Nyumba za kupanga majanga sometimes

Nyumba za kupanga majanga sometimes

Mwanakulipata

JF-Expert Member
Joined
Jul 17, 2018
Posts
718
Reaction score
1,203
Hii nyumba niliyopanga mama mwenye nyumba anaishi hapa hapa, kuna kitu kinanikwaza mno

Wiki iliyopita narudi gheto akaniita akaniambia kuna ratiba ya kudeki choo nikamwambia sawa haina shida lakin mimi kutokana na mishe zangu naondoka mapema sana saa 11 alfajiri siwezi kudeki nitakuwa nanunua vifaa kama ufagio na sabuni n.k, lakini mama mwenye nyumba amekazanaa amenyooka na mimi nideki chooni
Kodi ikiisha nasepa mapema tu, kuishi na mama mwenye nyumba tabu
 
Sasa mkuu unataka we uwe unatumia tu choo wanadeki wengine mwamba. Kununua mafagio sio ishu, kila mtu anaweza kununua mafagio na sabuni, kwani bei gani. Kila mtu akinunua mafagio yatajifagia yenyewe?

Sometimes vitu vingine kuamua tu mkuu. Kudeki choo unachotumia mwenyewe wala sio uduanzi. Siku ya zamu yako Amka mapema deki oga sepa zako
 
Kiukweli naishi na mother house ila ndiyo kila mtu busy na mambo yake, ni salamu tu na stories kidogo,kuhusu usafi alisema atasimamia shoo zote za usafi ila tutachangia kidogo so kwangu it's ok kabisa.

Na anatujali wapangaji wake kipindi cha covid na kujifukiza alikua anaandaa mchanganyiko anatuamsha asubuhi tujifukize, akiona kimya umechelewa kuamka maybe anakuita ajue unaendeleaje isijekua umezidiwa humo ndani. 👏
 
Sasa mkuu unataka we uwe unatumia tu choo wanadeki wengine mwamba. Kununua mafagio sio ishu, kila mtu anaweza kununua mafagio na sabuni, kwani bei gani. Kila mtu akinunua mafagio yatajifagia yenyewe?

Sometimes vitu vingine kuamua tu mkuu. Kudeki choo unachotumia mwenyewe wala sio uduanzi. Siku ya zamu yako Amka mapema deki oga sepa zako
Sijakataa lakin nilimuomba kutokana na pilika pilika zangu asubuh nikikurupuka nakuwaga fasta...lakin ameshakataa sasa najidamka mapemaaa nadeki... kodi ikiisha nihame...maana nachelewa kutoka
 
Kiukweli naishi na mother house ila ndiyo kila mtu busy na mambo yake, ni salamu tu na stories kidogo,kuhusu usafi alisema atasimamia shoo zote za usafi ila tutachangia kidogo so kwangu it's ok kabisa.

Na anatujali wapangaji wake kipindi cha covid na kujifukiza alikua anaandaa mchanganyiko anatuamsha asubuhi tujifukize, akiona kimya umechelewa kuamka maybe anakuita ajue unaendeleaje isijekua umezidiwa humo ndani. [emoji122]
Hii nzuri aisee...basi ata ukimwambia nitachangia hela ya usafi yeye anataka nidekiii tu [emoji706][emoji706][emoji706]
 
Sijakataa lakin nilimuomba kutokana na pilika pilika zangu asubuh nikikurupuka nakuwaga fasta...lakin ameshakataa sasa najidamka mapemaaa nadeki... kodi ikiisha nihame...maana nachelewa kutoka
Duh basi tu huyo mama si mwelewa si hata angekuambia uwe unachangia kiasi fulani kama hataki ununue hiyo mifagio na dawa.😬
 
Hahahahaa.

Vituko vya upangaji haviepukiki, vumilia mkuu. Hata huku unakotaka kuhamia unaweza kukuta vimbwanga vya hatari zaidi ya sasa.

Au tafuta chumba self-contained
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom