Official: Wimbo mpya ya Roma Mkatoliki - Zimbabwe

Official: Wimbo mpya ya Roma Mkatoliki - Zimbabwe

Huo hapo

Sent from Ili iweje
Mistari bora katika wimbo wa Roma, Zimbabwe.

Mungu wa Paulo, ndiye Mungu wa Daudi.
Na ndiye Mungu wa John mnayemuita Yohana wa Wayahudi.

Kipi bora?, nife mseme nilikufa kiharakati?.
Siogopi kufa ila nawaachaje wanaobaki?.

Je kaburi langu mtalipalilia majani?.
Nimeumwa hamjakuja kuniona mnangoja mje msibani?.

Ahsante mliopaza sauti, Nimeiona nguvu ya umma.

Nanasi linaoza msoga tikiti lanaoza shamba.

Kutekana tekana na uhuni wa kishamba.

Aminini siku hazigandi, we ni Yanga mimi ni Simba kuwa mpinzani siyo dhambi.
Ipo siku mtawala atakuwa mpinzani simba akichukua kombe sijui atapona nani?.
 
Umeenda mbali sana mkuu! Hiko ni kionjo tu,ungekuwa umebahatika kucheza mgambo au kupitia jkt ungeelewa hilo neno Zimbabwe,hutumiwa tu kuongeza hamasa pindi munspokimbia mchakamchska
Mkuu,Jaribu kuliangalia jina Zimbabwe katika jicho la mbali/tatu.


Zimbabwe liweke katika mizani ya uongozi,uchumi nk..kisha tumia ubongo na ufahamu kufanya upembezi na kuchanganua.
 
Nakwenda Zimbabwe, kuna kila sababu yakuamini anaitabiria Tanzania inaelekea kuwa Zimbabwe, kiuchumi (inaanguka) kisiasa (udikteta) kijamii (Maisha duni).

Kuna ule mstari kuhusu ripoti ya kutekwa kuna fumbo kubwa sana pale. Yan mtekaji ndie anapewa kazi ya kuchunguza mtekaji.
 
Sikuona nyota kwa shoulder
Ila najua wewe ni soldier
Ulikuja mwenyewe ama ulipewa order
 
Wimbo mzuri lakin angeweka na kizimbabwe mfano kishona kidogo nadhan huu wimbo kwa Zimbabwe ange hit sana pia..


Ndeipa roma
 
Kwann asiwataje sasa.....na mbona yupo nao.
Majibu kwa nini hawataji yapo kwenye wimbo.

Mwanangu aliuliza Mama lini baba atarudi,
Na mke wangu aliwaliza kuwashukuru sina budi.

Fahamu ya kuwa mimi sio tu rapper pia ni baba wa familia,
Nina watoto pia mahitaji nawapa kama isemavyo biblia.

Kipi bora nife mseme nilikufa kiharakati,
Siogopi kufa ila nawaachaje waliobaki.

Je nani kati yenu mwanangu atampa malezi,
Wapi atapata mahitaji wapi atapata mapenzi,
Mama nae wapi atapata mahitaji na malezi.

Na ripoti ya upelelezi vipi akiiteka mtekaji?
 
Hujaelewa mkuu! Zimbabwe ametumia kama kiitikio lkn hakija beba maana yeyote,nilipokuwa jkt miaka kadhaa iliyopita tuliimba sana kwenye mchakamchaka hiko kiitikio cha Zimbabwe.
Kua mpole hata sisi jeshi tulienda....sema wewe hujaona maana ila sio kwamba hakijabeba maana.Roma kila alichokiimba kwenye wimbo wake+video vina maana.Kumuelewa Roma ni swala la kutuliza akili tu

[HASHTAG]#NakwendaZimbabwe[/HASHTAG]

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mkuu,Jaribu kuliangalia jina Zimbabwe katika jicho la mbali/tatu.


Zimbabwe liweke katika mizani ya uongozi,uchumi nk..kisha tumia ubongo na ufahamu kufanya upembezi na kuchanganua.
Sawa mkuu
 
Umeenda mbali sana mkuu! Hiko ni kionjo tu,ungekuwa umebahatika kucheza mgambo au kupitia jkt ungeelewa hilo neno Zimbabwe,hutumiwa tu kuongeza hamasa pindi munspokimbia mchakamchska
We jamaa acha kujifanya mjuaji kizazi hiki wengi jkt wamepita....Binafsi nlikua mgambo kwa kanole na uo wimbo wako naujua ila hauapply hapa kwenye wimbo wa Roma.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
f6b6459bb67d8a165a5001b0ec39f308.jpg
nakwenda Zimbabwe.
 
ila kwa hiyo ngoma soon tutasikia Roma katekwa tena....Labda aishie Zimbabwe hukohuko.
 
Back
Top Bottom