Nyuma ya pazia Bunge live

hii serikali ya ajabu sana yaani inataka iungwe mkono na wananchi huku haitaki wakisikie inachopanga kukitekeleza pamoja nao.
sijajua ni GENIUS GANI kaishauri kufanya huu uvunjifu wa haki ya kupata habari mchana kweupe.
washauri wa CCM ni wa kiwango cha chini mno.
 

ni vema mwananchi mwenyewe akachuja mbivu na mbichi
 
hawa jamaa wakae wakijua kuwa ule ukumbi ni wetu tuna haki ya kusikia na kuona wanachokifanya mle ndani, kama hawataki kuonyesha bunge haina maana ya wao kuendelea kukaa mle heri tukaufunge ukumbi wetu. watafute vichaka vya kufanyia kazi zao ni vichakani pekee ambapo watu hufanya kazi mafichoni.
 
ni vema mwananchi mwenyewe akachuja mbivu na mbichi

Halafu hawa wanaoendesha bunge kijima ndio wanawaongopea wananchi eti Tanzania itakuwa nchi ya viwanda. Ni kipi kinachowafanya wajadili hayo mambo mazuri kwa kificho?
 
hakuna kazi halali inayoweza kufanywa kwa kificho wao wanafanya kazi gani humo ndani? yaani kujadili masuala ya wananchi tuyafanye behind closed doors?
 
Fanyezi kazi kusikiliza Bonge hakutasaidia chochote kwa maisha ya wanamchi wa kawaida
 
hii serikali ya ajabu sana yaani inataka iungwe mkono na wananchi huku haitaki wakisikie inachopanga kukitekeleza pamoja nao.
sijajua ni GENIUS GANI kaishauri kufanya huu uvunjifu wa haki ya kupata habari mchana kweupe.

tatizo mwenezi wa chama kawa waziri wa habari,bado anaendeleza mbinu za fitna alizokuwa anafanya akiwa katibu mwenezi.Kajisahau na Magufuli anamwangalia tu
 
Halafu hawa wanaoendesha bunge kijima ndio wanawaongopea wananchi eti Tanzania itakuwa nchi ya viwanda. Ni kipi kinachowafanya wajadili hayo mambo mazuri kwa kificho?

wanachojaribu kufanya ndio kinawashushia heshima tofauti na wanavyofanya.
 
Ni hivii wanajua itakuwa ni aibu kwa serikali kwa kuwa wabunge wa chama chetu hawajazoea kuikosoa serikali. Leo wabunge watawala wanaweza pinga hoja fulani kesho Mkulu anatangaza kumtumbua muhusika ambaye wabunge wa CHAMA walimtetea kwa nguvu zote. Nadhani Hapa mkulu anataka kurekebisha kitu....labda akiona wabunge wake wameshajielewa anaweza akaondoa marufuku hiyo...
 
Ndiyo maana enzi za mzee wa chama kimoja mpaka chakula tulikaa foleni.

naona unataka kupoza machungu kwa kuhamishia mada kwa Nyerere,haya daraja la kigamboni lilishapewa jina nyerere.Najua uliumia sana,asante kwa kutambua mchango wa upinzani.
 
Fanyezi kazi kusikiliza Bonge hakutasaidia chochote kwa maisha ya wanamchi wa kawaida

Kwa nini tusizime kabisa vituo vya television mpaka jioni wakati tunapokuwa tumerudi makazini? Huoni hata hao wanaoonyesha vipindi wakati wakazi ni kama wanapoteza muda?
 
Fanyezi kazi kusikiliza Bonge hakutasaidia chochote kwa maisha ya wanamchi wa kawaida

Hizi akili nyingine huwa nashindwa kuzielewa,kusikiliza bunge maana yake hufanyi kazi?Sitashangaa siku ya uchaguzi ukija kusema,kafanyeni kazi kwani kupiga kura hakutawasaidia chochote.
 
ni jambo la ajabu sana watu wazima tena kuna wanaume kabisa wanalilia kuangalia tv. kuna watu humu itakua wananyanganyana remote na wake zao na watoto.
 
ni zamu ya wabunge wa chama chetu kudai posho na kupiga usingizi. masikini watanzania...
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…