Obama ana Hasira na Winnie?

Obama ana Hasira na Winnie?

Nitofautiane nanyi woote, Mandela ameshakufa, kwa mujibu wa kiapo cha ndoa tayari kifo kishawatenganisha, ile hati ya ndoa imeisha thamani. anabaki kuwa graca na huyu hayati mandela, sasa kwa kuwa huyu Mandela enzi za uhai wake alikwishaapa kuwa mume wa winnie, kwa sababu zao binafsi wakaamua kutengana haifuti ukweli kuwa once upon a time hawa watu walikuwa mtu na mkewe.

kwa hiyo basi kwa kuwa Mandela amekufa, wale aliopata kututangazia hadharani kuwa ni wake zake wanakuwa wajane wake. Enzi za uhai wake akimwita x-wife, zama za umauti anakuwa widow wake full stop.

KAMA ILITOKEA MNAVYOSIMULIA, BASI WAMEMNYANYASA WINNIE.

this is too hypothetical and practically very impossible!
 
Na Madiba kumuoa mke wa best ake inamaana alikua akimzimia toka kitambo!!hahahahah

no you are very wrong!! Kama rafiki mkubwa wa Samora alikuwa sahihi kumuoa mke wa rafiki yake, naamini hata Samora alikuwa anafurahi huko mbele ya haki! Unajua mojawapo ya mambo yanayokera mtu unapofikiria kufa, ni je wapendwa wako wataishije? Watapata furaha ya maisha? So mandela did very well kwa kufanya kile Hayati samora angependa kitokee. That's happiness for the loved ones. Au sio?
 
Yaani swali lako ni typical uswahili. Unakuta kaka yenu ana hawara ama ex wife, siku mnamzika kaka yenu kila mtu anajidai anampenda ex ama hawara. Hakuna heshima wala nini! Winnie is part of family kwa sababu ana watoto na madiba. Graca ni mke!

Sasa uswahili uko wapi hapo? Mbona finally umejijibu (rejea sentensi zako mbili za mwisho)? Unafyatuka tu!
 
Winie msaliti kwa madiba kama jepesi kwa chama tawala kijacho.
 
Haya jamani ahsanteni sana ila itifaki inamtambua graca kama ndo mke halisi wa marehemu mandela. Hata hivyo ilikuwa ni vigumu sana kwa winnie kuendelea kumsubiria mandela na hali mtu amefungwa maisha. Sema labda hata baada ya kutoka mandela jela mama aliendelea kujiburudisha that is why mdingi akamua kumtema. I believe that mandela was know for good in forgiving, if at all winnie could seek apology to mandela madiba could forgive her but huenda mama alikuwa na kichwa ngumu na ukizingatia madiba alikuwa 70 or so alipotoka jela akaona labda asingeweza kazi vizuri kama vijana wa mitaani. But winnie was wrong according to my view. Good rest madiba
 
Ndiyo maana Slaa anaogopa kwenda kwenye matukio maana hana mke ana vimada-funguka. Maana yangu ni kwamba mke wa Mandela aliyefiwa na mme ni Gracia, si Winnie- hiyo ni culture ya wazungu. Zuma anataja wote kwa sababu hata yeye ana wake 5.

Kwani mandela mzungu?
Obama je?
Labda ni itikadi na utaratibu alio shauriwa!!!
 
Sasa uswahili uko wapi hapo? Mbona finally umejijibu (rejea sentensi zako mbili za mwisho)? Unafyatuka tu!

GT hujifunza kuvumilia na kuthamini mawazo ya wengine!!
Usiwe mkali k-boko!!
 
Well said mkuu, kama Mandela aliweza kuwasamehe wajahili waliotaka kumtia kitanzi kwa nini hakumsamehe Winnie - hata kama alikuwa hataki kuendelea kuishi naye sioni sababu ya chama cha ANC kuendelea na njama za kutaka kumdhalilisha mbele za wageni? Watu wanacho sahau ni kwamba kelele na vitimbwi vya Winnie kwa Serikali ya makaburu wakati Mandela yuko kifungoni ndio kulikuwa kunaifanya Dunia ikumbuke Nelson Mandela, bila ya Winnie kuwasumbua Makaburu na kufanya vyombo vya habari kuwa vina andika habari zake mara kwa mara Mandela angesahulika, tuwe wakweli hapa - Winnie aliteseka sana na wanawe, aliwahi kufungwa gerezani, nyumbani kwake, kupigwa marufuku asikutane na watu etc, nasema hivi pamoja na mapungufu yake kama binadamu wengine tulivyo sihungi mkono mbinu za akina Jacob Zumma na kundi lake kufanya mbinu za kumu-ignore mama huyu - binafsi nimekasirishwa sana na njama hizi - Baraka Obama atakuwa alighafirika tu awezi kumu-ignore Winnie kimaksudi, si ajabu hajawahi kukutana nae hata Baraka na familia yake walipo kuwa wanakuja kumtembelea Mandela nyumbani kwake nadhani walikuwa wanakutana na Graca sio Winnie, Winnie alikuwa anaishi mbali na Graca. Tuwe wakweli hapa mtu uwezi kuzungumzia Mandela ukamsahau Winnie, looking back now naona wakina Zuma walikuwa wanakasirishwa na kauli za Winnie Mandela ambaye alikuwa anashutumu Serikali ya ANC kwa kuwasahau watu weusi walio pigana kufa na kupona kuiweka madarakani lakini anaona miaka karibu ishirini tangu wapate uhuru bado hali ya Wafrica ni duni sana, wengi wao wanaendelea kuishi kwenye slums, hawana umeme wala maji ya bomba - Winnie yuko outspoken sana katika suala hili na wanachi wengi wanamuhunga mkono - chukulia mfano wa leo pale uwanjani walipo kuwa wanataja jina la Winnie uwanja ulikuwa unalipuka kwa vifijo na makofi lakini sio kwa Graca, hata Zuma alizomewa - kwa nini?
Inavyo semekana kama winne yuko nyuma ya bwana mdogo Julius malema na ndiyo maana magwiji wa siasa wa ANC wanatumia kete ya usaliti kama fimbo ya kumchapia winne.
 
Inavyo semekana kama winne yuko nyuma ya bwana mdogo Julius malema na ndiyo maana magwiji wa siasa wa ANC wanatumia kete ya usaliti kama fimbo ya kumchapia winne.
Well said mkuu, inavyo onekana mambo sio shwali ndani ya chama cha ANC, inaonekana kuna makundi ndani ya chama wanao pingana - hii sio dalili nzuri kwa mstakhabali wa chama, wasipo jirekebisha ANC itasambaratika within fifteen years kutokana na vices zifuatazo: Viongozi wake kuwa wabinafsi, mafisadi na wezi wa kutupwa wa mali za Umma! Wamewasahau kabisa Wafrica wenzao wamewagehuka na kuwa wakoloni mamboleo, Aibu kweli kweli!! Winnie bado namuona ni shujaa regardless ya mapungufu yake ya kibinadamu. ANC haitaki kuelezwa ukweli - juzi juzi hapa walikuwa wamekula njama ili Askofu Desmond TUTU asihudhulie mazishi ya Mzee Mandela - kisa, wanaogopa asije kulipuka na ku-usema ubovu wa uongozi wa ANC mbele ya waombolezaji; viongozi wengi wa Kiafrica wako hivyo - hawapendi kokusolewa wanajiona ndio wenye hati miliki ya kuwamulia raia walio wengi waishi vipi! Hawajali haki za binadamu, wanajiona ni Miungu watu.
 
Back
Top Bottom