Ofisa JWTZ ahofiwa kutorokea Rwanda

Ndugu usiogope Mtu mwenyewe kumbe wa IT situnaflsh maprogram yote kijeshijeshi tunaanza upya -Mi ningeogopa sana kama angekuwa mkuu wa pale Ngelengele au Monduli

Sasa kama keshapita kote huko Ngerengere, Monduli n.k.? Hawa jamaa wako siku nyingi sana ndani ya majeshi yetu even ndani ya TISS, watanzania tunaona sifa tukiambiwa wakarimu kwa kuruhusu wageni bila hata kuhoji.
 
sasa kama keshapita kote huko ngerengere, monduli n.k.? Hawa jamaa wako siku nyingi sana ndani ya majeshi yetu even ndani ya tiss, watanzania tunaona sifa tukiambiwa wakarimu kwa kuruhusu wageni bila hata kuhoji.

bado hatujachelewa, tuanze kwa kasi kuwadhibiti!
 
shame! shame! shame,huenda tuma matumaini feki na jeshi letu labda ni taasis nyingine tu kama wizara zetu, mashirika ya umma na timu ya taifa stars...ee Mungu tulinde.
 
Hakuna kitu hapo huyo ofisa hawezi kuwa na jipya ht km akikimbia na nini
 
Kumbe ndiyo maana kajamaa kana kidomo domo sana! Yaani mpaka mamluki anafikia cheyo cha Luteni Kanali hagunduliki tu?? Naanza kupata wasiwasi na intelijensia ya JWTZ.


Kutokea Mamluki jeshini au usalama sio jambo la ajabu kwenye masuala ya ULINZI SA Taifa.......Kila nchi INAO fungu la ku recruit ."....Askari wa nchi kadiri ys risk of war....kwa ajili ya kuwapa taarifa......"..
pia inawezekana kabisa ku plant informers pale jeshi husika linapotangaza kuajiri Askari ....

Hii ishu ya Sagamba .ipo kwenye corridors za mambo ya usalama kwa miezi mitano iliyopita lilipotoka.......wenzetu wanapenda ku recruit Watu wa pembezoni.

Adhabu ya kufanya ESPIONAGE inajulikana ni KIFO ......kunao maafisa kwenye ngazi mbali mbali wanaofuatiliwa........wakipotea...msiwasikitikie....that is the rule of the game....
 
Aisee hata Kikwete mrundi! Bagamoyo waliwekwa watumwa wenye afya mbovu kama baba yake
 
Hii sio habari ya kuandikwa na kuishia ikiwa humu, moods be patriotic, ama ndi ya Edward Snowden haya ......
 
Shukrani kwa taarifa mkuu...ukijenga utaratibu wa kusoma Threads kabla hujaweka mpya utasaidia kupunguza duplication ya threads...Wenzako wawili washakutangulia!
 
Aisee hata Kikwete mrundi! Bagamoyo waliwekwa watumwa wenye afya mbovu kama baba yake


Ndugu yangu tukijadili hapa nchi itaanguka sasa hivi! Jamaa katimka mwaka sasa ndo inakuja leo?
Tukiwaambia nji ngumu hii hamsikii na nyinyiemu yenu!
 
Mmmh mimi naona Tanzania inataka kuweka chumvi kwenye Chakula ili kiwe kitamu. Suala muhimu ni kuwa miaka yote walikuwa hawajui Kama kuna mashushu ndani ya Jeshi na Vyombo vya ulinzi vya TZ?.
 
Ndugu usiogope Mtu mwenyewe kumbe wa IT situnaflsh maprogram yote kijeshijeshi tunaanza upya -Mi ningeogopa sana kama angekuwa mkuu wa pale Ngelengele au Monduli
Wewe ndio hujui kitu kwa cheo chake yule anaujuzi wa kuwa mkuu wa kikosi chochote angeweza kupelekwa ngerengere kuwa co au mkuu wa chuo au monduli kuwa co au mkuu wa chuo IT ni sifa ya ziada sio inayompa vyeo
 
Hivi mtu akiwa mtanzania mwenye asilia ya 'kigeni' katika mabano ndani ya JWTZ ni jambo la ajabu? Lt. Hans Pope, Meja Jenerali Walden, Major Hall , Kanali Chacha (wapo Kenya/Tanzania) n.k inakuwa ndo suala kubwa la kuingiza Tanzania ktk mgogoro wa 'vita-mtandao-wa-kijamii? Majeshi mengi duniani yana watu wa namna hiyo Ufaransa, USA, Marekani, India (mradi una asili ya India unaweza kujiunga na Jeshi la India hata kama umekua na kuzaliwa Tanzania. Na suala la AWOL (Military Absent Without Leave) ni suala linalotokea kwa ngazi zote kutokana na sababu mbalimbali. Hivyo ni kweli JAMIFORUMS inabidi kuwa makini kusubiri official statement toka makao makuu ya JWTZ na siyo kuanza kuitia nchi katika uvumi usio na tija.
 
amewezaje kutoroka?, hapo kuna udhaifu na watu inabidi wawajibike
 
Lakin tulisema kuna vitu vya kugawa kama njugu, ila c paspoti, na vyet vya kuzaliwa.. mkatupuuza.. na bado!! ucione hao polis wanavyoua watu, wengine kungoa kucha, weng wao si watanzania mkuu...
 
Inasikitisha jinsi watanzania tusivyo sirias. Jeshi lipo lakini - Ndege ya Qatar ikatua kIA na kuchukua Twiga bila wao kujua. Sasa hivi tena majasusi wa Kinyarwanda wapo ndani ya nchi. Lo! Na huyu mwanajeshi atakuwa wa pili kwa mwaka huu kutoroka na nyaraka za jwt.
 
Hata Al qaeda walikuwa na majasus kwny Jesh na vyombo vya ulinz vya Marekan lakin bado tunaamin US una jesh imara zaid Dunian kwa sasa, huyo jamaa katoroka baada ya kugundua kuwa anafuatiliwa, suala la ushushushu ni mambo ya kawaida fuatilia ujue kuwa hakuna jesh Dunian lisilokuwa na mamluk wa majesh mengine, ujasir na ubingwa upo kwenye kuwastukia mapema! We unadhan M23 hata wakiwa na mashushushu kwenye Drone wanaweza kuepuka kipigo?

Kagame hana ubavu wa kuitisha Tz, ni chui wa karatas anaetisha Swala kama yule museven alietishwa akakimbilia kuomba asuluhishwe na BLAIR, hapa akijaribu tunam Iddi Amin!
 
Kabla ya kutoweka ofisa huyo, ambaye nyendo zake zimekuwa katika darubini kali za makachero wa JWTZ,
Utasemaje alikuwa anafuatiliwa kwa "darubini kali" wakati ametoweka without a trace na manyaraka yenu ya kijeshi na hamjui alipo???
This is so funny, eti wanajisifu kwamba walikuwa wanamcheki nyendo zake kwa karibu sana, lakini kawatoka! Laughing out loud!


Msemaji wa JWTZ, Meja Erick Komba, alipoulizwa na gazeti ...."Jamani suala hili ni zito, naliogopa, nyinyi hamlioni kama ni zito? .... mbona wanajeshi wengi wanatoroka na hamripoti! Waliotoroka ni wengi, wangine wametorokea Rwanda na kwingine nawamefungwa.
Msemaji wa JWTZ nae kituko, eti hili swala "naliogopa." Yani hata mimi ambae sijasoma hata darasa moja la mass communication nisingeweza kusema suala la ofisi yangu, ambalo mimi ndio natakiwa kuliongelea, "naliogopa." Hawa wazee masikini hawana exposure hata za kuangalia ma TV ya nje waone spokespeople wanavyojibu maswala magumu ya kinchi? Msemaji wa Jeshi anaiambia nchi hili swala "naliogopa."

Halafu anasema hii si mara ya kwanza kwa wanajeshi kukimbilia Rwanda. Kama si mara ya kwanza mbona suala unaliogopa????
 
Naomba Raisi Jk awaite wamiliki wote wa vyombo vya habari ikulu awaambie nini cha kuandika na chombo kikiuka kifungiwe mara moja. Huu uandikaji ni wa ovyo sana, ni sawa na kwenda kijiweni na kusema funguo za geti la home zimepotea pamoja na funguo za safe. SHAME ON US .
 
Kikwete ana nini na rwanda???

Matokeo ya kauli za dharau zinaliingiza taifa kwenye matatizo makubwa.


Sent from my BlackBerry 9700 using JamiiForums

Daud mchambuzi ukiona baba yako anatukanwa mtaani msitiri kama hutafanya hivyo ukamcheka basi ujue utachukua laana na utakosa radhi. Kama wabisha basi usimsaidie endelea kusema kakosea utaona urithi wako utakapopokwa au wewe sie wakwetu?
 
Back
Top Bottom