ni kweli, huyo ofisa ametoweka jeshini na sijui sababu zilizo nyuma yake…hili suala la kuwa anakusanya taarifa za siri za jeshi letu na kuzipeleka Rwanda nadhani ziligunduliwa na watu wetu ambao wapo kwenye mfumo wa kijeshi,” alidokeza mmoja wa watoa taarifa wa MTANZANIA Jumapili.

Msemaji wa JWTZ, Meja Erick Komba, alipoulizwa na gazeti hili kupitia simu yake ya kiganjani kuhusu ukweli wa taarifa hizo, alishindwa kukubali au kukataa, kwa kile alichoeleza kuwa suala hilo ni zito hivyo alikuwa akipaswa kuzungumza kwanza na viongozi wake kabla ya kulitolea taarifa.

Meja Komba alieleza kuwa, wanajeshi wanaotoroka ni wengi na wapo waliofungwa kwa kosa hilo la utoro.

“Jamani suala hili ni zito, naliogopa, nyinyi hamlioni kama ni zito? Sio kwamba sipendi wananchi wapate habari, suala hili tupeni muda kwanza tulifanyie ‘analysis’, mbona wanajeshi wengi wanatoroka na hamripoti! Waliotoroka ni wengi, wangine wametorokea Rwanda na kwingine na wamefungwa.

“Ni lazima kwanza niongee na mabosi wangu ndiyo nizungumzie vizuri hili… njoo ofisini Jumatatu (Kesho),” alisema Meja Komba.

Sanjari na tukio hilo, taarifa zaidi zilizonaswa na gazeti hili zimedai kuwa sasa imebainika pasipo shaka kuhusu kuwapo kwa makachero wa Serikali ya Kigali wanaodaiwa kupandikizwa katika taasisi na idara nyeti za serikali kwa ajili ya kufanya ushushu kwa maslahi ya Rwanda.

Inadaiwa kuwa intelijensia ya JWTZ iliyo na mizizi ndani na nje ya nchi ilibaini mapema kuwapo kwa majasusi wa Kinyarwanda ndani ya mfumo wa dola na nyendo zao zimekuwa zikichunguzwa kwa muda mrefu na zilibainisha hali hiyo.

ss si tunajifanya nchi ya amani na nyenye upendo na watu wote, ngoja tuonje shubiri,

watu wa rwanda wako wengi mno wanegine ni wakuu wa sekondari, wangine wamewahi kuwa mawaziri, wengine wamewahi kuwa wakuu wa vyombo mablimbali vay nchi, wengine wamepewa hadi passport za Tanzania

sio hilo tu hata Kinana KM wa CCM ni raia wa Tz kutoka Somalia au sivyo? mwenyekiti wa ccm mkoa wa Mara sio mtanzania nk. tukumbuke hakuna anayeacha asili yake hata akikana uraia wake. wengine wanaukana kwa maelekezo ya serikali zao kuwa watawatumia katika maeneo fulani ndio maana strategically wanapoingia katika nchi yetu wanakuwa katika maeneo maalumu kabisa

wapo wengine wanafanana kabisa na Kagame lkn wana passport za tz, vyeti vya kuzaliwa vya tz, tumewasomesha kwa kodi za watz, tunatarajia nn?

ukicheka na nyani utavuna mabua,?
 
Hii ndio Tanzania bwana, Ukachero ni kawaida ndani ya vyombo vya ulinzi mbona sisi tunao wengi tu ndani ya majeshi ya watu. vilevile tunao wanasiasa ndani ya nchi moja hivi kusini mwa tanzania.
 
Mkuu ALEYN cheo cha Lt Col ni kikubwa sana jeshi na si JWTZ tu bali majeshi yote unayoyajua dunia.Huyu mjeshi kaanzia Lt usu akapanda hadi Lt kamili,then Capt,Major hadi Lt Col lazima kaenda kazi kadhaa za nguvu eg Platoon cammander course (kiongozi wa kikosi cha between 26 - 64) lazima atakuwa amehudhuria course ya Company cammander (kiongozi wa kikosi cha jeshi 80 - 225) halafu atakuwa ana mafunzo ya kuongoza Battalion (kiongozi wa between 300 - 1200) kutegemeana na mfumo wa jeshi au aina ya kikosi eg Artillery units,Logistics units, or air defence and ets au unafuata system gani ingawa inafahamika JWTZ ilikuwa ikifuata mfumo wa China na Russia siku hizi naona Marekani nayo inajiingiza ingiza.

Kifupi Lt Col ni mjeshi wa cheo cha juu sana huyu kabakiza ngazi mbili afikie cheo cha one star general ili aweze kuongoza regiment au brigade.

Nakili kuwa nilijichanganya, JWTZ wapitishe msako mkali. Wakibainika ni Kuwaua tu.
 
Last edited by a moderator:
Sijui kwa nini 'kipeperushi' hiki Mtz J.pili kinapenda kukuza suala la rwanda. Kila wiki kagame kagame. Hamna kingine cha kuandika?
Wengine kama mimi ninapenda sana "kipeperushi hicho". Kwako, usifungue sehemu hiyo wala kusoma!
 
Ukiwa mwanaume legelege mke atakuletea watoto wa nje na kukuambia ni wako ukija shtuka wameishamaliza chuo kikuu na wanajitegemea, Tanzania ni sawa na mwanaume legelege asiyejua majukumu yake...... Ni aibu kwetu sisi wote
 
Kumbe wewe unafahamiana naye huyo jamaa? Unajuaje kama aliondoka miezi mitatu ilivyopita? Maana migogoro na Kagame imeanza mwezi wa sita mwanzoni, ina maana wakati migogoro inaanza jamaa alikuwa ameshaondoka? Acha uzushi wewe. Au wewe ni mmojawao hao waliopenyezwa nchini?
Mkuu Lukolo mimi jamaa huyu nilishamstukia siku nyingi tu, jaribu kufatilia thread/majibu yake siku za nyuma. Back 2 the point - Taifa letu alikuwahi kuwa na moles kwenye vitengo vyetu nyeti wakati wa utawala wa Habyalimana (MHUTU) na wenzake walio mtangulia (Watutsi); kinacho shangaza kwa nini tangu utawala wa sasa (Rwanda) uingie madarakani naona wako obsessed ku-recruit na pukenyeza moles nchini mwetu wakati hatujawahi kuwa na uhasama/vita na Rwanda na wala hatutegemei kama hilo linaweza kutokea - sasa moles wanapenyezwa kwenye jeshi letu ili iweje, kama ingekuwa upelelezi wa kiuchumi/bihashara ningeweza kuelewa - lakini jeshi? Hii sio dalili nzuri. Kwa akili za kawaida upenyezaji wa moles kwenye JWTZ na Polisi unaweza kutafisiriwa vipi - simple, utawala wa sasa nchini Rwanda hawana/hawakuwa nia njema na TAIFA letu (tangu waingie madarakani) na hii sio kwamba imeanza leo ni long term plan za utawala huu - watu wanafikili uhamiaji holela wa jamaa hawa mkoani Kagera ni bahati mbaya - si kweli, matatizo ya kuchonga nchini DRC (Kivu) wanataka yajirudie Mkoani Kagera.
 
sijui wakiondoka wote kwa pamoja: wajaluo na wakurya ambao ni mapandikizi ya Kenya, wahaya feki ambao ni waganda, wanyasa na makabila la kusini ambao ni wa zambia na wamalawi, warundi na wanyarwanda wote wakasaidi nchi zao..tubaki na wakwere, wapemba wenye wake wa kisomali etc...
Mkuu NICHOLAS hapa tunazungumzia mambo ya usalama wa Taifa letu, nchi unazo zizungumzia hazijawahi kuvamia nchi jirani na kuondoa watawala madarakani na kuweka wanaowapenda, narudia kupindua Serikali halali au kutishia uhai wa Kiongozi mwenzake - Baba wa Taifa na Mzee Jomo Kenyatta hawakuwa in good terms lakini hatukuwahi kusoma mahali kwamba Kenyatta au Kambarage akimtishia maisha mwezake hata Iddi Amini alizungumzia mambo ya kuingia ulingoni (Ngumi) na Kambarage kama utani. Raia wengi unao wazungumzia hapa ni economic refugees hawana an hidden agenda za kujitanua kwa njia yoyote ile hata kama ni kupigana vita ili watimize malengo yao wako radhi kabisa - watu wengi tishio hili lililo dhahili wala hawalioni!!!!! Hebu niambie ni nchi gani za jirani ziliwahi kuweka/penyeza moles kwenye JWTZ, Polisi kawaida, Uhamiaji and the list goes on. Mkuu Nicholas je nchi jirani kupenyeza moles kwenye vitengo nyeti in peace time kunashiria nini?
 
Mkuu Lukolo mimi jamaa huyu nilishamstukia siku nyingi tu, jaribu kufatilia thread/majibu yake siku za nyuma. Back 2 the point - Taifa letu alikuwahi kuwa na moles kwenye vitengo vyetu nyeti wakati wa utawala wa Habyalimana (MHUTU) na wenzake walio mtangulia (Watutsi); kinacho shangaza kwa nini tangu utawala wa sasa (Rwanda) uingie madarakani naona wako obsessed ku-recruit na pukenyeza moles nchini mwetu wakati hatujawahi kuwa na uhasama/vita na Rwanda na wala hatutegemei kama hilo linaweza kutokea - sasa moles wanapenyezwa kwenye jeshi letu ili iweje, kama ingekuwa upelelezi wa kiuchumi/bihashara ningeweza kuelewa - lakini jeshi? Hii sio dalili nzuri. Kwa akili za kawaida upenyezaji wa moles kwenye JWTZ na Polisi unaweza kutafisiriwa vipi - simple, utawala wa sasa nchini Rwanda hawana/hawakuwa nia njema na TAIFA letu (tangu waingie madarakani) na hii sio kwamba imeanza leo ni long term plan za utawala huu - watu wanafikili uhamiaji holela wa jamaa hawa mkoani Kagera ni bahati mbaya - si kweli, matatizo ya kuchonga nchini DRC (Kivu) wanataka yajirudie Mkoani Kagera.
Mkuu Bukyanagandi, Kagame ana mashaka makubwa sana na Tanzania kwa kuwa ndiyo iliyokuwa msuluhishi wa migogoro yao tangu kabla ya Habyarimana kuuawa. Tanzania inajua vema ushiriki wa Kagame na RPF katika mauaji yale ya kimbali wakati huo akipigana kutokakea Uganda. Unajua ni kwanini Kagame alimuua Prof. Jwani Mwaikusa? Mwaikusa alikuwa na ushahidi wote wa ushiriki wa Kagame kwenye mauaji ya Kimbari. Na wauaji walimuua Mwaikusa na kuchukua tu zile document zake zenye ushahidi na kuishia.
Hata Kikwete anaposema Kagame aongee na wapinzani anajua vema kwamba Kagame ni nani na ameshiriki vipi kwenye lile sakata. Kwa hiyo Kagame amekuwa kama ni mtu wa kujihadhari sana, anaogopa asije akatajwa hadharani.
 
Last edited by a moderator:
Mkuu Bukyanagandi, Kagame ana mashaka makubwa sana na Tanzania kwa kuwa ndiyo iliyokuwa msuluhishi wa migogoro yao tangu kabla ya Habyarimana kuuawa. Tanzania inajua vema ushiriki wa Kagame na RPF katika mauaji yale ya kimbali wakati huo akipigana kutokakea Uganda. Unajua ni kwanini Kagame alimuua Prof. Jwani Mwaikusa? Mwaikusa alikuwa na ushahidi wote wa ushiriki wa Kagame kwenye mauaji ya Kimbari. Na wauaji walimuua Mwaikusa na kuchukua tu zile document zake zenye ushahidi na kuishia.
Hata Kikwete anaposema Kagame aongee na wapinzani anajua vema kwamba Kagame ni nani na ameshiriki vipi kwenye lile sakata. Kwa hiyo Kagame amekuwa kama ni mtu wa kujihadhari sana, anaogopa asije akatajwa hadharani.

Kuondoka kwa huyu Askari kumeniuma sana. Humu ndani Jf kuna Wanyarwanda wengi tu, pole sana kwa kuwajibu Mkuu.
 
Last edited by a moderator:
Kuondoka kwa huyu Askari kumeniuma sana. Humu ndani Jf kuna Wanyarwanda wengi tu, pole sana kwa kuwajibu Mkuu.
Yah, ninajua wapo wengi sana na wana maneno kwelikweli. Tutaendelea kuwajibu tu hadi mwisho, ili wajue kwamba tunawajua vema.
 
Jamani mbona wanyarwanda wapo tu wengi jeshini,na walishashikwa siyo mara moja mpakani wakiwa na nyaraka za jeshi letu,sasa kwakuwa kuna mgogoro kati yetu na Rwanda ndo hayo yanaibuka,yapo siku nyingi sana.
 
hapo kwenye jk ni mwanajeshi ndipo ulipokosea mkuu, jk alitoka jkt akaenda kuwa mwalimu wa katiba ya ccm jeshini, anajua mwenyewe sarakasi aliyocheza akawa kanali.
Mkuu kuna tofauti gani kubwa kati ya JKT na JWTZ? je JK alistaafu jeshi akiwa na cheo gani? Nani kakwambia vyeo vya jeshi vinatolewa kama njugu au vyeti vya ONLINE!! Sarakasi ninazo zijua za JK niza kucheza BASKETBALL, sasa kama kuna sarakasi za ziada hiyo sijui mkuu.
 
Mkuu kuna tofauti gani kubwa kati ya JKT na JWTZ? je JK alistaafu jeshi akiwa na cheo gani? Nani kakwambia vyeo vya jeshi vinatolewa kama njugu au vyeti vya ONLINE!! Sarakasi ninazo zijua za JK niza kucheza BASKETBALL, sasa kama kuna sarakasi za ziada hiyo sijui mkuu.

jk hana tofauti na halima mdee kijeshi wote ni makuruta wa jkt, hivi inawezekana mwalimu wa katiba ya CCM jeshini akapanda mpka kuwa kanali.
 
Kumbe ndiyo maana
kajamaa kana kidomo domo sana! Yaani mpaka mamluki anafikia cheyo cha
Luteni Kanali hagunduliki tu?? Naanza kupata wasiwasi na intelijensia ya
JWTZ.
mleta uzi kaja kuwatisha tu mbona hazungumzii wa tanzania walioko katka jeshi la rwanda ambae wa cheo cha juu sasa ni kanali au majasusi wa tz waliopo vyuo vikuu vya rwanda kama malecturers
 
Back
Top Bottom