Nyoka Mkubwa avuka barabara

Nyoka Mkubwa avuka barabara

Kama unaendesha Pikipiki au Baiskeli unakutana na nyoka mkubwa kama huyu itabidi usimamae apite ndipo na wewe upite kwa usalama wako.

Sasa si atakufanya kitoweo? Hapo ni Kupiga u-turn na kurudi ulikotoka kwa speed ya Hali ya juu Kuokoa nafsi Tena unahairisha safari kabisa maana huenda anafanya timing ukajua katokomea kumbe yupo around.
 
Njia nyingine wanatumia hawa watu wanaokamata nyoka kwa ajili ya masomo na kazi nyingine ,ila unatakiwa uwe mjasiri..Wanatumia kioo kikubwa ,nyoka anagonga kioo akifikiri anakugonga wewe mpaka anachoka.
Hicho kioo lazima kiwe na ubora unaostahili lasivyo tunaweza kula ubwabwa wa matanga....
 
Huyo ni chatu, na anaweza kukua zaidi ya hapo. Aliyemzidi kwa urefu ni anaconda peke yake ambaye hayuko kwetu Africa.
 
hakuna madhara,labda akikosea kugonga,agonge bega,lakini uwa tunajiprotect,nakumbuka dodoma mpwapwa koboko alimgonga mtu na kufa hapo hapo na mwili ulibadilika rangi na kuwa blue,akikugonga ni bora ukae chini ukitembea poison inasafiri faster mwili wote,pia hapo hapo mpwapwa kikombo road koboko aliwahi kugonga kioo cha gari cha mbele akidhania watu wale wapo nje,kile kioo akikupasuka ila kilichange rangi na kuwa blue na kama ukungu,sumu yake uwa inakimbilia kwenye brain na masozi.ni nyoka mkali sana,akishituliwa uwa anagonga hata mti au jiwe.

Kipo kikawa cha bluu!dah kumbee!
 
Ni kweli mkuu nyoka aina ya black mamba(koboko) ni hatari ila hawezi kuwa hatari zaidi ya simba
1:Akikugonga una dakika 20 hadi 30 za kupata matibabu sahihi au unakufa,
2:Akikukomalia anakukimbiza na anakupata sio lazima ajiviringishe sehemu ili akugonge
3:Nyoka wengi akikugonga anaacha meno ila huyo bwana haachi
4:Kiboko yake ni nguchiro,anapiga chenga mpaka nyoka anachoka halafu anamuwahi kichwa
Dk 20 au 30 ni cobra!
 
Huyo sio Koboko ni Chatu. Koboko anaweza kuwa mrefu lakini siyo mkubwa kiasi hiki. Huyu ndiye nyoka wa pili kwa ukubwa duniani asiye na sumu wa group la Constrictors ( wa kwanza kwa ukubwa ni Anaconda then chatu au Python).

Chatu anaweza kuwa na urefu hadi mita 6 na katika urefu huo anauwezo wa kummeza adult. Huyo aliyeko pichani ni mkubwa sana akikukuta kwenye mtego wake anakukamata na hautoki labda upate msaada wa haraka.
 
Ni kweli mkuu nyoka aina ya black mamba(koboko) ni hatari ila hawezi kuwa hatari zaidi ya simba
1:Akikugonga una dakika 20 hadi 30 za kupata matibabu sahihi au unakufa,
2:Akikukomalia anakukimbiza na anakupata sio lazima ajiviringishe sehemu ili akugonge
3:Nyoka wengi akikugonga anaacha meno ila huyo bwana haachi
4:Kiboko yake ni nguchiro,anapiga chenga mpaka nyoka anachoka halafu anamuwahi kichwa

Hivi ni kweli kuwa nyoka haoni vizuri kama sisi tunavyoona usiku na mchana
 
Back
Top Bottom