Oa mwanamke mwenye elimu

Oa mwanamke mwenye elimu

Maisha ni mtazamo wa mtu, hapa lets say uoe mwanamke mwenye maono au mtazamo chanya katika maisha

Mfano mama ambae anaeka kipaumbele makuzi ya wanae. Including elimu, afya etc huyu anamtazamo chanya

Na kuna wale wanadekeza na kulea watoto kimayai mayai hawa most wanakua hawana maono ya kesho

So elimu ya mama i think inachukua asilimia ndogo sana
Kimara Stationary 20200819_105219.jpg

The way nakuzoom Palina wangu😘😘
 
  • Kicheko
Reactions: 511
Daah! inanipa ukakasi sana asee
Form 4 failure sidhani ka atapenda yaliyotokea kwake yajirudie kwa. Wanae ndo maana most wana struggle na watoto wao wasiwe kama wao

Hawa wasomi sasa things are different kutegemea na background aliyopitia
 
Tofautisha kati ya madarasa na elimu.

La saba pia msomi ila ana madarasa machache ukimlinganisha na WA kidato Cha nne.

Kidato Cha nne naye ana madarasa machache kwa Binti wa kidato Cha sita.

Huyu Cha sita kwa Vyuo vikuu naye Cha mtoto tu.

Hivi nataka kusema nini ila utagundua elimu ni tofauti na madarasa hivyo saka mwenye elimu sio idadi ya madarasa aliyopitia
 
Form 4 failure sidhani ka atapenda yaliyotokea kwake yajirudie kwa. Wanae ndo maana most wana struggle na watoto wao wasiwe kama wao

Hawa wasomi sasa things are different kutegemea na background aliyopitia
but i think the intelligence pass genetically, sasa kama hazikuwemo kwa mama mtoto atazitoa wapi?
 
Hamna mtihani mgumu sana kama kuchagua mke yaani kuna sometimes unatamani kuanza maisha ya ndoa ila huyo mwenzako sasa unayempata kisanga.

Ktk maboko yote usithubutu kuoa mke asiye na hofu ya Mungu, asiyekuwa na akili za maisha (utafutaji).Kuna wanawake ni la Saba ila hata ukimkabidhi fedha,anajua kuitunza na kuizalisha,anaheshim fedha na hababishwi na trending hizi material things (fashion na simu nk).Ila type hizi zipo chache, demu anaweza kukuomba elfu 20 ya kusuka, ukamtumia 50 baada ya siku mbili anakuomba efu 5 ya vocha ,sasa kama huyu hata awe nana degree hafai kuwa mke.

Nina mwanangu kaoa dem form ila yule binti ni hustler hakuna na alikuwa anamuwezesha mwanagu kipindi hana issues na kipindi hiko wapo kwenye uchumba.Sasa jamaa sasa hivi mambo yame mnyookea, hela anamkabizi mke anazungusha kwenye biashara zao familia.

Ukija kwetu si wengine demu unamtongoza asubuhi, jioni ana hela ya kula,kodi,king'amuzi hajalipa,luku imeisha, mdogo wake kameza shoka nk,sometimes basi wengine wanatuona tupo single sio kwamba hatutaki kuoa tatizo tunokutana nao.

Wenyewe ndio wanakwambia kumpiga mizinga mwanaume ndio,kipimo cha kujua kama mwanaume wana hela na siku hizi kuna michezo mara vikoba bado anataka presha zake za vikoba na michezo anayocheza uibebe ww na husiombe demu wako ndio awe kijumbe,mana vijumbe wengi wanatabia ya kujikopesha hela za watu za michezo ila uwezo wa kulipa hawana.

Halafu hamna mahusiano eti mama akiwa na elimu labda degree na kuendelea watoto watakuwa hivyo hivyo, kuna wazee kibao wana elimu ila watoto zao wapo hovyo,hivi vitu unaweza kuvijenga kupitia malezi ufuatiliaji na mazingira utakayo yajenga kama mzazi.
 
Mimi mama yangu la nne (60s huko) na tena mjane since aged 27 na elimu yangu na mimi ya kuunga unga tu ila nimetoboa kuliko ndugu zangu waliosomeshwa int schools siku hizi naona kwao vinakaliwa vikao kusuluhisha gomvi za ndugu kwa ndugu wakitaka urithi mama yao akiwa bado hai.

Huwa natamani kujua elimu za wazazi wa wale wote wanaoonekana kama wamesoma sana,doctors engineers professors etc ili niamini kwamba akili zinarithishwa.mke atafutwe kwa kigezo cha kujua maisha,heshima kwa mume na wale wanaomzunguka mama/baba mkwe pamoja na kujua angalao kusahihisha homework za watoto mengine yataji-set yenyewe.
 
Ni kweli lakini at least anakuwa ana kitu flani kichwani tofauti na ambaye hajafika kabisa

Mkuu mimi najihusisha na masuala ya watoto..naona kabisa ni namna gani baadhi ya wanaume wameta hasara kubwa katika suala zima malezi ya msingi ya watoto wao

Na asilimia kubwa ya hao wanaume wameoa darasa la saba A na B

Be careful mkuu..choose wisely
Dah mkuu this is rude! 😅

Hebu tujadili vizuri labda kila mtu atatoka na kitu hapa, akili inarithishwa? Akili ni genetical? Je kuna cases za wazazi wawili wenye akili wakazaa mtoto kilaza? Hapa lazima tutambue tofauti kati ya mtoto kilaza na mtoto asiye elewa kwasababu labda ana tatizo linalohusiana na zile tunaita “learning difficulties” sijui kama neno liko sahihi.

Na je vipi ile theory inayosema watoto wote huzaliwa wakiwa empty (tabular rasa) Ndiposa ubongo wa mtoto huanza kujazwa vitu kidogo kidogo na mazingira ndio yataamua mtoto yupi awe smart na yupi awe mzito.

Je kuna case ya wazazi wawili vilaza (kwa vipimo vya kitaaluma) ikatokea wakazaa katoto kako smart?

Naomba nimkaribishe Dr Lizzy na wengineo tujadili haya maswali walau kwa ufupi.
 
Nilitamani nikuonyeshe mama fulani amezaa na wanaume watatu wote professionals !!! kuna injinia, daktari na mwanasheria na akafanikiwa kuzaa watoto na kila mmoja wa hao wanaume watoto wote walisoma na wa mwisho kisomi ni daktari.
Mama hadi leo ukimwambia andika ' a' mnagombana japo kusoma anaweza kidogo.
Wakati fulani lilia amani tu kwenye ndoa mengine yana settle kirahisi sana mkiwa na amani.
Nadhani huyo mama ana akili ni vile labda hajapata bahati ya kupita katika mfumo wa elimu rasmi.

Kuna wale watu hawajui kuandika kwenye karatasi ila ukimpa smartphone anaweza kutype hawa huwa wana nini? Wanakuwa hawajui kuandika lakini wanajua kusoma au hawajui kuumba herufi, i’m confused.
 
Mtu wakuzaa nae watoto lazima achaguliwe kwa umakini, bila hivyo unaweza juta sana mbeleni.

Ila kufika Form 4 sio kigezo maana hata kilaza anaweza akafika.
Utafika mbali Sana daktari.

Watu wasichokielewa ni kuwa akili za darasani ni tofauti kabisa na za maisha.

Kuwa na uwezo wa kutoboa form foo haimaanishi wewe ni mzuri kiakili zaidi ya ambae hakusoma kabisa.
 
Back
Top Bottom