Obama ana Hasira na Winnie?

Obama ana Hasira na Winnie?

Nitofautiane nanyi woote, Mandela ameshakufa, kwa mujibu wa kiapo cha ndoa tayari kifo kishawatenganisha, ile hati ya ndoa imeisha thamani. anabaki kuwa graca na huyu hayati mandela, sasa kwa kuwa huyu Mandela enzi za uhai wake alikwishaapa kuwa mume wa winnie, kwa sababu zao binafsi wakaamua kutengana haifuti ukweli kuwa once upon a time hawa watu walikuwa mtu na mkewe.

kwa hiyo basi kwa kuwa Mandela amekufa, wale aliopata kututangazia hadharani kuwa ni wake zake wanakuwa wajane wake. Enzi za uhai wake akimwita x-wife, zama za umauti anakuwa widow wake full stop.

KAMA ILITOKEA MNAVYOSIMULIA, BASI WAMEMNYANYASA WINNIE.
 
Nimejiuliza hilo swali nimeshindwa kupata jibu! Kwa sababu Obama amemtaja Graca katika hotuba yake lakini siyo Winnie na pia alipomaliza hotuba yake akampa pole Graca, tena kwa hug, isipokuwa Winnie ingawa akina mama hao walikuwa wamekaa karibu sana! Was it that questionable integrity on the part of Winnie?

K-Boko katika hili wewe hujui lolote mpaka uambiwe au hili neno "protokali" limekufelisha, wenzio wametumia sayansi ya lugha kukupiga chenga.
 
Last edited by a moderator:
Na Madiba kumuoa mke wa best ake inamaana alikua akimzimia toka kitambo!!hahahahah
 
Nimejiuliza hilo swali nimeshindwa kupata jibu! Kwa sababu Obama amemtaja Graca katika hotuba yake lakini siyo Winnie na pia alipomaliza hotuba yake akampa pole Graca, tena kwa hug, isipokuwa Winnie ingawa akina mama hao walikuwa wamekaa karibu sana! Was it that questionable integrity on the part of Winnie?

Acha mke apate hadhi yake. Graca ndio alikuwa mkewe mpaka mauti yalipomkuta. Pia Obama alienda msibani na si kwenye sherehe za ukombozi wa S.A.
 
Winnie ni kama changudoa tu na ilivyo anaweza hata kunyimwa nafasi ya kuweka shada la maua wakati wa mazishi
 
Rais Zuma amemtaja!

Mimi binafsi siungi mkono tabia chafu za Winnie kama binadamu, lakini baadhi bado wanauthamini mchango wake katika struggles za apartheid South Africa, nao tusiwapuuze sana--democracy at work!

Mmesahau Winnie aliamua kula raha na kijana mdogo wa miaka 32 aliyekuwa mwanasheria wa ANC na alimletea TATA MADIBA kiburi alipomshauri asiende safari ya Ulaya?
Alilewa penzi la kijana hivyo HASTAHILI kupata heshima ya Mandela.
Asante Obama na wenzako kwa kuendelea kumfunza adabu Winnie!
 
Winnie ni kama changudoa tu na ilivyo anaweza hata kunyimwa nafasi ya kuweka shada la maua wakati wa mazishi

Acha hizo hata kama ni siwez vumilia miaka 27 yote nisifanye labda kama ni mgonjwa!winnie alichokosea ni baada ya Mandela kutoka gerezani na kuendelea kumsaliti,lakin Mandela alijua alikua anapigiwa mkewe wakati yupo gerezan hilo alisamehe
Lakin alivyogundua kuwa mkewe bado anaendelea kule ndipo alipoamua maamuz mazito
 
Mandela hakuamini msemo wa kuchapiwa ni siri ya ndani.......!Alisamehe yoote lakini kuchapiwa mhhhhhhhh!!!!Inaumaaaaaa
 
Winnie hawezi kuwa mfano wa kuigwa..alitenda uzinzi akiwa kwenye ndoa so hawezi kuwa mfano hata kidogo
 
Sasa mlitegemea hiyo miaka 27 aliyokuwa jela Winnie afe kisabuni?
 
sijui hapa unataka kumaanisha nini? Kama unataka kusema mzee madiba nae hakuwa ametulia kama Winnie basi utakuwa umepotoka sana, katika maisha ya utu uzima na huru Mandela alioa mara 3, ndoa yake ya kwanza na Evelyn na waliachana kutokana na kuhitirafiana kiitikadi, Dini ya mashahidi wa Yehova ya Evelyn ilikuwa hairuhusu kujihusisha na siasa hivyo Mandela hakuwa na jinsi. Akamuoa Winnie ambae alimsaliti akiwa jela na hata baada ya kutoka gerezani tena kwa kijana mdogo. Hivyo nae wakatalikiana. Ndipo alipomua Graca!
Utaona kuoa na kuacha kwa Mandela kulikuwa na sababu za msingi na wala si vinginevyo!

Bahati mbaya wanaume wote wa Kiafrika wakiacha mke au wakitaka kuongeza mwingine hawakosi sababu za udhaifu wa mke wa kwanza. Kwahiyo sishangai haya. Hata hivyo sidhani kuwa sababu kubwa ya kumwacha Winnie ni uzinifu wake. Hii ni sababu ya public consumption, lakini siyo sababu mahsusi.
 
K-Boko katika hili wewe hujui lolote mpaka uambiwe au hili neno "protokali" limekufelisha, wenzio wametumia sayansi ya lugha kukupiga chenga.

Nimeingia JF baada ya kuvutiwa na 'uchokozaji fikra' uliomo humu! Umeninyaka Jogi?
 
Back
Top Bottom