BaaaaasiKwani Elimu lazima nadhani huo ni ujinga Elimu ya bongo ni upuuzi Mimi nashauri mtu atafute Mwanamke mwenye akili na sio Elimu yetu ya ku-claim kiima na kiarifu.
Nimeipenda sana hii line.Wengine tumezaliwa na wamama ambao hawakusoma hata darasa moja lakini wametukuza na tumefika mbali sana na tunawashukuru wametufikisha kwenye mafanikio.
Sijui unamaanisha nini unaposema atakavokuwa mke ndio atakavokuwa mtoto??
Sent from my SM-T285 using JamiiForums mobile app
Kuna ule upumbavu wa ndani/tabia ya mtu huwa hauondoki hata kwa elimu ndio maana unaweza kutana na mtu msomi lakini anayoyafanya utastaajabu ni upuuzi mtupu hata mtu ambae hakufika shule ana afadhali.Akili ya darasani ni tofauti na ya maisha ya kawaida, utakuwa mwanaume anajivunia elimu lakini maisha anayoishi au vitu anavyovifanya ukiambiwa huyu mtu mwenye elimu yake zakutosha mpaka unamuogopa, njoo sasa kwenye maisha ya nyumbani mbuzi si mbuzi ,ng'ombe si ng'ombe ndama si ndama unabaki kushika kichwa, mie nazani na malezi toka kwa wazazi yanachangia, mtoto darasani pia apate elimu ya maisha ya kawaida ,na akili ya kuzaliwa nimuhimu sana( Mungu anahusika)
100%Kuna ule upumbavu wa ndani/tabia ya mtu huwa hauondoki hata kwa elimu ndio maana unaweza kutana na mtu msomi lakini anayoyafanya utastaajabu ni upuuzi mtupu hata mtu ambae hakufika shule ana afadhali.
Akili ya Maisha hayafundishwi shule na hiki kinafanya mzani ubalansi. Nakubaliana nawe malezi nayo huchangia kwa kiasi kikubwa utimamu wa mtu.