Nyumba za kupanga majanga sometimes

Nyumba za kupanga majanga sometimes

Kwa hiyo wewe ulitakaje?

Utumie choo, alafu kudeki wahusike wengine?
 
Hapana, huyu bwana si mstaarabu katika matumizi ya vyoo.
Kama umeelewa, mama mwenye nyumba anataka huyu bwana aone tabu yakusafisha ili ajifunze kutumia kistaarabu ndio maana mama kakataa huyo mwamba kununua vifaa, anataka ASAFISHE choo.

Watu wa hivi huwa:-
Hawamwagi maji wakikojoa
Wakitoka haja kubwa wanamwaga maji machache mzigo hauendi
Hawahakikishi ile mistari ya kinyesi inayobaki kwenye sink imeondoka
Wakikojoa hawalengi tundu, choo kizima mikojo tuu.
Wanaingia na viatu vinamatope nakuyaacha bila kuyamwagia maji.
Wakikuta maji hamna/ hayatoki wanaacha mizigo yao hapo na kuondoka, hawajishuhulishi kutafuta maji.

Sio lazima yawe yote haya, ila lazima kuna yanayomuhusu.
[emoji3][emoji3][emoji3][emoji3]
Kwa maana nyingine wapangaji wenzake wamemchomea kwa mazahausi, mazahausi kaapa kumfundisha ustaarabu wa chooni kijana wake

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mi nilipanga nyumba yenye vyumba 8 - vinne kila upande pale magomeni miaka hiyo, nyumba haikuwa na dari - vyumba vitatu walipanga mabinti na vingine 2 tulipanga vijana afu vingine vitatu walitumia mama mwenye nyumba maana alikuwa na familia. -- sasa aiseee yaliyokuwa nashuhudia mule si mchezo... mengine ni kero mengine yanahamasishaa....

Mkuu hebu tupe hayo ya kuhamasisha kwanza[emoji3]
 
Sasa mkuu unataka we uwe unatumia tu choo wanadeki wengine mwamba. Kununua mafagio sio ishu, kila mtu anaweza kununua mafagio na sabuni, kwani bei gani. Kila mtu akinunua mafagio yatajifagia yenyewe?

Sometimes vitu vingine kuamua tu mkuu. Kudeki choo unachotumia mwenyewe wala sio uduanzi. Siku ya zamu yako Amka mapema deki oga sepa zako
Kufanya usafi muhimu Sana,

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Una akili ndogo sana we jamaa, hiko choo hukitumii? Unataka nani akusafishie wewe uje utumie tu. Ukiona hiyo ni kero, kapange chumba master, hakuna mtu hata siku moja atakuja kukuletea habari za usafi wa choo.
 
Hii nyumba niliyopanga mama mwenye nyumba anaishi hapa hapa, kuna kitu kinanikwaza mno

Wiki iliyopita narudi gheto akaniita akaniambia kuna ratiba ya kudeki choo nikamwambia sawa haina shida lakin mimi kutokana na mishe zangu naondoka mapema sana saa 11 alfajiri siwezi kudeki nitakuwa nanunua vifaa kama ufagio na sabuni n.k, lakini mama mwenye nyumba amekazanaa amenyooka na mimi nideki chooni
Kodi ikiisha nasepa mapema tu, kuishi na mama mwenye nyumba tabu
Wewe unazingua Yani mtu amekupangisha hafu unataka akufanyie usafi, usafi muhimu , wewe Ni sawa na huyu mpangaji wangu yani tokea mke wake aondoke hajawahi fanya usafi ,hapa nafikiria kumtimua , miezi miwili sasa, kwamba mke wangu awe anamfanyia usafi, huu ni upumbavu inabidi ufanye usafi au mtafute mtu wa kukufanyia usafi ndo uwe unamlipa.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Sijakataa lakin nilimuomba kutokana na pilika pilika zangu asubuh nikikurupuka nakuwaga fasta...lakin ameshakataa sasa najidamka mapemaaa nadeki... kodi ikiisha nihame...maana nachelewa kutoka
Mbona mimi nilipanga nyumba ambayo mwenye nyumba hayupo tulikuwa wapangaji tu na usafi tulipangiana ratiba ,

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Unaweza kumlipa mtu akakufanyia hyo kazi mbona simple tu,au unampa hela yeye kama anaweza kufanya au wapangaji wengine akikataa na hapo basi ana lake jambo
 
Sasa mkuu unataka we uwe unatumia tu choo wanadeki wengine mwamba. Kununua mafagio sio ishu, kila mtu anaweza kununua mafagio na sabuni, kwani bei gani. Kila mtu akinunua mafagio yatajifagia yenyewe?

Sometimes vitu vingine kuamua tu mkuu. Kudeki choo unachotumia mwenyewe wala sio uduanzi. Siku ya zamu yako Amka mapema deki oga sepa zako

Halafu hawa wanunua mafagio ndo wachafuaji wazuri sana wa choo. Maana yeye akishanunua fagio na sabuni kamaliza. Akitoka zake huko kalewa anakojoa hovyo hovyo humo chooni kisa yeye hadeki [emoji42]. Mkiamka asubuhi choo haitamaniki. Mama mwenye nyumba yuko sahihi kabisa.
 
Inavyo elekea hata usafi wa mazingira ya chumba chako unafanya kwa bahati
 
Kiukweli naishi na mother house ila ndiyo kila mtu busy na mambo yake, ni salamu tu na stories kidogo,kuhusu usafi alisema atasimamia shoo zote za usafi ila tutachangia kidogo so kwangu it's ok kabisa.

Na anatujali wapangaji wake kipindi cha covid na kujifukiza alikua anaandaa mchanganyiko anatuamsha asubuhi tujifukize, akiona kimya umechelewa kuamka maybe anakuita ajue unaendeleaje isijekua umezidiwa humo ndani. [emoji122]

Nakumbuka siku ile alitugongea[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji16][emoji16][emoji16][emoji16][emoji16][emoji16][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji16][emoji16][emoji16][emoji16][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji16][emoji16][emoji16][emoji16][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji847][emoji847][emoji847][emoji847][emoji847][emoji847][emoji847][emoji847][emoji2226][emoji2226][emoji2226][emoji2226]
 
Usijali mpe pesa atadeki. Anataka pesa.
Yaliwahi kunikuta ila Mungu mkubwa sasa nina nyumba nikitembelea ile nyumba naiona kama choo tu nashangaa niliwezaje kuishi nyumba mbaya ile.
Yule mwenye nyumba nilimtafuna baada ya kuhama.
Nyumba ilikuwa ya urithi
 
Mpaka nafikiria kuhama ujue huko kote nshapita...nishaomba niwe natoa hela ila wamegoma
Huyo mama mwenye nyumba wako mwambie " mama moyo wangu u dhaifu kila nikuonapo, najisikia niingie chumbani kwako"
Akija juu, mwambie unamaanisha unamuogopa, asipokuja juu Anza kukagua shanga zake
 
Wewe tafuta mtu humo humo kama mko wengi mwachie hata 5000 per week anasfisha on your behalf
 
Nyongeza. Aongeze bidii kutafta hela aupukane na vyoo na mabafu ya kushare, umaskini wako ndio una kufanya uone una onewa kumbe ni kautaratibu hata huko unako taka kuhamia.
AMEKUPATA vzriii kabsa
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom