Naona umeamua kukurupuka tu kuijibu hoja yangu bila kusoma nilichoaandika, kilichokufanya uijibu hoja yangu ni hizo video. Mimi nimetaka kujua ni kwanini wabunge wanakomalia issue ya bunge kuonyeshwa live mada ambayo ilishapita muda wa miezi kama mitatu. Na nikasema badala ya wao kupigania mambo ya muhimu kama ya kufichua madhambi ya serikali wanapoteza muda kujadili mambo ya bunge kuonyeshwa live. Hiyo video niliyoiweka ya bunge la uingereza ni ku confirm hoja yangu kuwa shughuli muhimu tu wenzetu wanaonyesha live na ni kwa muda wa dakika 30 kama hiyo video inavyoonekana. Kama mtu anataka kuona yalijiri bungeni hua kuna channel initwa BBC Parliament hiyo inaonyesha matukio ya mabunge tofauti ya UK, kama vile House of Common (MPS), House of Lords ( ma Peers), Scottish Parliament, wales n.k Hapa kwetu TBC ingekua na Channel kama hiyo kuonyesha hata kinachojili Baraza la wawakilishi na siyo kuonyesha Dodoma tu. Ndiyo lengo langu mimi sipo katika siasa kama wewe na wenzako wanapigania kutetea serikali sababu wao ni ccm ama kutetea kina Peter Msigwa sababu wapo UKAWA. Matukio Muhimu kama ya kusomwa kwa Budget, rais kuhutbia Bunge lazima yawe Live lakini ukiniambia wabunge kujadili budget za serikali TBC waache mambo mengine watuonyeshe Bunge tu huo ni upuuzi tu na zaidi wengi mnataka Bunge lionyeshwe live si kwasababu mnataka kusikia nini kinajadiliwa bali mnataka kuona vituko, sasa kwanini serikali iingie hasara ya kutuonyesha vituko?????