Kwanza Kabisa nichukue muda huu kukupongeza kwa kazi nzuri unayoifanya, mimi kama mzalendo kwa badhi ya mambo naridhika sana, usitetereke katika msimamo wako ila naomba uelewe kuwa yapo baadhi ya mambo yanatia hofu utendaji wako wa kazi.
Giza ndani ya bunge-Hili ni jambo ambalo linatia hofu sana katika utoaji wa habari katika awamu ya tano, ukiwa unajinasibu kuwa muwazi lakini serikali yako inaonekana kuwa kinyume na yale unayosimama na kuyahubiri, tunashindwa kuelewa serikali inayohubiri uhuru iweje leo igeuke na kuweka mambo gizani?
Mheshimiwa najua uko busy sana, nadhan kuna kitu kinatengenenezwa nyuma ya pazia, kuna mambo ynafichwa na sijui kama ni sahihi katika kuyafanya haya, mtambue fika kuwa hakuna siri chini ya jua, naelewa manafilter some of information zisifike kwa wananchi but this is totally unacceptable,wananchi tulikupa dhamana ya kuleta utawala ulio huru na haki, unaminya haki ya kuwaruuhusu wananchi kuwashuhudia wawakilishi wao? kwa nini unayafanya haya na kwa manufaa ya wananchi? au kwa manufaa ya nani?
Tunaomba kujulishwa kilicho nyuma ya pazia.